< Luke 20 >

1 And yt fortuned in one of those dayes as he taught the people in the temple and preached the gospell: the hye prestes and the scribes came with the elders
Siku moja, Yesu alipokuwa akifundisha watu Hekaluni na kuhubiri habari njema, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria, pamoja na wazee wa watu wakamjia.
2 and spake vnto him sayinge. Tell vs by what auctorite thou doest these thinges? Ether who is he yt gave ye this auctorite?
Wakamuuliza, “Tuambie, unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ni nani aliyekupa mamlaka haya?”
3 He answered and saide vnto the: I also will axe you a questio and answer me.
Akawajibu, “Nami nitawauliza swali.
4 The baptyme of Iohn: was it from heaven or of men?
Je, ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni au kwa wanadamu?”
5 And they thought with in them selves sayinge: yf we shall saye from heave: he will saye: why then beleved ye him not?
Wakahojiana wao kwa wao wakisema, “Kama tukisema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atatuuliza, ‘Mbona hamkumwamini?’
6 But and yf we shall saye of men all ye people will stone vs. For they be persuaded that Ihon is a Prophet.
Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ watu wote watatupiga mawe, kwa sababu wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii.”
7 And they answered that they coulde not tell whence it was.
Basi wakajibu, “Hatujui ulikotoka.”
8 And Iesus sayde vnto them: nether tell I you by what auctorite I do these thinges.
Yesu akawaambia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda mambo haya.”
9 Then begane he to put forthe to the people this similitude. A certayne man planted a vyneyarde and let it forthe to fermers and went him selfe into a straunge countre for a greate season.
Akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima fulani, kisha akasafiri kwa muda mrefu.
10 And when the tyme was come he sent a servaut to his tennauntes that they shuld geve him of the frutes of the vyneyarde. And the tennauntes dyd bet him and sent him awaye empty.
Wakati wa mavuno ulipofika, akamtuma mtumishi wake kwa hao wapangaji ili wampe sehemu ya mavuno ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga, wakamfukuza mikono mitupu.
11 And agayne he sent yet another servaunt. And they dyd bet him and foule entreated him also and sent him awaye emptye.
Akamtuma mtumishi mwingine, huyo naye wakampiga, wakamfanyia mambo ya aibu na kumfukuza.
12 Moreover he sent the thyrde to and him they wouded and cast out.
Bado akamtuma na mwingine wa tatu, huyu pia wakamjeruhi na kumtupa nje ya shamba.
13 Then sayde the lorde of the vyneyarde: what shall I do? I will sende my deare sonne him peradventure they will reverence when they se him.
“Basi yule mwenye shamba la mizabibu akasema, ‘Nifanye nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa, huenda yeye watamheshimu.’
14 But when the fermers sawe him they thought in them selves sayinge: this is the heyre come let vs kyll him that the inheritaunce maye be oures.
“Lakini wale wapangaji walipomwona, wakasemezana wao kwa wao. Wakasema, ‘Huyu ndiye mrithi. Basi na tumuue ili urithi uwe wetu.’
15 And they cast him out of the vyneyarde and kylled him. Now what shall the Lorde of the vyneyarde do vnto them?
Kwa hiyo wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamuua.” “Sasa basi yule mwenye shamba la mizabibu atawafanyia nini wapangaji hawa?
16 He will come and destroye those fermers and will let out his vyneyarde to other. When they hearde that they sayde: God forbyd.
Atakuja na kuwaua hao wapangaji, na kuwapa wapangaji wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia hayo wakasema, “Mungu apishie mbali jambo hili lisitokee!”
17 And he behelde them and sayde: what meaneth this then yt is wrytten: The stone that the bylders refused the same is made ye heed corner stone?
Lakini Yesu akawakazia macho, akasema, “Basi ni nini maana ya yale yaliyoandikwa: “‘Jiwe walilolikataa waashi, limekuwa jiwe kuu la pembeni’?
18 whosoever stomble at that stone shalbe broken: but on whosoever it faul vpon it wyll grynde him to powder.
Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia atasagwa kabisa.”
19 And the hye Prestes and the Scribes the same howre went about to laye hondes on him but they feared the people. For they perceaved that he had spoken this similitude agaynst them.
Walimu wa sheria na viongozi wa makuhani wakatafuta njia ya kumkamata mara moja, kwa sababu walifahamu kwamba amesema mfano huo kwa ajili yao. Lakini waliwaogopa watu.
20 And they watched him and sent forth spies which shuld fayne them selves perfecte to take him in his wordes and to delyvre him vnto the power and auctorite of the debite.
Kwa hiyo wakawa wanamchunguza na kutuma wapelelezi waliojifanya kuwa wenye haki ili wapate kumtega kwa maneno asemayo, ili wamtie katika uwezo na mamlaka ya mtawala.
21 And they axed him sayinge: Master we knowe that thou sayest and teachest ryght nother cosiderest thou eny manes degre but teachest the waye of God truly.
