< Genesis 37 >

1 And Iacob dwelt in the lande wherein his father was a straunger yt is to saye in the lande of Canaan.
Yakobo akaishi Kanaani katika nchi ambayo baba yake alikuwa ameishi.
2 And these are the generations of Iacob: when Ioseph was. xvij. yere olde he kepte shepe with his brethren and the lad was with the sonnes of Bilha and of Zilpha his fathers wyues. And he brought vnto their father an euyll saynge yt was of them.
Zifuatazo ni habari za Yakobo. Yosefu, kijana wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga makundi ya kondoo na mbuzi pamoja na ndugu zake wa mama wengine, yaani wana wa Bilha na wana wa Zilpa wake za baba yake, naye akawa akimletea baba yake taarifa mbaya kuhusu hao ndugu zake.
3 And Israel loued Ioseph more than all his childern because he begat hym in his olde age and he made him a coote of many coloures.
Basi, Israeli akampenda Yosefu kuliko yeyote miongoni mwa kaka zake, kwani ni mwanawe wa uzeeni, akamshonea joho lililorembwa vizuri sana.
4 When his brothren sawe that their father loued him more than all his brethern they hated him and coude not speke one kynde worde vnto him.
Ndugu zake walipoona kwamba baba yao anampenda Yosefu kuliko yeyote mwingine miongoni mwao, walimchukia na hawakusema naye neno lolote jema.
5 Moreouer Ioseph dreamed a dreawe and tolde it his brethren: wherfore they hated him yet the more.
Yosefu akaota ndoto, naye alipowaeleza ndugu zake, wakamchukia zaidi.
6 And he sayde vnto them heare I praye yow this dreame which I haue dreamed:
Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota:
7 Beholde we were makynge sheues in the felde: and loo my shefe arose and stode vpright and youres stode rounde aboute and made obeysaunce to my shefe.
Tulikuwa tukifunga miganda ya nafaka shambani, ghafula mganda wangu ukasimama wima, wakati miganda yenu ikiuzunguka na kuuinamia.”
8 Than sayde his brethren vnto him: what shalt thou be oure kynge or shalt thou reigne ouer us? And they hated hi yet the more because of his dreame and of his wordes.
Ndugu zake wakamwambia, “Wewe unakusudia kututawala? Hivi kweli wewe utatutawala sisi?” Wakaongeza kumchukia zaidi kwa sababu ya ndoto yake pamoja na yale aliyowaambia.
9 And he dreamed yet another dreame and told it his brethren saynge: beholde I haue had one dreame more: me thought the sonne and the moone and. xi. starres made obaysaunce to me.
Kisha akaota ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake akisema, “Sikilizeni, nimeota ndoto nyingine, wakati huu jua, mwezi na nyota kumi na moja zilikuwa zinanisujudia.”
10 And when he had told it vnto his father and his brethern his father rebuked him and sayde vnto him: what meaneth this dreame which thou hast dreamed: shall I and thy mother and thy brethren come and fall on the grounde before the?
Alipomwambia baba yake pamoja na ndugu zake, baba yake akamkemea akisema, “Ni ndoto gani hii uliyoota? Hivi kweli mama yako na mimi na ndugu zako tutakuja kukusujudia wewe hadi nchi?”
11 And his brethern hated him but his father noted the saynge.
Ndugu zake wakamwonea wivu, lakini baba yake akaliweka jambo hilo moyoni.
12 His brethren went to kepe their fathers shepe in Sichem
Basi, ndugu zake walikuwa wamekwenda kuchunga makundi ya baba yao karibu na Shekemu,
13 and Israell sayde vnto Ioseph: do not thy brethern kepe in Sichem? come that I may send ye to the. And he answered here am I
naye Israeli akamwambia Yosefu, “Kama ujuavyo, ndugu zako wanachunga makundi huko karibu na Shekemu. Njoo, nitakutuma kwao.” Yosefu akajibu, “Vema sana, niko tayari.”
14 And he sayde vnto him: goo and see whether it be well with thy brethren and the shepe and brynge me worde agayne: And sent him out of the vale of Hebron for to go to Sichem.
Kwa hiyo akamwambia, “Nenda uone kama mambo yote ni salama kwa ndugu zako na makundi, kisha uniletee habari.” Ndipo akamtuma Yosefu kutoka Bonde la Hebroni. Yosefu alipofika Shekemu,
15 And a certayne man founde him wandrynge out of his waye in the felde ad axed him what he soughte.
mtu mmoja akamkuta akizungukazunguka mashambani na akamuuliza, “Unatafuta nini?”
16 And he answered: I seke my brethren tell me I praye the where they kepe shepe
Akajibu, “Ninawatafuta ndugu zangu. Unaweza kuniambia wanachunga wapi makundi yao?”
17 And the man sayde they are departed hece for I herde them say let vs goo vnto Dothan. Thus went Ioseph after his brethren and founde them in Dothan.
Yule mtu akajibu, “Wamehama hapa. Nilisikia wakisema, ‘Twende Dothani.’” Kwa hiyo Yosefu akawafuatilia ndugu zake na kuwakuta karibu na Dothani.
18 And whe they sawe him a farr of before he came at them they toke councell agaynst him for to sley him
Ndugu zake walipomwona akiwa mbali, kabla hajawafikia, wakapanga shauri baya la kumuua.
