< Romans 16 >

1 [By means of this letter] I am introducing and recommending to you our fellow believer Phoebe, [who will be taking this letter to you]. She is a deacon in the congregation in Cenchrea [city].
Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea.
2 [I request that] you receive her because of her relationship with the Lord. [You should do that because] those who are God’s people ought to receive [their fellow believers]. [I am also requesting] that you help her [by giving her] [EUP] whatever she needs, because she has helped many people, including me.
Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia.
3 Tell Priscilla and [her husband] Aquila that I (send greetings to/am thinking fondly of) them. They worked with me for Christ Jesus,
Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu.
4 and they were even willing to die [IDM] in order [to save] my life. It is not only I who thank them [for helping me], but the people in all [HYP] the non-Jewish congregations also [thank them for saving my life].
Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine.
5 Also tell the congregation [that meets] in their house that I (send my greetings to/am thinking fondly of) them. Tell my dear friend Epaenetus the same thing. He is the first man in Asia [province] who [believed] in Christ.
Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni kwa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.
6 Tell Mary, who has worked hard [for Christ] in order to [help] you, that I (send my greetings to/am thinking fondly of) her.
Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu.
7 Tell the same thing to Andronicus and [his wife] Junia (OR, and [his sister] Junia) who are my fellow Jews and who were also [previously] in prison with me. They are well-known/respected (OR, respected by the) apostles, and they became Christians before I did.
Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi.
8 I also send my greetings to Ampliatus, who is a dear friend because of his relationship with the Lord.
Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana.
9 I also send my greetings to Urbanus, who works for Christ with us, and to my dear friend Stachys.
Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku.
10 I also send my greetings to Apelles, whom Christ has approved [because Apelles successfully endured trials]. Tell the [believers] who [live in the house] of Aristobulus that I send my greetings to them.
Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo.
11 Also tell Herodion, who is my fellow Jew, that I send my greetings to him. Tell the same thing to those who [live in the house] of Narcissus who belong to the Lord.
Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana.
12 Tell the same thing to Tryphaena and [her sister] Tryphosa, who work hard for the Lord. I also send my greetings to Persis. [We all] love her and she has worked very hard for the Lord.
Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana.
13 Tell Rufus, who is an outstanding Christian, that I send my greetings to him. [Tell the same thing to] his mother, [who has treated me as though] I [were her son] [MET].
Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia.
14 Tell Asyncritus and Phlegon and Hermes and Patrobas and Hermas and the fellow believers who [meet] with them that I am sending my greetings to them.
Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao.
15 I also send my greetings to Philologus, to [his wife] Julia (OR, [his sister] Julia), to Nereus and his sister, and to Olympas, and to all God’s people who [meet] with them.
Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olumpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao.
16 Greet one another affectionately, but in a pure way, [when you gather together]. The [believers in] all the Christian congregations [HYP] [in this area (send their] greetings to/say they are thinking fondly of) you.
Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
17 My fellow believers, I exhort you that you beware of those people who are causing divisions among you and who cause people to turn away [from God] [MTY] [because they teach things that] are contrary to the message [about Christ] that you have learned (OR, that others taught you). Keep away from such people!
Ndugu zangu, nawasihi muwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao,
18 They do not serve our Lord Christ! On the contrary, they only want to satisfy their own desires [MTY]! Also, by all the eloquent things that they say [DOU] they deceive those people who do not realize [that their teaching is false].
maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu.
19 [Believers] everywhere know that you have paid attention to [the good message about Christ], with the result that I rejoice about you. But I also want you to be wise, [with the result that you do] what is good. I also want you to avoid doing what is evil.
Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na hivyo mmekuwa sababu ya furaha yangu. Nawatakeni muwe na hekima katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya.
20 [If you avoid people who teach what is false], what will [soon happen] [MET] [will be as though] God, who causes us to be peaceful, will be crushing Satan under your feet! [I pray that] our Lord Jesus will continue to act kindly towards you.
Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
21 Timothy, who works with me, and Lucius and Jason and Sosipater, who are my fellow Jews, [want you to know that they are] (sending their greetings to/thinking fondly of) you.
Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipatro, wananchi wenzangu, wanawasalimu.
22 I, Tertius, [one who belongs to] the Lord, [also want you to know] that I am (sending my greetings to/thinking fondly of) you. [I am writing this letter as Paul tells me what to write for him].
Nami Tertio, ninayeandika barua hii nawasalimuni katika Bwana.
23 I, [Paul], am staying in the house of Gaius, and the whole congregation [here meets] in his house. He [also wants you to know] that he is (sending his greetings to/thinking fondly of) you. Erastus, the treasurer of [this] city, also [wants you to know that] he is (sending his greetings to/thinking fondly of) you. Our fellow believer Quartus also (sends his greetings to you./says he is thinking fondly of you.)
Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.
25 As [I] proclaim [the good message about] Jesus Christ, [I tell about God], the one who is able to strengthen you [spiritually]. I also proclaim the [truth] that was not revealed {which [God] did not reveal} in all previous ages/times (aiōnios g166)
Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya ujumbe wa Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. (aiōnios g166)
26 but which has now been {which [he] has now} revealed. [I, along with others, have proclaimed] what the prophets wrote [about Christ]. We are doing what the eternal God commanded [us(exc)/me to do]. We want [people in] all ethnic groups to know [Christ] so that they can believe [in him] and obey [him]. (aiōnios g166)
Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirisha kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. (aiōnios g166)
27 [I desire that by] Jesus Christ [enabling us, we] will forever praise the one who alone is God, who alone is [truly] wise. (May it be so!/Amen!) (aiōn g165)
Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina. (aiōn g165)

< Romans 16 >