< Hebrews 2 >

1 Wherfore we ought to geve ye more hede to ye thinges we have herde lest we perysshe.
Kwa hiyo ni lazima tuweke kipaumbele zaidi kwa yale tuliyosikia, ili kwamba tusije tukatengwa mbali nayo.
2 For yf the worde which was spoke by angels was stedfast: so yt every trasgressio and disobediece receaved a iust recopece to rewarde:
Kwa maana ikiwa ujumbe uliozungumzwa na malaika ni halali, na kila kosa na uasi hupokea adhabu tu,
3 how shall we escape yf we despyse so great saluacio which at ye fyrst bega to be preached of ye lorde him silfe and afterwarde was cofermed vnto vs warde by the ye hearde it
tutapataje kuepuka kama tusipojali wokovu huu mkuu? —wokuvu ambao kwanza ulitangazwa na Bwana na kuthibitishwa kwetu na wale waliousikia.
4 god bearynge witnes therto bothe with sygnes and wonders also and with divers miracles and gyftes of the holy gooste accordynge to his awne will.
Mungu pia aliuthibitisha kwa ishara, maajabu, na kwa matendo makuu mbalimbali, na kwa zawadi za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake mwenyewe.
5 He hath not vnto the angels put in subieccion the worlde to come where of we speake.
Mungu hakuuweka ulimwengu ujao, ambao tunaongelea habari zake, chini ya malaika.
6 But one in a certayne place witnessed sayinge. What is man that thou arte myndfull of him?
Badala yake, mtu fulani ameshuhudia mahali fulani akisema, “Mtu ni nani, hata uweze kumkumbuka? Au mwana wa mtu, hata umtunze?
7 After thou haddest for a season made him lower then the angels: thou crounedst him with honour and glory and hast set him above the workes of thy hondes.
mtu kuwa mdogo kuliko malaika; umemvika taji ya utukufu na heshima. (Zingatia: Katika nakala halisi za kwanza, mstari huu haupo. “Na umemuweka juu ya kazi ya mikono yako.)
8 Thou hast put all thynges in subieccion vnder his fete. In that he put all thynges vnder him he left nothynge that is not put vnder him.
Umeweka kila kitu chini ya miguu yake.” Kwa hiyo Mungu ameweka kila kitu chini ya mtu. Hakuacha kitu chochote ambacho hakiko chini yake. Lakini sasa hivi hatuoni bado kila kitu kikiwa chini yake.
9 Neverthelesse we yet se not all thynges subdued but him yt was made lesse the ye angelles: we se that it was Iesus which is crouned with glory and honour for the sofferinge of death: that he by the grace of god shulde tast of deeth for all men.
Hata hivyo, tunaona ambaye alikuwa amefanywa kwa muda, chini kuliko malaika—Yesu, ambaye, kwa sababu ya mateso yake na kifo chake, amevikwa taji ya utukufu na heshima. Hivyo sasa kwa neema ya Mungu, Yesu ameonja kifo kwa ajili ya kila mtu.
10 For it becam him for whom are all thynges and by whom are all thynges after that he had brought many sonnes vnto glory that he shuld make the lorde of their saluacion parfect thorow sofferynge.
Ilikuwa sahihi kwamba Mungu, kwa sababu kila kitu kipo kwa ajili yake na kupitia yeye, alipaswa kuwaleta watoto wengi katika utukufu, na kwamba alipaswa kumfanya kiongozi katika wokovu wao kuwa mkamilifu kupitia mateso yake.
11 For he that sanctifieth and they which are sanctified are all of one. For which causes sake he is not ashamde to call the brethren
Kwa maana wote wawili yule anayeweka wakfu na wale ambao wanawekwa wakfu, wote wanatoka kwenye asili moja, Mungu. Kwa sababu hii yule anayewaweka wakfu kwa Mungu haoni aibu kuwaita ndugu.
12 sayinge: I will declare thy name vnto my brethren and in the myddes of the congregacio will I prayse the.
Anasema, “Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu, nitaimba kuhusu wewe kutoka ndani ya kusanyiko.”
13 And agayne: I will put my trust in him. And agayne. beholde here am I and the children which god hath geven me.
Tena asema, “Nitaamini katika yeye.” Na tena, “Tazama, hapa nipo na watoto ambao Mungu amenipa.”
14 For as moche then as the children were parte takers of flesshe and bloud he also him silfe lyke wyse toke parte with them for to put doune thorow deth him that had lordshippe over deeth that is to saye the devyll
Kwa hiyo, kwa kuwa watoto wa Mungu wote hushiriki mwili na damu, kadhalika Yesu alishiriki vitu vilevile, ili kwamba kupitia kifo apate kumdhohofisha yule ambaye ana mamlaka juu ya mauti, ambaye ni ibilisi.
15 and yt he myght delyver the which thorow feare of deeth were all their lyfetyme in dauger of bondage.
Hii ilikuwa hivyo ili awaweke huru wale wote ambao kupitia hofu ya kifo waliishi maisha yao yote katika utumwa.
16 For he in no place taketh on him the angels: but the seede of Abraham taketh he on him.
Kwa hakika siyo malaika anaowasaidia. Badala yake, anawasaidia wazao wa Abraham.
17 Wherfore in all thynges it became him to be made lyke vnto his brethre that he myght be mercifull and a faythfull hye preste in thynges concernynge god for to pourge the peoples synnes.
Kwa hiyo, ilikuwa lazima yeye awe kama ndugu zake katika njia zote, ili aweze kuwa kuhani mkuu mwenye huruma na mwaminifu kwa vitu vya Mungu, na ili kwamba awe na uwezo wa kutoa msamaha kwa dhambi za watu.
18 For in that he him silfe suffered and was tempted he is able to sucker them that are tempted.
Kwa sababu Yesu mwenyewe ameteseka, na kujaribiwa, ana uwezo wa kuwasaidia wale wanaojaribiwa.

< Hebrews 2 >