< Psalms 44 >

1 God, we ourselves have heard what our parents and grandparents told us. They told us about the miracles that you performed long ago.
Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
2 [They told us] how you expelled the ungodly people and enabled us to live in their land. [They told us] that you punished those ungodly people and enabled your own people to prosper [IDM].
Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
3 It was not by using their own swords that they conquered the people that lived in that land, and it was not by their own power that they were victorious; it was only by your power [MTY, DOU] [that they did those things]; and they were sure that you were with them, and that showed that you were pleased with them.
Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
4 You are my King and my God; it is you who enable us, your people [MTY], to defeat our enemies.
Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
5 It is by your power that we knock our enemies down and tramp on them.
Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
6 I do not trust that I will be saved by using my bow [and arrows] and my sword.
Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
7 No, it is you who have rescued us from our enemies, it is you who have caused those who hate us to become ashamed [because they were defeated].
Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
8 We have continually boasted about what God [has done for us], and we will thank him [MTY] forever.
Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
9 But [now] you have rejected us and caused us to be disgraced; when our armies march out [to fight a battle], you no [longer] go with them.
Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
10 You have caused us to run away from our enemies, with the result that they captured the things that belonged to us.
Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
11 You have allowed us to become like [MET] sheep that were ready to be slaughtered; you scattered us [far away] among [other].
Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
12 [It is as though] [MET] you sold us, your people, [to our enemies] for a very small price, and you did not gain much profit from selling us!
Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
13 People who live in nations near us make fun of us; they laugh at us and deride/belittle us.
Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
14 They make jokes using the name of [our country], they shake their heads [to indicate that they despise us].
Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
15 All day I feel disgraced; from seeing my face, people know that I am ashamed.
Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
16 I hear what those who sneer at me and revile me say; I am ashamed in front of my enemies and those who want to harm me.
kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
17 All these things have happened to us [even] though we have not forgotten you, and we are not the ones who disobeyed the agreement you made with [our ancestors].
Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
18 We have not stopped being loyal to you, and we have not stopped doing what you want us to do [IDM].
Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 But [it is as though] you have allowed us to be helpless among wild animals, and abandoned us in a deep dark [ravine].
Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
20 If we had forgotten to worship [MTY] our God, or if we had spread out our hands to [worship] a foreign god,
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
21 you certainly would have known that, because you know [even] what we secretly think.
Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
22 But it is because we belong to you, [that our enemies] are constantly killing us. They act toward us as though we were only sheep to be slaughtered.
Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
23 [So], Yahweh, arise! Why are you asleep [RHQ]? Get up! Do not reject us forever!
Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24 Why are you not looking at us? Why are you forgetting that we are suffering and being oppressed [by our enemies]?
Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25 We are pushed down to the ground and we cannot get up.
Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26 Arise, and come and help us! Rescue us because you faithfully love us!
Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.

< Psalms 44 >