< Zechariah 7 >

1 When Darius had been the emperor for almost four years, on December 7, Yahweh gave me [another] message.
Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
2 The people of Bethel [city] sent two men, Sharezer and Regem-Melech, along with some other men, [to the temple of Yahweh, the Commander of the armies of angels, ] to request that Yahweh bless them.
Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
3 They also asked the priests at Yahweh’s temple and the prophets [this question]: “For many years, during the fifth month [and during the seventh month of each year], we have mourned and (fasted/abstained from eating food). Should we [continue to do that]?”
kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
4 Then the Commander of the armies of angels gave me a message.
Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
5 [He said], “Tell [RHQ] the priests and all the [other] people of Judah that during the past 70 years, when they mourned and fasted during the fifth and seventh months [of each year], it was not really [RHQ] me, [Yahweh], whom they were [honoring].
“Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
6 And when they ate and drank, it was really [RHQ] to [benefit] themselves.
Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
7 That is certainly [RHQ] what I continually told the former prophets to proclaim [to the people], when Jerusalem and the nearby towns were prosperous and filled with people, and people [also] lived in the desert area to the south and in the foothills [to the west].”
Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
8 Yahweh gave another message to me, saying
Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
9 “[Tell the people that] this is what the Commander of the armies of angels says: ‘Do what is just/right, and act kindly and mercifully toward each other.
“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
10 Do not (oppress/treat cruelly) widows or orphans or foreigners or poor people. Do not even think about doing evil to anyone else.’”
Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
11 But the people refused to pay attention [to what Yahweh said]. They turned their backs [to him], and put their hands over their ears in order to not hear [what he said].
“Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
12 They were very stubborn [IDM], and they would not listen to the laws [that God gave to Moses] or the messages that the Commander of the armies of angels told his Spirit to give to the prophets who were now dead. So the Commander of the armies of angels was very angry.
Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
13 The Commander of the armies of angels says, “When I called/spoke [to the people], they would not listen. So when they called/prayed [to me], I did not listen.
“‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 And I caused them to be scattered among many nations, where they were strangers. [It was as though] [MET] a whirlwind [picked them up and carried them away from their country]. The country/land that they [were forced to] leave was ruined, with the result that no one could [live there or even] travel through it. [It was previously] a delightful land, but they caused it to become (desolate/like a desert).”
‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”

< Zechariah 7 >