< Numbers 22 >

1 Then the Israelis traveled west to the area of Moab that was in the valley of the Jordan [River], across the river from Jericho [city].
Watu wa Israeli wakasafiri mpaka wakaweka kambi kwenye uwanda wa Moabu karibu na Yeriko, kwenye upande mwingine wa mto Yorodani kutoka mji ule.
2 But King Balak, the son of Zippor, who ruled Moab, found out what the Israelis had done to the Amor people-group.
Balaki mwana wa Zippori aliona yote ambayo Israeli aliwafanyia Waamori. Moabu aliogopa sana hao watu kwa sababu walikuwa wengi sana,
3 [When he saw that] the Israelis were very numerous, he and his people became terrified.
na Moabu alIwahofia wana wa Israeli.
4 So the king of Moab [went to] the leaders of the Midian people-group and said to them, “This huge group [of Israelis] will (wipe out/destroy) everything around them, like an ox devours grass!” Balak was the king of Moab.
Mfalme wa Moabu akawaambia wazee wa Midiani, “Huu umati utakula kila kitu tulicho nacho na maksai hula nyasi za kondeni.” Sasa Balaki mwana wa Zippori alikuwa mfalme wa Moabu.
5 He sent messengers to [a prophet named] Balaam, who was living in his own area, in Pethor [town], near the [Euphrates] River. He sent this message to request that Balaam would come [to help him]: “A huge group of people has arrived here from Egypt. [It looks like] they are covering the entire land! And they have begun to live close to us.
Akatuma wajumbe kwenda kwa Balamu mwana wa Beori, kule Petho ambayo iko karibu na mto Frati, katika nchi ya taifa lake na watu wake. Akamwita na kumwambia, “Tazama, Kuna taifa ambalo wamekuja hapa tokea Misiri. Wanafunika uso wa dunia na sasa wananifuatia mimi.
6 Because they are very powerful/numerous, [we are afraid of them. So] please come and curse them for me. Then my army may be able to defeat them and expel them from the land [where they are now living]. I know that good things will happen to the people whom you bless, and disasters will happen to the people whom you curse.”
Tafadhali naomba uje unilaanie hili taifa, kwa sababu wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwavamia na kuwafukuza watoke katika nchi yangu. Najua kuwa yeyote unayembariki hubarikiwa na yeyote unayemlaani atalaaniwa.”
7 [Balak’s messengers, who were] leaders of both the Moab and Midian people-groups, took money with them to pay Balaam in order that he would [come and] curse the Israelis. They went to Balaam and told him what Balak had said.
Kwa hiyo wazee wa Moabu na wale wa Midiani wakaondoka, pamoja nao wakachukua malipo ya uganga. Wakafika kwa Balaamu wakamwambia maneno ya Balaki.
8 Balaam said, “Stay here tonight. [Tomorrow morning] I will tell you whatever Yahweh tells me that I should say to you.” So the leaders from Moab stayed there that night.
Balaamu akawaambia, “Bakini hapa usiku wa leo. Kesho nitawaletea atakachoniambia BWANA.” Kwa hiyo wale viongozi wa Moabu wakabaki na Balaamu kwa usiku huo.
9 During the night, God appeared to Balaam and asked him, “(Who are/Tell me about) these men who are staying with you.”
Mungu akaja kwa Balaamu na kumwambia, “Ni akina nani hawa waliokuja kwako?”
10 Balaam replied, “Balak, the king of Moab, sent these men to tell me this:
Balaamu akamjibu Mungu, “Balaki mwana wa Zippori, Mfalme wa Moabu amewatuma kwangu. Alisema,
11 ‘A huge group of people has come from Egypt, and they have spread all over this area. Please come immediately to curse them. Then I may be able to defeat them and expel them [from this area].’”
'Tazama hawa watu waliotoka Misri wanafunika uso wa nchi yangu. Sasa naomba uje unilaanie hawa watu. Labada nitaweza kuwa kuwashinda na kuwafukuza.'”
12 God replied to Balaam, “Do not go with them! I have blessed those people, so you must not curse them!”
Mungu akamjiu Balaam, “Usiambatane na hao wanaume. Na usiwalaani hawa wana wa Israeli kwa sababu wamebarikiwa.”
13 The next morning, Balaam got up and told Balak’s men, “Go back home. [But go by yourselves, because] Yahweh is not allowing me to go with you.”
Balaamu akaamka asubuhi na kuwaambia wale viongozi wa Balaki, “Rudini nchini kwenu kwa sababu BWANA amenikataza kuambatana nanyi.”
14 So the men from Moab returned to King Balak and they reported to him, “Balaam refused to come with us.”
Kwa hiyo wale viongozi wa Moabu wakaondoka na kurudi kwa Balaki. Wakamwambia, “Balaamu amekataa kuambatana nasi.”
15 But Balak sent another [group of] leaders to Balaam. It was a group that was larger and they were more important [than the men in the first group].
Balaki akatuma viongozi wengine waliokuwa wanaheshimiwa zaidi kuliko kundi lile la awali.
16 They went to Balaam and told him this: “This is what King Balak says: ‘Please do not allow anything to hinder you from coming here.
Wakaja kwa Balaamu na kumwambia, “Balaki mwana wa Zippori anasema hivi, 'Tafadhali hebu kitu chochote kisikuzuie kuja kwangu,
17 I will pay you (a lot of money/very well) [if you come], and I will do anything that you ask me to do. Just come and curse these [Israeli] people for me!’”
kwa sababu nitakulipa malipo mazuri sana na kukupa heshima kubwa, nami nitakufanyia chochote utakachoniambia. Tafadhali sana uje unilaanie hawa watu.'”
