< Luke 13 >

1 Ther were present at the same season that shewed him of ye Galileas whose bloude Pylate mengled with their awne sacrifice.
Kwa wakataihuo huo, kulikuwa na baadhi watu waliomtaarifu juu ya Wagalilaya ambao Pilato aliwaua na kuchanganya damu yao na sadaka zao.
2 And Iesus answered and sayde vnto them: Suppose ye that these Galileans were greater synners then all the other Galileas because they suffred suche punisshmet?
Yesu akajibu na kuwaambia, “Je mwadhani kuwa Wagalilaya hao walikuwa na dhambi kuliko Wagalilaya wengine wote ndiyo maana wamepatwa na mabaya hayo?
3 I tell you naye: but except ye repent ye shall all in lyke wyse perysshe.
Hapana, nawaambia, lakini msipotubu, nanyi mtaangamia vivyo hivyo.
4 Or those. xviii. apon which ye toure in Syloe fell and slewe the thinke ye that they were synners above all men yt dwell in Ierusalem?
Au wale watu kumi na nane katika Siloamu ambao mnara ulianguka na kuwaua, mnafikiri wao walikuwa wenye dhambi zaidi kuliko watu wengine katika Yerusalemu?
5 I tell you naye: But excepte ye repent ye all shall lykewyse perisshe.
Hapana, mimi nasema, lakini kama msipotubu, ninyi nyote pia mtaangamia.
6 He put forthe this similiiude A certayne man had a fygge tree planted in his veneyarde and he came and sought frute theron and founde none.
Yesu aliwaambia mfano huu, “Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake na alikwenda kutafuta matunda juu yake lakini hakupata.
7 Then sayde he to ye dresser of his vyneyarde: Beholde this thre yeare have I come and sought frute in this fygge tree and fynde none: cut it doune: why combreth it the grounde?
Akamwambia mtunza bustani, 'Tazama, kwa miaka mitatu nimekuja na kujaribu kutafuta matunda kwenye mtini huu lakini sikupata. Uukate. Kwani ulete uharibifu wa ardhi?
8 And he answered and sayde vnto him: lorde let it alone this yeare also till I digge rounde aboute it and doge it to se
Mtunza bustani akajibu na kusema, 'uache mwaka huu ili niupalilie na kuweka mbolea juu yake.
9 whether it will beare frute: and if it beare not then after yt cut it doune
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, ni vema; lakini kama hautazaa, uukate!”'
10 And he taught in one of their sinagoges on ye saboth dayes.
Sasa Yesu alikuwa akifundisha katika mojawapo ya Masinagogi wakati wa Sabato.
11 And beholde ther was a woma which had a sprete of infirmite. xviii. yeares: and was bowed to gether and coulde not lifte vp hersilfe at all.
Tazama, alikuwepo mama mmoja ambaye kwa miaka kumi na minane alikuwa na rohomchafu wa udhaifu, na yeye alikuwa amepinda na hana uwezo kabisa wa kusimama.
12 When Iesus sawe her he called her to him and sayde to her: woman thou arte delyvered from thy disease.
Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umewekwa huru kutoka kwenye udhaifu wako.”
13 And he layde his hondes on her and immediatly she was made strayght and glorified God.
Akaweka mikono yake juu yake, na mara mwili wake akajinyoosha na akamtukuza Mungu.
14 And the ruler of the sinagoge answered with indignacion (be cause that Iesus had healed on the saboth daye) and sayde vnto the people. Ther are sixe dayes in which men ought to worke: in them come and be healed and not on the saboth daye.
Lakini mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo mtawala akajibu akawambia makutano, “Kuna siku sita ambazo ni lazima kufanya kazi. Njoni kuponywa basi, si katika siku ya Sabato. '
15 Then answered him the Lorde and sayd: Ypocrite doth not eache one of you on the saboth daye lowse his oxe or his asse from the stall and leade him to the water?
Bwana akamjibu na akasema, “wanafiki! Hakuna kila mmoja wenu kufungua punda wako au ng'ombe kutoka zizini na kuwaongoza kumpeleka kunywa siku ya Sabato?
16 And ought not this doughter of Abraham whom Sathan hath bounde loo. xviii. yeares be lowsed from this bonde on the saboth daye?
Hivyo pia binti wa Abrahamu, ambaye Shetani amemfunga kwa miaka kumi na minane, je haikumpasa kifungo chake kisifunguliwe siku ya sabato?”
17 And when he thus sayde all his adversaries were ashamed and all the people reioysed on all the excellent dedes that were done by him.
Alipokuwa akisema maneno hayo, wale wote waliompinga waliona aibu, bali makutano wote wa wengine walishangilia kwa ajili ya mambo ya ajabu aliyotenda.
18 Then sayde he: What is the kyngdome of God lyke? or wherto shall I compare it?
Yesu akasema, “Ufalme wa Mungu unafanana na nini, na naweza kuulinganisha na nini?
