< Psalms 17 >

1 Yahweh, listen to me while I plead with you to act justly toward me. Hear me while I call out to you to help me. Pay attention to what I say while I pray because I am speaking [MTY] honestly/truthfully.
Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
2 You are the one who is able to declare that I (am innocent/have not done anything that was wrong) because you see/know that I am telling the truth.
Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
3 You know what I think, [even] at night; you have examined what I say and do, and you know that I have determined to never tell any lies.
Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
4 I have not done like others do; I have always done what is right [IDM], and I have not acted cruelly toward others.
Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
5 I have always done what you told me to do [IDM], I have (never failed to do/always done) [LIT] those things.
Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
6 O God, I pray to you because you answer me; please listen [MTY] to what I am saying.
Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
7 Show me that you faithfully love me. By your great power [MTY] rescue those who (run to/trust in) you to protect them from their enemies.
Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
8 Protect me as people carefully protect their own eyes; protect me like [birds] protect [their babies] under their wings [MET].
Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
9 Do not allow wicked people to attack me; my enemies surround me, wanting to kill me.
kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
10 They never pity [IDM] anyone, and they are always boasting.
Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
11 They have hunted/searched for me and found me. They surround me, watching for an opportunity to throw me to the ground.
Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
12 They are like lions [SIM] that are ready to tear apart the animals that they capture; they are like young lions that are hiding, waiting to pounce [on their prey].
Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
13 Yahweh, come and (oppose/fight against) my enemies and defeat them! Use your sword to save me from those wicked people!
Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
14 Yahweh, by your power [MTY] rescue me from those people who are interested [only] in things here in this world. But you provide plenty of food for those whom you love dearly; their children also have many things that their grandchildren will inherit.
Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
15 Yahweh, because I act righteously, I will [some day] see you [SYN]. When I awake, I will see you face-to-face, and then I will be happy.
Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.

< Psalms 17 >