< Hebrews 10 >

1 For the lawe which hath but the shadowe of good thynges to come and not the thynges in their awne fassion can never with ye sacryfises which they offer yere by yere continually make the comers thervnto parfayte.
Sheria ya Wayahudi si picha kamili ya mambo yale halisi: ni kivuli tu cha mema yanayokuja. Dhabihu zilezile hutolewa daima, mwaka baada ya mwaka. Sheria yawezaje, basi, kwa njia ya dhabihu hizo, kuwafanya wale wanaoabudu wawe wakamilifu?
2 For wolde not then those sacrifises have ceased to have bene offered because that the offerers once pourged shuld have had no moare conscieces of sinnes.
Kama hao watu wanaomwabudu Mungu wangekuwa wametakaswa dhambi zao kweli, hawangejisikia tena kuwa na dhambi, na dhabihu hizo zote zingekoma.
3 Neverthelesse in those sacrifises is ther mencion made of synnes every yeare.
Lakini dhabihu hizo hufanyika kila mwaka kuwakumbusha watu dhambi zao.
4 For it is vnpossible that the bloud of oxen and of gotes shuld take awaye synnes.
Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi.
5 Wherfore when he commeth into the worlde he sayth: Sacrifice and offeringe thou woldest not have: but a bodie hast thou ordeyned me.
Ndiyo maana Kristo alipokuwa anakuja ulimwenguni, alimwambia Mungu: “Hukutaka dhabihu wala sadaka, lakini umenitayarishia mwili.
6 In sacrifices and synne offerynges thou hast no lust.
Sadaka za kuteketezwa au za kuondoa dhambi hazikupendezi.
7 Then I sayde: Lo I come in the chefest of the boke it is written of me that I shuld doo thy will o god.
Hapo nikasema: Niko hapa ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.”
8 Above when he had sayed sacrifice and offerynge and burnt sacrifices and synne offerynges thou woldest not have nether hast alowed (which yet are offered by the lawe)
Kwanza alisema: “Hutaki, wala hupendezwi na dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za kuondoa dhambi.” Alisema hivyo ingawa sadaka hizi zote hutolewa kufuatana na Sheria.
9 and then sayde: Lo I come to do thy will o god: he taketh awaye the fyrst to stablisshe the latter.
Kisha akasema: “Niko hapa, ee Mungu, tayari kufanya mapenzi yako.” Hivyo Mungu alibatilisha dhabihu za zamani na mahali pake akaweka dhabihu nyingine moja.
10 By the which will we are sanctified by the offeringe of the body of Iesu Christe once for all.
Kwa kuwa Yesu Kristo alitimiza mapenzi ya Mungu, sisi tunatakaswa dhambi zetu kwa ile dhabihu ya mwili wake aliyotoa mara moja tu, ikatosha.
11 And every prest is redy dayly ministrynge and ofte tymes offereth one maner of offerynge which can never take awaye synnes.
Kila kuhani Myahudi humhudumia Mungu kila siku, akitoa dhabibu zilezile mara nyingi, dhabibu ambazo haziwezi kuondoa dhambi.
12 But this man after he had offered one sacrifyce for synnes sat him doune for ever on the right honde of god
Lakini Kristo alitoa dhabihu moja tu kwa ajili ya dhambi, dhabihu ifaayo milele, kisha akaketi upande wa kulia wa Mungu.
13 and from hence forth tarieth till his foes be made his fotestole.
Huko anangoja mpaka adui zake watakapowekwa kama kibao chini ya miguu yake.
14 For with one offerynge hath he made parfecte for ever them yt are sanctified.
Basi, kwa dhabihu yake moja tu, amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wanaotakaswa dhambi zao.
15 And ye holy goost also beareth vs recorde of this even when he tolde before:
Naye Roho Mtakatifu anatupa ushahidi wake. Kwanza anasema:
16 This is the testament that I will make vnto them after those dayes sayth the lorde. I will put my lawes in their hertes and in their mynde I will write them
“Hili ndilo agano nitakalofanya nao, katika siku zijazo, asema Bwana: Nitaweka sheria zangu mioyoni mwao, na kuziandika akilini mwao.”
17 and their synnes and iniquyties will I remember no moare.
Kisha akaongeza kusema: “Sitakumbuka tena dhambi zao, wala vitendo vyao vya uhalifu.”
18 And where remission of these thinges is there is no moare offerynge for synne.
Basi, dhambi zikisha ondolewa, hakutakuwa na haja tena ya kutoa dhabihu za kuondoa dhambi.
19 Seynge brethren that by the meanes of the bloud of Iesu we maye be bolde to enter into that holy place
Basi, ndugu, kwa damu ya Yesu tunapewa moyo thabiti wa kuingia Mahali Patakatifu.
20 by the newe and livynge waye which he hath prepared for vs through the vayle that is to saye by his flesshe.
Yeye ametufungulia njia mpya na yenye uzima kupitia lile pazia, yaani kwa njia ya mwili wake mwenyewe.
