< Numbers 30 >

1 Moses/I spoke with the leaders of the Israeli tribes. He/I told them these commands that Yahweh had given to him/me:
Mose akawaambia viongozi wa makabila ya Israeli: “Hili ndilo Bwana analoagiza:
2 “If a man solemnly promises Yahweh that he will do something, he must do what he promised.
Mwanaume awekapo nadhiri kwa Bwana, au anapoapa kujifunga kwa ahadi, kamwe asitangue neno lake, bali ni lazima afanye kila kitu alichosema.
3 “If a young woman who is still living with her parents solemnly promises to Yahweh to do something,
“Wakati mwanamwali anayeishi bado nyumbani kwa baba yake atakapoweka nadhiri kwa Bwana, ama amejifunga mwenyewe kwa ahadi,
4 and if her father hears about what she promised, and if he does not object, she must do what she promised [DOU].
na baba yake akasikia kuhusu nadhiri au ahadi yake lakini asimwambie lolote, ndipo nadhiri zake zote na kila ahadi aliyoiweka na kujifunga kwayo itathibitika.
5 But if her father hears about what she promised and does not allow her to do that, then she does not need to do what she promised. Yahweh will forgive her for not doing what she promised.
Lakini kama baba yake akimkataza wakati anapoisikia, hakuna nadhiri wala ahadi yake yoyote aliyojifunga kwayo itakayosimama; Bwana atamweka huru huyo mwanamwali kwa sababu baba yake amemkataza.
6 “If a woman promises Yahweh that she will do something, but then she gets married,
“Ikiwa ataolewa baada ya kuweka nadhiri au baada ya midomo yake kutamka ahadi fulani bila kufikiri akawa amejifunga hivyo,
7 if her husband hears about what she promised to do, and he does not object, she must do what she promised [DOU].
na mume wake akasikia habari hiyo asimwambie neno lolote, ndipo nadhiri zake ama ahadi zake ambazo alikuwa amejifunga nazo zitathibitika.
8 But if her husband hears about it and does not allow her to do that, she does not need to do what she promised, and Yahweh will forgive her for not doing what she promised.
Lakini ikiwa mume wake atamkataza atakaposikia kuhusu hilo, atakuwa ametangua nadhiri ambazo zilikuwa zimemfunga mkewe, ama ahadi aliyotamka pasipo kufikiri ambayo amejifunga kwayo, naye Bwana atamweka huru yule mwanamke.
9 “If a widow or a woman who has been divorced makes a promise, she must do what she promised.
“Nadhiri yoyote ama patano ambalo limefanywa na mjane ama mwanamke aliyeachwa vitakuwa vimemfunga.
10 “If a woman who is married promises [DOU] to do something,
“Ikiwa mwanamke anayeishi na mumewe ataweka nadhiri ama kujifunga mwenyewe kwa ahadi chini ya kiapo,
11 and if her husband hears about it but does not object, she must do what she promised.
na mumewe akasikia kuhusu jambo hili lakini asimwambie lolote wala hakumkataza, ndipo viapo vyake vyote au ahadi zinazomfunga zitakapothibitika.
12 But if he hears about it and does not allow her to do that, she does not need to do what she promised, and Yahweh will forgive her for not doing it.
Lakini ikiwa mumewe atabatilisha nadhiri hizo baada ya kuzisikia, basi hakuna nadhiri au ahadi zozote alizoziweka kwa midomo yake zitakazothibitika. Mumewe atakuwa amezibatilisha, na Bwana atamweka huru yule mwanamke.
13 A woman’s husband may require her to do what she has promised, or he may not allow her to do what she has promised.
Mumewe anaweza kuthibitisha au kutangua nadhiri yoyote anayoweka, au ahadi yoyote aliyoweka kwa kuapa ili kujikana mwenyewe.
14 If he does not object for several days [after he hears about it], she must do what she promised.
Lakini ikiwa mumewe hasemi lolote kwake kuhusu jambo hilo siku baada ya siku, basi mumewe atakuwa amethibitisha nadhiri zote, na ahadi zote zinazomfunga mkewe. Anavithibitisha kwa kutokusema lolote kwa mkewe anapoyasikia hayo.
15 But if he waits a long time after she has promised to do something and then he tells her that he will not permit her to do it, if she does not do what she promised, [she will not be punished]; her husband is the one whom [Yahweh] will punish.”
Hata hivyo, ikiwa mumewe atavibatilisha baada ya kusikia hayo, basi atawajibika kwa hatia ya mkewe.”
16 Those are the rules that Yahweh gave to Moses/me for husbands and wives, and for young women who are still living with their parents.
Haya ndiyo masharti ambayo Bwana alimpa Mose kuhusu mahusiano kati ya mtu na mkewe, na kati ya baba na binti yake ambaye bado anaishi nyumbani kwa baba yake.

< Numbers 30 >