< Luke 5 >

1 Once, when the people were pressing round Jesus as they listened to God’s Message, he happened to be standing by the shore of the Lake of Gennesaret, and saw two boats close to the shore.
Siku moja Yesu alipokuwa amesimama karibu na Ziwa la Genesareti, watu wengi wakiwa wanasongana kumzunguka ili wapate kusikia neno la Mungu,
2 The fishermen had gone away from them and were washing the nets.
akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa, zikiwa zimeachwa hapo na wavuvi waliokuwa wanaosha nyavu zao.
3 So, getting into one of the boats, which belonged to Simon, Jesus asked him to push off a little way from the shore, and then sat down and taught the people from the boat.
Akaingia katika mojawapo ya hizo mashua ambayo ilikuwa ya Simoni, akamwomba aisogeze ndani ya maji kidogo kutoka ufuoni. Kisha akaketi na kufundisha watu akiwa mle ndani ya mashua.
4 When he had finished speaking, he said to Simon: “Push off into deep water, and throw out your nets for a haul.”
Alipomaliza kunena, akamwambia Simoni, “Sasa peleka mashua hadi kilindini kisha mshushe nyavu zenu mkavue samaki.”
5 “We have been hard at work all night, Sir,” answered Simon, “and have not caught anything, but, at your bidding, I will throw out the nets.”
Simoni akamjibu, “Bwana, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha na hatukuvua chochote. Lakini, kwa neno lako nitazishusha nyavu.”
6 They did so, and enclosed such a great shoal of fish that their nets began to break.
Nao walipozishusha nyavu zao, wakavua samaki wengi sana, nyavu zao zikajaa zikaanza kukatika.
7 So they signalled to their partners in the other boat to come and help them; and they came and filled both the boats so full of fish that they were almost sinking.
Wakawaashiria wavuvi wenzao kwenye ile mashua nyingine ili waje kuwasaidia. Wakaja, wakajaza mashua zote mbili samaki hata zikaanza kuzama.
8 When Simon Peter saw this, he threw himself down at Jesus’ knees, exclaiming: “Master, leave me, for I am a sinful man!”
Simoni Petro alipoona haya yaliyotukia, alianguka miguuni mwa Yesu na kumwambia, “Bwana, ondoka kwangu. Mimi ni mtu mwenye dhambi!”
9 For he and all who were with him were lost in amazement at the haul of fish which they had made;
Kwa kuwa yeye na wavuvi wenzake walikuwa wameshangazwa sana na wingi wa samaki waliokuwa wamepata.
10 and so, too, were James and John, Zebediah’s sons, who were Simon’s partners. “Do not be afraid,” Jesus said to Simon; “from to-day you shall catch men.”
Vivyo hivyo wenzake Simoni, yaani Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, walishangazwa pia. Ndipo Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.”
11 And, when they had brought their boats to shore, they left everything, and followed him.
Hivyo wakasogeza mashua zao mpaka ufuoni mwa bahari, wakaacha kila kitu na kumfuata.
12 On one occasion Jesus was staying in a town, when he saw a man who was covered with leprosy. When the leper saw Jesus, he threw himself on his face and implored his help: “Master, if only you are willing, you are able to make me clean.”
Ikawa siku moja Yesu alipokuwa katika mji fulani, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamjia. Alipomwona Yesu, alianguka chini mpaka uso wake ukagusa ardhi, akamsihi akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 Stretching out his hand, Jesus touched him, saying as he did so: “I am willing; become clean.” Instantly the leprosy left the man;
Yesu akanyoosha mkono wake, akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Na mara ukoma wake ukatakasika.
14 and then Jesus impressed upon him that he was not to say a word to any one, “but,” he added, “set out and show yourself to the priest, and make the offerings for your cleansing, in the manner directed by Moses, as evidence of your cure.”
Yesu akamwagiza akisema, “Usimwambie mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na ukatoe sadaka alizoagiza Mose kwa utakaso wako, ili kuwa ushuhuda kwao.”
15 However, the story about Jesus spread all the more, and great crowds came together to listen to him, and to be cured of their illnesses;
Lakini habari zake Yesu zikazidi sana kuenea kotekote kuliko wakati mwingine wowote. Makutano makubwa ya watu yalikuwa yakikusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 but Jesus used to withdraw to lonely places and pray.
Lakini mara kwa mara Yesu alijitenga nao ili kwenda mahali pa faragha kuomba.
17 On one of those days, when Jesus was teaching, some Pharisees and Doctors of the Law were sitting near by. (They had come from all the villages in Galilee and Judea, and from Jerusalem; and the power of the Lord was upon Jesus, so that he could work cures.)
Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, Mafarisayo na walimu wa sheria, waliokuwa wametoka kila kijiji cha Galilaya na kutoka Uyahudi na Yerusalemu, walikuwa wameketi huko. Nao uweza wa Bwana ulikuwa juu yake kuponya wagonjwa.