21 And seynge also that we have an hye prest which is ruler over ye housse of god
Basi, tunaye kuhani maarufu aliye na mamlaka juu ya nyumba ya Mungu.
22 let vs drawe nye with a true herte in a full fayth sprynckeled in oure hertes from an evyll conscience and wesshed in oure bodies with pure water
Kwa hiyo tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu na imani timilifu, kwa mioyo iliyotakaswa dhamiri mbaya, na kwa miili iliyosafishwa kwa maji safi.
23 and let vs kepe the profession of oure hope with oute waveringe (for he is faythfull that promysed)
Tushikilie imara tumaini lile tunalokiri, maana Mungu aliyefanya ahadi zake ni mwaminifu.
24 and let vs consyder one another to provoke vnto love and to good workes:
Tujitahidi kushughulikiana kwa ajili ya kuongezeana bidii ya kupendana na kutenda mema.
25 and let vs not forsake the felishippe that we have amoge oure selves as the maner of some is: but let vs exhorte one another and that so moche the more because ye se that the daye draweth nye.
Tusiache ile desturi ya kukutana pamoja, kama vile wengine wanavyofanya. Bali tunapaswa kusaidiana kwani, kama mwonavyo, Siku ile ya Bwana inakaribia.
26 For yf we synne willyngly after that we have receaved the knowledge of the trueth there remayneth no more sacrifice for synnes
Maana, tukiendelea kutenda dhambi makusudi baada ya kufahamu ukweli, hakuna dhabihu iwezayo kutolewa tena kwa ajili ya kuondoa dhambi.
27 but a fearfull lokynge for iudgement and violent fyre which shall devoure the adversaries
Linalobaki ni kungojea tu kwa hofu hukumu ya Mungu na moto mkali utakaowaangamiza wote wanaompinga.
28 He that despiseth Moses lawe dyeth with out mercy vnder two or thre witnesses.
Mtu yeyote asiyeitii Sheria ya Mose, huuawa bila ya huruma kukiwa na ushahidi wa watu wawili au watatu.
29 Of how moche sorer punyshment suppose ye shall he be counted worthy which treadeth vnderfote the sonne of god: and counteth the bloude of the testament as an vnholy thynge wherwith he was sanctified and doth dishonoure to the sprete of grace.
Je, mtu yule anayempuuza Mwana wa Mungu na kuidharau damu ya agano la Mungu iliyomtakasa, mtu anayemtukana Roho wa Mungu, anastahili kupata adhabu kali ya namna gani?
30 For we knowe him that hath sayde vengeaunce belongeth vnto me I will recompence sayth the lorde. And agayne: the lorde shall iudge his people.
Maana tunamfahamu yule aliyesema, “Mimi nitalipiza kisasi, mimi nitalipiza,” na ambaye alisema pia, “Bwana atawahukumu watu wake.”
31 It is a fearfull thynge to faule into the hondes of the livynge God.
Kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai ni jambo la kutisha mno!
32 Call to remebraunce the dayes that are passed in the which after ye had receaved light ye endured a greate fyght in adversities
Kumbukeni yaliyotokea siku zile za kwanza mlipoangaziwa mwanga wa Mungu. Ingawa siku zile mlipatwa na mateso mengi, ninyi mlistahimili.
33 partly whill all men wondred and gased at you for the shame and trioulacion that was done vnto you and partly whill ye became companyons of the which so passed their tyme.
Mara nyingine mlitukanwa na kufedheheshwa hadharani; mara nyingine mlikuwa radhi kuungana na wale walioteswa namna hiyohiyo.
34 For ye suffered also with my bondes and toke a worth the spoylynge of youre goodes and that with gladnes knowynge in youre selves how that ye had in heven a better and an endurynge substaunce
Mlishiriki mateso ya wafungwa, na mliponyang'anywa mali yenu mlistahimili kwa furaha, maana mlijua kwamba mnayo mali bora zaidi na ya kudumu milele.
35 Cast not awaye therfore youre confidence which hath great rewarde to recopence.
Basi, msipoteze uhodari wenu, maana utawapatieni tuzo kubwa.
36 For ye have nede of paciece that after ye have done ye will of god ye myght receave the promes.
Mnahitaji kuwa na uvumilivu, ili mweze kufanya anayotaka Mungu na kupokea kile alichoahidi.
37 For yet a very lytell whyle and he that shall come will come and will not tary.
Maana kama yasemavyo Maandiko: “Bado kidogo tu, na yule anayekuja, atakuja, wala hatakawia.
38 But the iust shall live by faith. And yf he withdrawe him silfe my soule shall have no pleasure in him.
Lakini mtu wangu aliye mwadilifu ataamini na kuishi; walakini akirudi nyuma, mimi sitapendezwa naye.”
39 We are not whiche withdrawe oure selves vnto dampnacio but partayne to fayth to the wynnynge of the soule.
Basi, sisi hatumo miongoni mwa wale wanaorudi nyuma na kupotea, ila sisi tunaamini na tunaokolewa.

< Hebrews 10 >