< Luke 13 >

1 Just at that time some people had come to tell Jesus about the Galileans, whose blood Pilate had mingled with the blood of their sacrifices.
Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
2 “Do you suppose,” replied Jesus, “that, because these Galileans have suffered in this way, they were worse sinners than any other Galileans?
Naye Yesu akawaambia, “Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
3 No, I tell you; but, unless you repent, you will all perish as they did.
Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
4 Or those eighteen men at Siloam on whom the tower fell, killing them all, do you suppose that they were worse offenders than any other inhabitants of Jerusalem?
Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
5 No, I tell you; but, unless you repent, you will all perish in the same manner.”
Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao.”
6 And Jesus told them this parable — “A man, who had a fig tree growing in his vineyard, came to look for fruit on it, but could not find any.
Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: “Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
7 So he said to his gardener ‘Three years now I have come to look for fruit on this fig tree, without finding any! Cut it down. Why should it rob the soil?’
Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
8 ‘Leave it this one year more, Sir,’ the man answered, ‘till I have dug round it and manured it.
Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9 Then, if it bears in future, well and good; but if not, you can have it cut down.’”
Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata.”
10 Jesus was teaching on a Sabbath in one of the Synagogues,
Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11 and he saw before him a woman who for eighteen years had suffered from weakness owing to her having an evil spirit in her. She was bent double, and was wholly unable to raise herself.
Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12 When Jesus saw her, he called her to him, and said: “Woman, you are released from your weakness.”
Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, “Mama, umeponywa ugonjwa wako.”
13 He placed his hands on her, and she was instantly made straight, and began to praise God.
Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
14 But the President of the Synagogue, indignant that Jesus had worked the cure on the Sabbath, interposed and said to the people: “There are six days on which work ought to be done; come to be cured on one of those, and not on the Sabbath.”
Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, “Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato.”
15 “You hypocrites!” the Master answered him. “Does not every one of you let his ox or his ass loose from its manger, and take it out to drink, on the Sabbath?
Hapo Bwana akamjibu, “Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
16 But this woman, a daughter of Abraham, who has been kept in bondage by Satan for now eighteen years, ought not she to have been released from her bondage on the Sabbath?”
Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?”
17 As he said this, his opponents all felt ashamed; but all the people rejoiced to see all the wonderful things that he was doing.
Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
18 So Jesus said: “What is the Kingdom of God like? and to what can I liken it?
Yesu akauliza: “Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
19 It is like a mustard-seed which a man took and put in his garden. The seed grew and became a tree, and ‘the wild birds roosted in its branches.’”
NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake.”
20 And again Jesus said: “To what can I liken the Kingdom of God?
Tena akauliza: “Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
21 It is like some yeast which a woman took and covered in three pecks of flour, until the whole had risen.”
Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote.”
22 Jesus went through towns and villages, teaching as he went, and making his way towards Jerusalem.
Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
23 “Master,” some one asked, “are there but few in the path of Salvation?” And Jesus answered:
Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?”
24 “Strive to go in by the small door. Many, I tell you, will seek to go in, but they will not be able,
Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
25 when once the master of the house has got up and shut the door, while you begin to say, as you stand outside and knock, ‘Sir, open the door for us.’ His answer will be — ‘I do not know where you come from.’
“Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
26 Then you will begin to say ‘We have eaten and drunk in your presence, and you have taught in our streets,’ and his reply will be —
Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
27 ‘I do not know where you come from. Leave my presence, all you who are living in wickedness.’
Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
28 There, there will be weeping and grinding of teeth, when you see Abraham, Isaac, and Jacob, and all the Prophets, in the Kingdom of God, while you yourselves are being driven outside.
Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
29 People will come from East and West, and from North and South, and take their places at the banquet in the Kingdom of God.
Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
30 there are some who are last now who will then be first, and some who are first now who will then be last!”
Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
31 Just then some Pharisees came up to Jesus and said: “Go away and leave this place, for Herod wants to kill you.”
Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua.”
32 But Jesus answered: “Go and say to that fox ‘Look you, I am driving out demons and shall be completing cures to-day and to-morrow, and on the third day I shall have done.’
Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
33 But to-day and to-morrow and the day after I must go on my way, because it cannot be that a Prophet should meet his end outside Jerusalem.
Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
34 Jerusalem! Jerusalem! she who slays the Prophets and stones the messengers sent to her — Oh, how often have I wished to gather your children round me, as a hen takes her brood under her wings, and you would not come!
“Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
35 Verily your House is left to you desolate! and never, I tell you, shall you see me, until you say — ‘Blessed is He who comes in the name of the Lord.’”
Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”

< Luke 13 >