Hivyo wale wapelelezi wakamuuliza, “Mwalimu, tunajua unasema na kufundisha yaliyo kweli wala humpendelei mtu, bali wafundisha njia ya Mungu katika kweli.
22 Ys it laufull for vs to geve Cesar tribute or no?
Je, ni halali sisi kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
23 He perceaved their craftynes and sayde vnto them: why tept ye me?
Lakini Yesu akatambua hila yao, kwa hiyo akawaambia,
24 Shewe me a peny. Whose ymage and superscripcio hath it? They answered and sayde: Cesars.
“Nionyesheni dinari. Je, sura hii na maandishi haya yaliyoko juu yake ni vya nani?”
25 And he sayde vnto them: Geve then vnto Cesar that which belongeth vnto Cesar: and to God that which pertayneth to God.
Wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Akawaambia, “Basi mpeni Kaisari kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho cha Mungu.”
26 And they coulde not reprove his sayinge before the people. But they marvayled at his answer and helde their peace.
Wakashindwa kumkamata kwa yale aliyokuwa amesema hadharani. Nao wakashangazwa mno na majibu yake, wakanyamaza kimya.
27 Then came to him certayne of the Saduces which denye that ther is eny resurreccio. And they axed him
Baadhi ya Masadukayo, wale wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu, wakamjia Yesu na kumuuliza,
28 sayinge: Master Moses wrote vnto vs if eny mannes brother dye havinge a wyfe and the same dye with out yssue: that then his brother shuld take his wyfe and reyse vp seede vnto his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu wa mtu akifa na kumwacha mkewe bila mtoto, basi huyo mtu inampasa amwoe huyo mjane ili amzalie ndugu yake watoto.
29 Ther were seven brethren and the fyrste toke a wyfe and dyed with out children.
Basi palikuwepo ndugu saba. Yule wa kwanza akaoa, akafa bila kuzaa mtoto.
30 And the seconde toke the wyfe and he dyed chyldlesse.
Kisha yule wa pili akamwoa huyo mjane, naye akafa bila mtoto,
31 And the thyrde toke her and in lyke wyse the resydue of the seven and leeft no chyldren be hynde them and dyed.
naye wa tatu pia akamwoa. Vivyo hivyo ndugu wote saba wakawa wamemwoa huyo mwanamke, na wote wakafa pasipo yeyote kupata mtoto.
32 Last of all the woma dyed also.
Mwishowe, yule mwanamke naye akafa.
33 Now at the resurreccio whose wyfe of them shall she be? For seven had her to wyfe.
Sasa basi, siku ya ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani, maana aliolewa na ndugu wote saba?”
34 Iesus answered and sayde vnto them. The chyldre of this worlde mary wyves and are maryed (aiōn g165)
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
35 but they which shalbe made worthy to enioye that worlde and the resurreccion from deeth nether mary wyves nether are maryed (aiōn g165)
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
36 nor yet can dye eny moare. For they are equall vnto the angels: and are the sonnes of God in as moche as they are the chyldre of the resurreccion.
Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
37 And that the deed shall ryse agayne even Moses signified besydes the busshe when he sayde: the Lorde God of Adraham and the God of Isaac and the God of Iacob.
Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
38 For he is not the God of the deed but of them which live. For all live in him.
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
39 Then certayne of the Pharises answered and sayde: Master thou hast well sayde.
Baadhi ya walimu wa sheria wakasema, “Mwalimu, umesema sawasawa kabisa!”
40 And after that durst they not axe him eny question at all.
Baada ya hayo hakuna mtu aliyethubutu kumuuliza maswali tena.
41 Then sayde he vnto them: how saye they that Christ is Davids sonne?
Kisha Yesu akawaambia, “Imekuwaje basi wao husema Kristoni Mwana wa Daudi?
42 And David him selfe sayth in the boke of the Psalmes: The Lorde sayde vnto my Lorde syt on my right honde
Daudi mwenyewe anasema katika Kitabu cha Zaburi: “‘Bwana alimwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume,
43 tyll I make thine enemys thy fothe stole.
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”’
44 Seinge David calleth him Lorde: How is he then his sonne.
Ikiwa Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ basi atakuwaje mwanawe?”
45 Then in the audience of all the people he sayde vnto his disciples
Wakati watu wote walikuwa wanamsikiliza, Yesu akawaambia wanafunzi wake,
46 beware of the Scribes which desyre to goo in longe clothinge: and love gretynges in the markets and the hyest seates in the synagoges and chefe roumes at feastes
“Jihadharini na walimu wa sheria. Wao hupenda kutembea wakiwa wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa kwa heshima masokoni. Hupenda kukaa kwenye viti vya mbele katika masinagogi, na kukaa kwenye nafasi za heshima katika karamu.
47 which devoure widdowes houses and that vnder a coloure of longe prayinge: the same shall receave greater damnacion.
Wao hula nyumba za wajane, na ili waonekane kuwa wema, wanasali sala ndefu. Watu kama hawa watapata hukumu iliyo kuu sana.”

< Luke 20 >