< Acts 11 >

1 And the Apostles and the brethren that were thorowout Iewry harde saye that the hethen had also receaved the worde of God.
Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
2 And when Peter was come vp to Ierusalem they of the circumcision reasoned wyth him
Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
3 sayinge: Thou wentest in to men vncircumcised and atest with them.
“Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
4 Then Peter began and expounded ye thinge in order to the sayinge:
Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
5 I was in the cyte of Ioppa prayinge and in a traunce I sawe a vision a certen vessell descende as it had bene a large lynnyn clothe let doune from hevin by the fower corners and it cam to me.
“Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
6 Into the which when I had fastened myn eyes I consydered and sawe fowerfoted beastes of ye erth and vermen and wormes and foules of the ayer.
Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 And I herde a voyce sayinge vnto me: aryse Peter sley and eate.
Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
8 And I sayd: God forbyd lorde for nothinge comen or vnclene hath at eny tyme entred into my mouth.
Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
9 But the voyce answered me agayne from heven cout not thou those thinges come which god hath clensed.
Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
10 And this was done thre tymes. And all were takin vp agayne into heven.
Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
11 And beholde immediatly ther were thre men come vnto the housse where I was sent from Cesarea vnto me.
Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
12 And the sprete sayde vnto me that I shuld go with them with out doutinge. Morover the sixe brethren accompanyed me: and we entred into the mas housse.
Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
13 And he shewed vs how he had sene an angell in his housse which stod and sayde to him: Send men to Ioppa and call for Symon named also Peter:
Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
14 he shall tell the wordes wherby both thou and all thyne housse shalbe saved.
Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
15 And as I begane to preach ye holy goost fell on them as he dyd on vs at the begynninge.
Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
16 Then came to my remembrauce ye wordes of the Lorde how he sayde: Iohn baptised with water but ye shalbe baptysed with the holy goost.
Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
17 For as moche then as God gave the lyke gyftes as he dyd vnto vs when we beleved on the Lorde Iesus Christ: what was I that I shuld have with stonde God?
Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
18 when they hearde this they helde their peace and gloryfied God sayinge: then hath God also to the gentyls graunted repentaunce vnto lyfe.
Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
19 They which were scattryd abroade thorow the affliccion that arose aboute Steven walked thorow oute tyll they came vnto Phenices and Cypers and Antioche preachynge ye worde to no man but vnto the Iewes only.
Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
20 Some of them were men of Cypers and Syrene which when they were come into Antioche spake vnto the Grekes and preched the Lorde Iesus.
Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
21 And the honde of the Lorde was with them and a greate nombre beleved and turned vnto the Lorde.
Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
22 Tydinges of these thinges came vnto ye eares of the congregacion which was in Ierusalem. And they sente forth Barnabas that he shuld go vnto Antioche.
Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 Which when he was come and had sene the grace of God was glad and exhorted them all that with purpose of hert they wolde continually cleave vnto ye Lorde.
Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
24 For he was a good man and full of the holy goost and of faythe: and moche people was added vnto the Lorde.
Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
25 Then departed Barnabas to Tarsus for to seke Saul.
Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
26 And when he had founde him he brought him vnto Antioche. And it chaunsed yt a whole yere they had their conversacion with the congregacio there and taught moche people: in so moche that the disciples of Antioche were the fyrst that were called Christen.
Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
27 In those dayes came Prophetes fro Ierusalem vnto Antioche.
Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
28 And ther stode vp one of them named Agabus and signified by the sprete that ther shuld be great derth throughoute all the worlde which came to passe in ye Emproure Claudius dayes.
Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
29 Then the disciples every man accordinge to his abilite purposed to sende socoure vnto the brethren which dwelt in Iewry.
Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
30 Which thinge they also dyd and sent it to the elders by the hondes of Barnabas and Saul.
Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.

< Acts 11 >