18 And there some men brought on a bed a man who was paralysed. They tried to get him in and lay him before Jesus;
Wakaja watu wamembeba mgonjwa aliyepooza kwenye mkeka. Wakajaribu kumwingiza ndani ili wamweke mbele ya Yesu.
19 but, finding no way of getting him in owing to the crowd, they went up on the roof and lowered him through the tiles, with his pallet, into the middle of the people and in front of Jesus.
Walipokuwa hawawezi kufanya hivyo kwa sababu ya umati wa watu, wakapanda juu ya paa, wakaondoa baadhi ya matofali, wakamteremsha yule mgonjwa kwa mkeka wake hadi katikati ya ule umati pale mbele ya Yesu.
20 When he saw their faith, Jesus said: “Friend, your sins have been forgiven you.”
Yesu alipoiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa, “Rafiki, dhambi zako zimesamehewa.”
21 The Teachers of the Law and the Pharisees began debating about this. “Who is this man who speaks so blasphemously?” they asked. “Who can forgive sins except God?”
Mafarisayo na wale walimu wa sheria wakaanza kuuliza, “Ni nani mtu huyu anayesema maneno ya kukufuru? Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
22 When Jesus became aware of the way in which they were debating, he turned to them and exclaimed: “What are you debating with yourselves?
Yesu akijua mawazo yao akawauliza, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
23 Which is the easier? — to say ‘Your sins have been forgiven you’? or to say ‘Get up, and walk about’?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi, kumwambia, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uende’?
24 But that you may know that the Son of Man has power on earth to forgive sins” — he spoke to the paralysed man — “To you I say, Get up, and take up your pallet, and go to your home.”
Lakini ili mpate kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Akamwambia yule aliyepooza, “Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
25 Instantly the man stood up before their eyes, took up what he had been lying on, and went to his home, praising God.
Mara yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama mbele yao wote, akachukua mkeka wake, akaenda zake nyumbani, huku akimtukuza Mungu.
26 The people, one and all, were lost in amazement, and praised God; and in great awe they said: “We have seen marvellous things to-day!”
Kila mmoja akashangaa na kumtukuza Mungu. Wakajawa na hofu ya Mungu, wakasema, “Leo tumeona mambo ya ajabu.”
27 After this, Jesus went out; and he noticed a tax-gatherer, named Levi, sitting in the tax-office, and said to him: “Follow me.”
Baada ya haya, Yesu alitoka na kumwona mtoza ushuru mmoja jina lake Lawi akiwa amekaa forodhani, mahali pake pa kutoza ushuru. Akamwambia, “Nifuate.”
28 Levi left everything and got up and followed him.
Naye Lawi akaacha kila kitu, akaondoka, akamfuata.
29 And Levi gave a great entertainment at his house, in honour of Jesus; and a large number of tax-gatherers and others were at table with them.
Kisha Lawi akamfanyia Yesu karamu kubwa nyumbani kwake, nao umati mkubwa wa watoza ushuru na watu wengine walikuwa wakila pamoja nao.
30 The Pharisees and the teachers of the Law belonging to their party complained of this to the disciples of Jesus.”
Lakini Mafarisayo na walimu wa sheria waliokuwa wa dhehebu lao wakawalalamikia wanafunzi wa Yesu, wakisema, “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
31 In answer Jesus said: “It is not those who are well that need a doctor, but those who are ill.
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa.
32 I have not come to call the religious, but the outcast, to repent.”
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.”
33 “John’s disciples,” they said to Jesus, “Often fast and say prayers, and so do the disciples of the Pharisees, while yours are eating and drinking!”
Wakamwambia Yesu, “Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo mara kwa mara hufunga na kuomba, lakini wanafunzi wako wanaendelea kula na kunywa.”
34 But Jesus answered them: “Can you make the bridegroom’s friends fast while the bridegroom is with them?
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwafanya wageni wa bwana arusi kufunga wakati yuko pamoja nao?
35 But the days will come — a time when the bridegroom will be parted from them; and they will fast then, when those days come.”
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Hapo ndipo watakapofunga.”
36 Then, as an illustration, Jesus said to them: “No man ever tears a piece from a new garment and puts it upon an old one; for, if he does, he will not only tear the new garment, but the piece from the new one will not match the old.
Yesu akawapa mfano huu, akawaambia: “Hakuna mtu achanaye kiraka kutoka kwenye nguo mpya na kukishonea kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, atakuwa amechana nguo mpya, na kile kiraka hakitalingana na ile nguo iliyochakaa.
37 And no man puts new wine into old wine-skins; for, if he does, the new wine will burst the skins, and the wine itself will run out, and the skins be lost.
Hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo yote itamwagika.
38 But new wine must be put into fresh skins.
Divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 No man after drinking old wine wishes for new. ‘No,’ he says, ‘the old is excellent.’”
Wala hakuna mtu anayependelea divai mpya baada ya kunywa divai ya zamani, bali husema, ‘Ile ya zamani ni nzuri zaidi.’”

< Luke 5 >