< Luke 12 >

1 As ther gadered together an innumerable multitude of people (in so moche that they trood one another) he began to saye vnto his disciples: Fyrst of all beware of the leve of the Pharises which is ypocrisy.
Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2 For ther is no thinge covered that shall not be vncovered: nether hyd that shall not be knowen.
Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3 For whatsoever ye have spoken in in darknes: that same shalbe hearde in light. And that which ye have spoken in the the eare eve in secret places shalbe preached even on the toppe of the housses.
Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4 I saye vnto you my fredes: Be not afrayde of them that kyll the body and after that have no moare that they can do.
“Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5 But I will shewe you whom ye shall feare. Feare him which after he hath killed hath power to cast into hell. Ye I saye vnto you him feare. (Geenna g1067)
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna g1067)
6 Are not five sparowes bought for two farthinges? And yet not one of them is forgotten of God.
Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7 Also even the very heres of youre heedes are nombred. Feare not therfore: ye are moare of value then many sparowes.
Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8 I saye vnto you: Whosoever confesseth me before men eve him shall ye sonne of man confesse also before ye angels of God.
“Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9 And he that denyeth me before men: shalbe denyed before ye angels of God.
Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10 And whosoever speaketh a worde agaynst ye sonne of ma it shalbe forgeven him. But vnto him yt blasphemeth the holy goost it shall not be forgeven.
“Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 When they bringe you vnto the synagoges and vnto the rulers and officers take no thought how or what thinge ye shall answer or what ye shall speake.
“Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12 For the holy goost shall teache you in the same houre what ye ought to saye.
Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
13 One of the company sayde vnto hym: Master byd my brother devide the enheritauce with me.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
14 And he sayde vnto him: Man who made me a iudge or a devider over you?
Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
15 Wherfore he sayde vnto them: take hede and beware of covetousnes. For no mannes lyfe stondeth in the aboundaunce of the thinges which he possesseth.
Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
16 And he put forth a similitude vnto them sayinge: The groude of a certayne riche ma brought forth frutes plenteously
Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17 and he thought in himsilfe sayinge: what shall I do? because I have noo roume where to bestowe my frutes?
Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18 And he sayde: This will I do. I will destroye my barnes and bilde greater and therin will I gadder all my frutes and my goodes:
Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19 and I will saye to my soule: Soule thou hast moch goodes layde vp in stoore for many yeares take thyne ease: eate drinke and be mery.
Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 But God sayde vnto him: Thou fole this night will they fetche awaye thy soule agayne from the. Then whose shall thoose thinges be which thou hast provyded?
Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
21 So is it with him that gadereth ryches and is not ryche in God.
Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
22 And he spake vnto his disciples: Therfore I saye vnto you: take no thought for youre lyfe what ye shall eate nether for youre body what ye shall put on.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23 The lyfe is moare then meate and the bodye is moare then rayment.
Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24 Considre the ravens for they nether sowe nor repe which nether have stoorehousse ner barne and yet God fedeth them. How moche are ye better then the foules.
Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25 Which of you with takynge thought can adde to his stature one cubit?
Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26 Yf ye then be not able to do that thinge which is least: why take ye thought for the remmaunt?
Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27 Considre the lylies how they growe: They laboure not: they spyn not: and yet I saye vnto you that Salomon in all this royalte was not clothed lyke to one of these.
Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28 Yf the grasse which is todaye in the felde and tomorowe shalbe cast into the fornace God so clothe: how moche moore will he clothe you o ye endued wt litell faith?
Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29 And axe not what ye shall eate or what ye shall drinke nether clyme ye vp an hye
“Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30 for all suche thinges the hethen people of the worlde seke for. Youre father knoweth that ye have nede of suche thinges.
Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31 Wherfore seke ye after the kyngedome of God and all these thinges shalbe ministred vnto you.
Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32 Feare not litell floocke for it is youre fathers pleasure to geve you a kingdome.
“Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33 Sell that ye have and geve almes. And make you bagges which wexe not olde and treasure that fayleth not in heaven where noo these commeth nether moth corrupteth.
Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34 For where youre treasure is there will youre hertes be also.
Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35 Let youre loynes be gerdde about and youre lightes brennynge
“Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 and ye youre selves lyke vnto men that wayte for their master when he will returne fro a weddinge: that assone as he cometh and knocketh they maye ope vnto him.
muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37 Happy are those servauntes which the Lorde when he cometh shall fynde wakynge. Verely I saye vnto you he will gerdde him selfe about and make them sit doune to meate and walke by and minister vnto them.
Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38 And yf he come in the seconde watche ye if he come in the thyrde watche and shall fynde them soo happy are those servauntes.
Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39 This vnderstonde that yf the good man of the housse knewe what houre ye these wolde come he wolde suerly watche: and not suffer his housse to be broken vp.
Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40 Be ye prepared therfore: for the sonne of man will come at an houre when ye thinke not.
Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
41 Then Peter sayde vnto him: Master tellest thou this similitude vnto vs or to all men?
Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
42 And the Lorde sayde: If there be any faith full servaut and wise whom his Lorde shall make ruler over his housholde to geve them their duetie of meate at due season:
Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43 happy is that servaunt whom his master when he cometh shall finde soo doinge.
Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Of a trueth I saye vnto you: that he will make him ruler over all that he hath.
Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45 But and yf the evyll servaunt shall saye in his hert: My master wyll differre his cominge and shall beginne to smyte the servauntes and maydens and to eate and drinke and to be dronken:
Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46 the Lorde of that servaunt will come in a daye when he thinketh not and at an houre when he is not ware and will devyde him and will geve him his rewarde with the vnbelevers.
bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47 The servaut that knewe his masters will and prepared not him selfe nether dyd accordinge to his will shalbe bete with many strypes.
Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48 But he that knewe not and yet dyd committe thinges worthy of strypes shalbe beaten with feawe strypes. For vnto whom moche is geven of him shalbe moche requyred. And to whom men moche commyt the moare of him will they axe.
Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49 I am come to sende fyre on erth: and what is my dysyre but that it were all redy kyndled?
“Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50 Not with stondinge I must de baptised with a baptyme: and how am I payned till it be ended?
Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51 Suppose ye that I am come to sende peace on erth? I tell you naye: but rather debate.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52 For fro hence forthe ther shalbe five in one housse devided thre agaynst two and two agaynst thre.
Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 The father shalbe devided agaynst the sonne and the sonne agaynst the father. The mother agaynst the doughter and the doughter agaynst the mother. The motereleawe agaynst hir doughterelawe and the doughterelawe agaynst hir motherelawe.
Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
54 Then sayde he to the people: when ye se a cloude ryse out of the west strayght waye ye saye: we shall have a shower and soo it is.
Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55 And when ye se the south wynde blow ye saye: we shall have heet and it cometh to passe.
Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56 Ypocrites ye can skyll of the fassion of the erth and of the skye: but what is ye cause that ye canot skyll of this time?
Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57 Ye and why iudge ye not of youre selves what is righte?
“Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58 Whill thou goest with thyne adversary to the ruler: as thou arte in the waye geve diligence that thou mayst be delivered fro him least he bringe the to the iudge and the iudge delyver the to the iaylar and the iaylar cast the in to preson.
Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59 I tell ye thou departest not thence tyll thou have made good ye vtmost myte.
Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”

< Luke 12 >