19 and sayde one to another Beholde this dreamer cometh
Wakaambiana, “Yule mwota ndoto anakuja!
20 come now and let us sley him and cast him in to some pytt and let vs saye that sonne wiked beast hath deuoured him and let us see what his dreames wyll come to.
Njooni sasa, tumuue na kumtupa katika shimo mojawapo na tuseme kwamba mnyama mkali amemrarua. Kisha tutaona matokeo ya ndoto zake.”
21 When Ruben herde that he wet aboute to ryd him out of their handes and sayde let vs not kyll him.
Reubeni aliposikia jambo hili, akajaribu kumwokoa kutoka mikononi mwao akasema, “Tusiutoe uhai wake.
22 And Ruben sayde moreouer vnto them shed not his bloude but cast him in to this pytt that is in the wildernes and laye no handes vpon him: for he wolde haue rydd him out of their handes and delyuered him to his father agayne.
Tusimwage damu yoyote. Mtupeni katika shimo lililoko hapa jangwani, lakini msimguse.” Reubeni alisema hivyo ili amwokoe kutoka mikononi mwao, kisha amrudishe nyumbani kwa baba yake.
23 And as soone as Ioseph was come vnto his brethren they strypte him out of his gay coote that was vpon him
Kwa hiyo Yosefu alipowafikia ndugu zake, walimvua lile joho lake, lile joho lililorembwa vizuri alilokuwa amevaa.
24 and they toke him and cast him in to a pytt: But the pytt was emptie and had no water therein.
Kisha wakamchukua wakamtupa katika shimo. Wakati huo shimo lilikuwa tupu, halikuwa na maji ndani yake.
25 And they satt them doune to eate brede. And as they lyft vp their eyes and loked aboute there came a companye of Ismaelites from Gilead and their camels lade with spicery baulme and myrre and were goynge doune in to Egipte.
Walipokaa ili wale chakula chao, wakainua macho wakaona msafara wa Waishmaeli ukija kutoka Gileadi. Ngamia wao walikuwa wamepakizwa mizigo ya vikolezo, uvumba na manemane, nao walikuwa njiani kuvipeleka Misri.
26 Than sayde Iuda to his brethre what avayleth it that we sley oure brother and kepe his bloude secrett?
Yuda akawaambia ndugu zake, “Tutafaidi nini ikiwa tutamuua ndugu yetu na kuificha damu yake?
27 come on let vs sell him to the Ismaelites and let not oure handes be defyled vpon him: for he is oure brother and oure flesh. And his brethren were content.
Njooni, tumuuze kwa hawa Waishmaeli. Tusimguse, kwa kuwa hata hivyo yeye ni ndugu yetu, nyama yetu na damu yetu wenyewe.” Ndugu zake wakakubali.
28 Than as the Madianites marchaunt men passed by they drewe Ioseph out of the pytt and sold him vnto the Ismaelites for. xx. peces of syluer. And they brought him into Egipte.
Kwa hiyo wale wafanyabiashara Wamidiani walipofika pale, ndugu zake wakamtoa Yosefu kutoka kwenye lile shimo, na kumuuza kwa shekeli ishirini za fedha kwa wale Waishmaeli, ambao walimpeleka Misri.
29 And when Ruben came agayne vnto the pytt and founde not Ioseph there he rent his cloothes
Reubeni aliporudi kutazama kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hayupo, alirarua nguo zake.
30 and went agayne vnto his brethern saynge: the lad is not yonder and whether shall I goo?
Akawarudia ndugu zake na kusema, “Kijana hayuko mle! Nielekee wapi sasa?”
31 And they toke Iosephs coote ad kylled a goote and dypped the coote in the bloud.
Kisha wakalichukua lile joho la Yosefu, wakachinja mbuzi na kulichovya katika damu.
32 And they sent that gay coote and caused it to be brought vnto their father and sayd: This haue we founde: se whether it be thy sones coote or no.
Wakalichukua lile joho lililorembwa vizuri na kulipeleka kwa baba yao na kusema, “Tumeliokota hili joho. Uchunguze uone kama ni la mwanao.”
33 And he knewe it saynge: it is my sonnes coote a wicked beast hath deuoured him and Ioseph is rent in peces.
Baba yao akalitambua akasema, “Hili ni joho la mwanangu! Mnyama mkali amemrarua. Hakika Yosefu ameraruliwa vipande vipande.”
34 And Iacob rent his cloothes ad put sacke clothe aboute his loynes and sorowed for his sonne a longe season.
Kisha Yakobo akararua nguo zake, akavaa nguo ya gunia na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi.
35 Than came all his sonnes ad all his doughters to comforte him. And he wold not be comforted but sayde: I will go doune in to ye grave vnto my sonne mornynge. And thus his father wepte for him. (Sheol h7585)
Wanawe wote na binti zake wakaja kumfariji, lakini hakukubali kufarijiwa. Akasema, “Hapana, nitamwombolezea mwanangu mpaka nimfikie kaburini.” Kwa hiyo baba yake akaendelea kumlilia. (Sheol h7585)
36 And the Madianytes solde him in Egipte vnto Putiphar a lorde of Pharaos: and his chefe marshall.
Wakati ule ule, Wamidiani wakamuuza Yosefu huko Misri kwa Potifa, mmojawapo wa maafisa wa Farao, aliyekuwa mkuu wa ulinzi.

< Genesis 37 >