< Numbers 33 >

1 Here is a list of the places where the/we Israelis went as Aaron and Moses/I led them/us after they/we left Egypt.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Yahweh commanded Moses/me to write down the names of the places where they/we went.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 On the fifteenth day of the first month [of the year], the day after we celebrated the (Passover/the time when Yahweh killed all the firstborn sons of the people of Egypt), they/we left Rameses [city in Egypt] and marched boldly while the Egyptian army was coming behind them/us.
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 As they/we left, the people of Egypt were still burying the bodies of their firstborn sons. [By killing them], Yahweh showed that the gods that the people of Egypt worshiped were false gods.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 After leaving Rameses, they/we first went to Succoth and set up their/our tents there.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Then they/we left Succoth and went to Etham, at the edge of the desert, and set up their/our tents there.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Then they/we left Etham and returned to Pi-Hahiroth, to the east of Baal-Zephon, and set up their/our tents near Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Then they/we left Pi-Hahiroth and walked through the [Red] Sea into the Etham Desert, and set their/our tents at Marah.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Then they/we left Marah and went to Elim. There were twelve springs and 70 palm trees there. They/We set up our tents there.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Then they/we left Elim and went to the area near the Red Sea and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Then they/we left the Red Sea area and went to the area near the Sin Desert and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Then they/we left the Sin Desert and went to Dophkah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Then they/we left Dophkah and went to Alush and set up their/our tents there.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Then they/we left Alush and went and set up their/our tents at Rephidim, where they/we had no water to drink.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Then they/we left Rephidim and went to the Sinai Desert and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Then they/we left the Sinai Desert and went to Kibroth-Hattaavah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Then they/we left Kibroth-Hattaavah and went to Hazeroth and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Then they/we left Hazeroth and went to Rithmah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Then they/we left Rithmah and went to Rimmon-Perez and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Then they/we left Rimmon-Perez and went to Libnah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Then they/we left Libnah and went to Rissah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Then they/we left Rissah and set up their/our tents at Kehelathah.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Then they/we left Kehelathah and went to Shepher Mountain and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Then they/we left Shepher and went to Haradah [Mountain] and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Then they/we left Haradah and went to Makheloth and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Then they/we left Makheloth and went to Tahath and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Then they/we left Tahath and went to Terah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Then they/we left Terah and went to Mithcah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Then they/we left Mithcah and went to Hashmonah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Then they/we left Hashmonah and went to Moseroth and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Then they/we left Moseroth and went to Bene-Jaakan and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Then they/we left Bene-Jaakan and went to Hor-Haggidgad and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Then they/we left Hor-Haggidgad and went to Jotbathah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Then they/we left Jotbathah and went to Abronah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Then they/we left Abronah and went to Ezion-Geber and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Then they/we left Ezion-Geber and went to Zin Desert and set up their/our tents at Kadesh there.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Then they/we left Kadesh and went to Hor Mountain, at the border of Edom land and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Aaron, the priest, obeyed Yahweh and climbed up the mountain. There he died, on the first day of their/our fifth month, 40 years after the/we Israelis left Egypt.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron was 123 years old when he died.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 (That was when the king of Arad [city] heard that the/we Israelis were coming. Arad was in the southern part of Canaan, where the Canaan people-group lived.)
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 The Israelis left Hor Mountain and went to Zalmonah and set up their/our tents there.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Then they/we left Zalmonah and went to Punon and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Then they/we left Punon and went to Oboth and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Then they/we left Oboth and went to Iye-Abarim, which was on the border of the Moab region, and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Then they/we left Iye-Abarim and went to Dibon-Gad and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Then they/we left Dibon-Gad and set up their/our tents at Almon-Diblathaim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Then they/we left Almon-Diblathaim and went to the Abarim Mountains, near Nebo and set up their/our tents there.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Then they/we left the Abarim Mountains and went to the plains of the Moab region, near the Jordan [River], across from Jericho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 They/We set up our tents there; their/our tents stretched [for several miles/km.] from Beth-Jeshimoth to Acacia.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 While we were there on the plains of the Moab [region] near the Jordan [River], across from Jericho, Yahweh spoke to Moses/me. He said,
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 “Tell this to the Israeli people: When you cross the Jordan [River] and enter the Canaan [region],
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 you must force all the people who live there to leave. Destroy all their carved statues and all their idols made of metal. Wreck all the places where they worship [their idols].
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Take their land from them and start to live there, because I have given their land to you for you to own.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 “Divide up the land by throwing (lots/small stones which have been marked) [to decide which group will get which area]. Give the larger areas to the groups that have more people, and give the smaller areas to the groups that have fewer people. Each tribe will receive its own land.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 If you do not force the people who live there to leave, they will cause you to have much trouble. They will be like sharp hooks in your eyes, and like thorns in your sides. And they will bring trouble to you, in that land where you will be living.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 And then I will punish you, as I had planned to punish them.”
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Numbers 33 >