< Ruth 3 >

1 One day, Naomi said to Ruth, “My daughter, I think that I should [RHQ] try to arrange for you to have a husband [MTY] who will (take care of/provide for) you.
Kisha Naomi akamwambia mkwewe, “Binti yangu, je, nisingelikutafutia pumziko ambako utatunzika vyema?
2 Boaz, the man with whose [servant] girls you have been [gathering grain], is a close relative [of our dead husbands]. Listen [carefully]. Tonight he will be at the ground where [the barley has] been threshed. He will be separating the barley grain from the chaff.
Je, Boazi, ambaye umekuwa pamoja na watumishi wake wasichana, si jamaa yetu wa karibu? Usiku wa leo atakuwa anapepeta ngano kwenye sakafu ya kupuria.
3 Bathe yourself and put on some perfume. Put on your [best] clothes. Then go down to the ground where they have threshed [the grain]. But do not let Boaz know that you are there while he is eating [supper] and drinking.
Basi oga na ukajipake marashi, ujivalie nguo zako nzuri. Kisha uende kwenye sakafu ya kupuria, lakini angalia asijue kwamba upo pale mpaka atakapomaliza kula na kunywa.
4 [When he has finished eating], notice where he lies down to sleep. Then [when he is asleep], take the blanket off his feet and lie [close to his feet]. [When he wakes up], he will tell you what to do.”
Atakapokwenda kulala, angalia mahali atakapolala. Kisha uende ufunue miguu yake, ulale. Naye atakuambia utakalofanya.”
5 Ruth replied, “I will do everything that you have told me [to do].”
Ruthu akajibu, “Lolote usemalo nitatenda.”
6 So she went down to the ground where they had threshed [the barley grain]. There she did everything that her mother-in-law had told her [to do].
Basi akashuka mpaka kwenye sakafu ya kupuria, akafanya kila kitu mama mkwe wake alichomwambia kufanya.
7 When Boaz finished eating [supper] and drinking [wine], he felt happy. Then he went over to the far end of the pile of grain. He lay down [and went to sleep]. Then Ruth approached him quietly. She took the blanket off his feet and lay down [there].
Wakati Boazi alipomaliza kula na kunywa, naye akawa amejawa na furaha, alikwenda kulala mwisho wa lundo la nafaka. Ruthu akanyemelea polepole, akafunua miguu yake, na akalala.
8 In the middle of the night, he suddenly awoke. He sat up and saw that a woman was lying at his feet.
Usiku wa manane, kitu kilimshtua Boazi, akajigeuza, akagundua yupo mwanamke amelala miguuni pake.
9 He asked her, “Who are you?” She replied, “I am your servant, Ruth. Since you are the one who has a responsibility to take care of [someone like me whose dead husband was] your close relative, spread the corner of your cloak over my [feet to show that you will marry me].”
Akauliza, “Wewe ni nani?” Akajibu, “Ni mimi Ruthu, mjakazi wako. Uitande nguo yako juu yangu, kwa sababu wewe ndiwe jamaa wa karibu wa kutukomboa.”
10 Boaz replied, “Young lady, I hope that Yahweh will (bless/be kind to) you! You have acted kindly [toward your mother-in-law], and now you are acting even more kindly [toward me by wanting to marry me, instead of wanting to marry a young man]. You have not looked for either a rich young man or a poor young man, [to marry him].
Akamwambia, “Binti yangu, ubarikiwe na Bwana. Wema huu wa sasa ni mkuu kushinda hata ule ulioonyesha mwanzoni. Hukuwakimbilia vijana, wakiwa matajiri au maskini.
11 Now, young lady, I will do everything you ask. Don’t worry [that people in this town might think I am doing wrong by marrying you because you are a woman from Moab]. All the people in this town know that you are an honorable woman.
Sasa, binti yangu, usiogope. Nitakufanyia yote uliyoomba. Kwa maana mji wote wa watu wangu wanakujua ya kwamba wewe ni mwanamke mwenye tabia nzuri.
12 But [there is one problem]. Although it is true that I am a close relative [of your mother-in-law’s dead husband], there is another man who is a closer relative [than I am], and therefore he should be the one to [marry you and] take care of you.
Ingawa ni kweli kwamba mimi ndiye jamaa aliye karibu, bado kuna mtu mwingine wa jamaa aliye karibu zaidi wa kukomboa kuliko mimi.
13 You stay here for the rest of this night. Tomorrow morning [I will tell this man about you]. If he says that he will [marry you and] take care of you, fine, [we will] let him do that. But if he is not willing [to do that], I solemnly promise that as surely as Yahweh lives, I will [marry you and] take care of you. So lie/sleep here until it is morning.”
Wewe kaa hapa usiku huu, kisha asubuhi kama akikubali kukomboa, vyema na akomboe. La sivyo kama hayuko tayari, hakika kama Bwana aishivyo nitafanya hivyo. Lala hapa mpaka asubuhi.”
14 So she lay at his feet until morning. But she got up and left before it was light enough that people would be able to recognize her, because Boaz said, “I do not want anyone to know that a woman was here.”
Hivyo huyo mwanamke akalala miguuni pake mpaka asubuhi, akaondoka mapema pasipo mtu kuweza kumtambua mwenzake, maana Boazi alisema, “Isijulikane kabisa ya kuwa mwanamke alifika kwenye sakafu ya kupuria.”
15 He also said to her, “Bring to me your cloak and spread it out.” When she did that, he poured into it six measures/24 liters/50 pounds of barley, and put in on her back. Then he (OR, she) went back to the town.
Pia akamwambia, “Leta shela yako uliyoivaa, uitandaze.” Naye alipoitandaza, akamimina vipimo sita vya shayiri, akamtwika. Kisha Ruthu akarudi zake mjini.
16 When Ruth arrived home, her mother-in-law asked her, “My daughter, how did (things go/Boaz act toward you)?” Then Ruth told her everything that Boaz had done for her [and said to her].
Basi Ruthu alipofika kwa mama mkwe wake Naomi, akamuuliza, “Je, binti yangu, ilikuwaje huko?” Ndipo akamwelezea kila kitu Boazi alichomfanyia.
17 She also said [to Naomi], “He gave me all this barley, saying ‘I do not want you to return to your mother-in-law empty-handed.’”
Akaendelea kusema, “Amenipa shayiri vipimo sita akisema, ‘Usiende kwa mama mkwe wako mikono mitupu.’”
18 Then Naomi said, “My daughter, just wait until we see what happens. [I am sure that] Boaz will take care of [LIT] the matter [of your marriage]. [LIT]”
Kisha Naomi akasema, “Subiri binti yangu, mpaka utakapojua kwamba hili jambo limekwendaje. Kwa sababu mtu huyu hatatulia mpaka akamilishe jambo hili leo.”

< Ruth 3 >