< Luke 10 >

1 After this, the Master appointed seventy-two other disciples, and sent them on as his Messengers, two and two, in advance, to every town and place that he was himself intending to visit.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 “The harvest,” he said, “is abundant, but the labourers are few. Therefore pray to the Owner of the harvest to send labourers to gather in his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Now, go. Remember, I am sending you out as my Messengers like lambs among wolves.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Do not take a purse with you, or a bag, or sandals; and do not stop to greet any one on your journey.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 Whatever house you go to stay at, begin by praying for a blessing on it.
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 Then, if any one there is deserving of a blessing, your blessing will rest upon him; but if not, it will come back upon yourselves.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 Remain at that same house, and eat and drink whatever they offer you; for the worker is worth his wages. Do not keep changing from one house to another.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 Whatever town you visit, if the people welcome you, eat what is set before you;
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 cure the sick there, and tell people ‘The Kingdom of God is close at hand.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 But, whatever town you go to visit, if the people do not welcome you, go out into its streets and say
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 ‘We wipe off the very dust of your town which has clung to Our feet; still, be assured that the Kingdom of God is close at Hand.’
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 I tell you that the doom of Sodom will be more bearable on ‘That Day’ than the doom of that town.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Alas for you, Chorazin! Alas for you, Bethsaida! For, if the Miracles which have been done in you had been done in Tyre and Sidon, they would have sat in sackcloth and ashes and repented long ago.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 Yet the doom of Tyre and Sidon will be more bearable at the Judgment than yours.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 And you, Capernaum! Will you ‘exalt yourself to heaven’? ‘You shall go down to the Place of Death.’ (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 He who listens to you is listening to me, and he who rejects you is rejecting me; while he who rejects me is rejecting him who sent me as his Messenger.”
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 When the seventy-two returned, they exclaimed joyfully: “Master, even the demons submit to us when we use your name.”
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 And Jesus replied: “I have had visions of Satan, fallen, like lightning from the heavens.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Remember, I have given you the power to ‘trample upon serpents and scorpions,’ and to meet all the strength of the Enemy. Nothing shall ever harm you in any way.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Yet do not rejoice in the fact that the spirits submit to you, but rejoice that your names have been enrolled in Heaven.”
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 At that same time, moved to exultation by the Holy Spirit, Jesus said: “I thank thee, Father, Lord of Heaven and earth, that, though thou hast hidden these things from the wise and learned, thou hast revealed them to the childlike! Yes, Father, I thank thee that this has seemed good to thee.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Everything has been committed to me by my Father; nor does any one know who the Son is, except the Father, or who the Father is, except the Son and those to whom the Son may choose to reveal him.”
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 Then, turning to his disciples, Jesus said to them alone: “Blessed are the eyes that see what you are seeing;
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 for, I tell you, many Prophets and Kings wished for the sight of the things which you are seeing, yet never heard them.”
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 Just then a Student of the Law came forward to test Jesus further. “Teacher,” he said, “what must I do if I am to ‘gain Immortal Life’?” (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 “What is said in the Law?” answered Jesus. “What do you read there?”
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 His reply was — “‘Thou shalt love the Lord thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy strength, and with all thy mind; and thy neighbour as thou dost thyself.’”
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 “You have answered right,” said Jesus; “do that, and you shall live.”
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 But the man, wanting to justify himself, said to Jesus: “And who is my neighbour?”
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 To which Jesus replied: “A man was once going down from Jerusalem to Jericho when he fell into the hands of robbers, who stripped him of everything, and beat him, and went away leaving him half dead.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 As it chanced, a priest was going down by that road. He saw the man, but passed by on the opposite side.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 A Levite, too, did the same; he came up to the spot, but, when he saw the man, passed by on the opposite side.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 But a Samaritan, traveling that way, came upon the man, and, when he saw him, he was moved with compassion.
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 He went to him and bound up his wounds, dressing them with oil and wine, and then put him on his own mule, and brought him to an inn, and took care of him.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 The next day he took out four shillings and gave them to the inn-keeper. ‘Take care of him,’ he said, ‘and whatever more you may spend I will myself repay you on my way back.’
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Now which, do you think, of these three men,” asked Jesus, “proved himself a neighbour to the man who fell into the robbers’ hands?”
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 “The one that took pity on him,” was the answer; on which Jesus said: “Go and do the same yourself.”
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 As they continued their journey, Jesus came to a village, where a woman named Martha welcomed him to her house.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 She had a sister called Mary, who seated herself at the Master’s feet, and listened to his teaching;
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 but Martha was distracted by the many preparations that she was making. So she went up to Jesus and said: “Master, do you approve of my sister’s leaving me to make preparations alone? Tell her to help me.”
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 “Martha, Martha,” replied the Master, “you are anxious and trouble yourself about many things;
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 but only a few are necessary, or rather one. Mary has chosen the good part, and it shall not be taken away from her.”
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luke 10 >