< Zechariah 12 >

1 [This is] a message from Yahweh concerning Israel. Yahweh is the one who stretched out the sky, who created the earth, and who (gave life to humans/caused humans to be alive). This is what he says:
Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
2 “I will soon cause Jerusalem to be [like] [MET] a cup full [of very strong alcoholic drink], and the people of other nations who drink it will stagger around. And they will come and attack Jerusalem and [the other towns in] Judah.
“Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
3 At that time, [the armies of] all the nations will gather to attack Jerusalem, but I will cause [the leaders of] Judah to be [like] [SIM] a very heavy rock, and all who [try to] lift it will be badly injured.
Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
4 At that time I will cause every [one of their enemies’] horses to panic, and their riders to become crazy. I [IDM] will protect the people of Judah, but I will cause all their enemies’ horses to become blind.
Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
5 Then the leaders of Judah will say to themselves, ‘The people in Jerusalem are strong because the Commander of the armies of angels is their God.’
Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
6 At that time I will enable the leaders of Judah to be like [SIM] a pan containing hot coals [that is put] in a woodpile [to set it on fire], or like [SIM] a burning torch [that is put] in a [field of] ripe grain [to set it on fire]. The leaders of Judah [and their army] will destroy the people of the surrounding nations in all directions. But [the people of] Jerusalem will remain safe.
Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
7 And [I], Yahweh, will protect the tents of [the soldiers in other places in] Judah before [I rescue the people of Jerusalem], in order that the leaders of Jerusalem [DOU] will not be honored more than [the people in other places in] Judah [are honored].
Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
8 At that time, I will protect [MET] the people of Jerusalem. When that happens, even the weakest people in Jerusalem will be [strong] like [King] David [was]. And the descendants [MTY] of David will [rule the people] like I [would], as though an angel sent from [me], Yahweh, was their leader.
Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
9 At that time, I will prepare to destroy all the nations that attack Jerusalem.”
“Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
10 “I, [Yahweh, ] will cause the descendants [MTY] of [King] David to act very kindly and mercifully. They will look at me, [the one] who has been stabbed, and they will cry bitterly, like people cry for a firstborn son [who has died] [DOU].
Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
11 At that time, many people in Jerusalem will be crying bitterly, like people cried [when King Josiah was killed in the battle] at Hadad-Rimmon on the Megiddo Plain.
Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
12 Many people in Judah will cry, each family by themselves: the male descendants of David by themselves, and their wives by themselves, the male descendants of [David’s son] Nathan by themselves, and their wives by themselves,
Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
13 the male descendants [MTY] of Levi by themselves, and their wives by themselves, the male descendants of [Levi’s grandson] Shimei by themselves, and their wives by themselves,
Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
14 and all the other members [of the kings’ clans and the priests’ clans] by themselves, and their wives by themselves.”
Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.

< Zechariah 12 >