+ Hebrews 1 >

1 God in tyme past diversly and many wayes spake vnto the fathers by Prophetes:
Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
2 but in these last dayes he hath spoken vnto vs by his sonne whom he hath made heyre of all thinges: by who also he made the worlde. (aiōn g165)
lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote. (aiōn g165)
3 Which sonne beynge the brightnes of his glory and very ymage of his substance bearinge vp all thinges with the worde of his power hath in his awne person pourged oure synnes and is sitten on the right honde of the maiestie an hye
Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
4 and is more excellent then the angels in as moche as he hath by inheritaunce obteyned an excellenter name then have they.
Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
5 For vnto which of the angels sayde he ateny tyme: Thou arte my sonne this daye be gate I the? And agayne: I will be his father and he shalbe my sonne.
Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako.” Wala hakusema juu ya malaika yeyote: “Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu.”
6 And agayne whe he bringeth in the fyrst begotten sonne in to the worlde he sayth: And all the angels of God shall worshippe him.
Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: “Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu.”
7 And of the angels he sayth: He maketh his angels spretes and his ministres flammes of fyre.
Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: “Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
8 But vnto the sonne he sayth: God thy seate shalbe forever and ever. The cepter of thy kyngdome is a right cepter. (aiōn g165)
Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: “Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki. (aiōn g165)
9 Thou hast loved rightewesnes and hated iniquyte. Wherfore God which is thy God hath anoynted the with ye oyle of gladnes above thy felowes.
Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako.”
10 And thou Lorde in the begynninge hast layde the foundacion of the erth. And the heves are the workes of thy hondes.
Pia alisema: “Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
11 They shall perisshe but thou shalt endure. They all shall wexe olde as doth a garment:
Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
12 and as a vesture shalt thou chaunge them and they shalbe chaunged. But thou arte all wayes and thy yeres shall not fayle.
Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma.”
13 Vnto which of the angels sayde he at eny tyme? Sit on my ryght honde tyll I make thyne enemyes thy fote stole.
Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: “Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako.”
14 Are they not all mynistrynge spretes sent to minister for their sakes which shalbe heyres of salvacion?
Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.

+ Hebrews 1 >