19 It is lyke a grayne of mustard seede which a man toke and sowed in his garden: and it grewe and wexed a greate tree and the foules of the ayer made nestes in the braunches of it.
Ni kama mbegu ya haradari aliyoitwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake, na ikamea ikawa mti mkubwa, na ndege wa mbinguni wakajenga viota vyao katika matawi yake.
20 And agayne he sayde: wher vnto shall I lyken ye kyngdome of god?
Tena akasema, “Niufananishe na nini ufalme wa Mungu?
21 it is lyke leve which a woman toke and hidde in thre busshels of floure tyll all was thorow levended.
Ni kama chachu ambayo mwanamke aliichukua na kuchanganyakwenye vipimo vitatu vya unga hata ukaumuka.”
22 And he went thorow all maner of cities and tounes teachinge and iorneyinge towardes Ierusalem.
Yesu alitembelea kila mji na kijiji njiani akielekea Yerusalemu na kuwafundisha.
23 Then sayde one vnto him: Lorde are ther feawe that shalbe saved? And he sayde vnto them:
Mtu mmoja akauliza, “Bwana, ni watu wachache tu watakaookolewa?” Hivyo akawaambia,
24 stryve with youre selves to enter in at ye strayte gate: For many I saye vnto you will seke to enter in and shall not be able.
“Jitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba, kwa sababu wengi watajaribu na hawataweza kuingia.
25 When the good man of ye housse is rysen vp and hath shett to the dore ye shall beginne to stonde with out and to knocke at the dore sayinge: Lorde lorde open vnto vs: and he shall answer and saye vnto you: I knowe you not whence ye are.
Mara baada ya mmiliki wa nyumba kusimama na kufunga mlango, basi mtasimama nje na kupiga hodi mlangoni na kusema, Bwana, Bwana, tufungulie yeye atajibu na kuwaambia, siwajui ninyi wala mtokako.'
26 Then shall ye begin to saye. We have eaten in thy presence and dronke and thou hast taught in oure stretes.
Ndipo mtasema, Tulikula na kunywa mbele yako na wewe ulifundisha katika mitaa yetu.”
27 And he shall saye: I tell you I knowe you not whence ye are: departe from me all ye workers of iniquite.
Lakini yeye atawajibu, `nawaambia, siwajui mtokako, ondokeni kwangu, ninyi watenda maovu!'
28 There shalbe wepinge and gnasshinge of teth when ye shall se Abraham and Isaac and Iacob and all the prophetes in the kyngdom of God and youre selves thrust oute at dores.
Kutakuwa na kilio na kusaga meno wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka, Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mumetupwa nje.
29 And they shall come from the eest and from the weest and from the northe and from the southe and shall syt doune in the kyngdome of God.
Watafika kutoka Mashariki, Magharibi, Kaskazini na Kusini, na kupumzika katika meza ya chakula cha jioni katika ufalme wa Mungu.
30 And beholde ther are last which shalbe fyrst: And ther are fyrst which shalbe last.
Na tambua hili, wa mwisho ni wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho.”
31 The same daye there came certayne of the pharises and sayd vnto him: Get the out of the waye and departe hence: for Herode will kyll ye.
Muda mfupi baadaye, baadhi ya Mafarisayo walikuja na kumwambia, “Nenda na ondoka hapa kwa sababu Herode anataka kukuua.”
32 And he sayd vnto them. Goo ye and tell that foxe beholde I cast oute devyls and heale the people to daye and to morowe and the third daye I make an ende.
Yesu akasema, “Nendeni mkamwambie yule mbweha, `Tazama, ninawafukuza pepo na kufanya uponyaji leo na kesho, na siku ya tatu nitatimiza lengo langu.
33 Neverthelesse I must walke todaye and tomorowe and the daye folowinge: For it cannot be that a Prophet perishe eny other where save at Ierusalem.
Katika hali yoyote, ni muhimu kwa ajili yangu kuendelea leo, kesho, na siku iliyofuata, kwa vile haikubaliki kumuua nabii mbali na Yerusalemu.
34 O Ierusalem Ierusalem which kyllest prophetes and stonest them that are sent to ye: how often wolde I have gadered thy childre to gedder as the hen gathereth her nest vnder her wynges but ye wolde not.
Yerusalemu, Yerusalemu, nani anawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu. Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wenu kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini humkulitaka hili.
35 Beholde youre habitacion shalbe left vnto you desolate. For I tell you ye shall not se me vntill the tyme come that ye shall saye blessed is he that commeth in the name of the Lorde.
Tazama, nyumba yako imetelekezwa. Nami nawaambia, hamuwezi kuniona hata mtakaposema 'Amebarikiwa huyo ajaye kwa jina la Bwana.'”

< Luke 13 >