18 But Balaam answered them, “Even if Balak would give me a palace filled with silver and gold, I would not do anything to disobey Yahweh, (my God/the God whom I [worship]).
Balaamu akawajibu watu wa Balaki akawaambia, “Hata kama Balaki atanipa ikulu yake ikiwa imejaa fedha na dhahabu, sitaweza kufanya dhidi ya maneno ya BWANA, Mungu wangu na kufanya pungufu au zaidi ya kile anachoniambia.
19 But stay here one more night, like the other messengers did, and I will find out if Yahweh has anything more to say to me.”
Sasa basi, tafadhali subirini hapa usiku wa leo pia, ili kwamba nipate kujifunza kitu zaidi ambacho BWANA ananiambia.”
20 That night God appeared to Balaam again and said to him, “These men have come to request that you go back with them, so you may go with them, but do only what I tell you [to do]!”
BWANA akaja kwa Balaamu usiku ule na kumwambia, “kwa kuwa hawa watu wamekuja kukuita, inuka uende nao. Lakini utafanya tu kile nitakachokuambia kufanya.”
21 So the next morning, Balaam put a saddle on his donkey and he departed [with two of his servants] along with the men from Moab.
Balaamu akainuka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na viongozi wa Moabu.
22 [Even though God had given Balaam permission to go, he was still angry]. So he sent one of his angels to Balaam. This angel stood in the road to block Balaam’s path. As Balaam and the two servants were riding on their donkeys,
Lakini kwa sababu alienda, hasira za Mungu zikawaka. Malaika wa BWANA akasimama barabarani kama adui wa Balaamu, aliyekuwa akimpanda yule punda. Watumishi wawili wa Balaamu walikuwa pamoja naye.
23 Balaam’s donkey saw the angel. The angel was standing in the road and was holding a sword in his hand, [but Balaam did not see him]. Balaam’s donkey turned off the road into a field. So Balaam struck the donkey and forced it to go back onto the road.
Yule punda alimwona yule malaika wa BWANA akiwa amesimama barabarani akiwa na upanga mkononi mwake. Yule punda akageuka na kwenda shambani. Balaamu akampiga yule punda ili arudi barabarani.
24 Then the angel stood in a place where the road was very narrow, between two vineyards, with walls on each side of the road.
Sasa malaika wa BWANA akasimama kwenye njia nyembamba katikati ya mashamba ya mizabibu, na kushoto kwake kulikuwa na ukuta.
25 When the donkey saw the angel standing there, it walked very close to the wall [to try to get past the angel]. As a result, it bashed Balaam’s foot against the wall. So Balaam struck the donkey again.
Yule punda akamwona yule malaika wa BWANA tena. Akasogea zaidi ukutani na kuubana mguu wa Balaamu ukutani. Balaamu akampiga tena yule punda.
26 Then the angel went further along the road and stood at a place that was extremely narrow, with the result that the donkey could not get past at all.
Yule malaika wa BWANA akasogea mbele zaidi kwenye eneo jingine jembamba zaidi ambalo haikuwezekana kugeuka upande mwingine.
27 This time, when the donkey saw the angel, it lay down [on the ground] with Balaam sitting on top of it. Balaam became extremely angry, and he struck the donkey again with his walking stick.
Yule Punda akamwona tena yule malaika wa BWANA, akalala chini ya Balaamu. Hasira za Balaamu zikawaka, akampiga yule punda kwa fimbo yake.
28 Then Yahweh enabled the donkey to speak! It said to Balaam, “What bad thing have I done to you that caused you to strike me three times?”
Kisha BWANA akafungua kinywa cha punda na akaongea. Akamwambia Balaamu, “Nimekukosea nini kiasi kwamba umenipiga mara tatu?”
29 Balaam shouted, “I struck you because you have caused me to appear to be foolish! If I had a sword with me, I would kill you!”
Balaamu akamjibu yule punda, “Ni kwa sababu umenitendea kwa ujinga. Natamani kama ningekuwa na upanga mkononi mwangu, kama ningekuwa nao, sasa hivi ningekuwa nimekuua.”
30 But the donkey answered, “I am your own donkey [RHQ], the one that you have always ridden! Have I ever done anything like this previously?” Balaam said, “No.”
Yule punda akamwambia Balaamu, “Je, mimi si punda wako ambaye umenipanda maishani mwako mwote mpaka hivi sasa? Je, nimewahi kuwa na tabia ya kukufanyia hivi hapo awali?” Balaamu akasema “hapana.”
31 Then Yahweh enabled Balaam to see the angel standing on the road, holding a sword in his hand. Balaam [realized that it was an angel and] prostrated himself on the ground in front of the angel.
Basi BWANA akafungua macho ya Balaamu, na akamwona malaika wa BWANA amesimama barabarani akiwa na upanga mkononi mwake. Balaamu akainamisha kichwa chake chini.
32 The angel asked him, ‘(Why did you strike your donkey three times?/ You should certainly not have struck the donkey three times! [RHQ] I have come to block your path because what you are planning to do is wrong.
Yule malaika wa BWANA akamwambia, “Kwa nini umempiga punda wako mara tatu? Tazama, Nimekuja kama adui yako kwa sababu matendo yako kwangu yamekuwa maovu.
33 Three times your donkey saw me and turned away from me. If it had not done that, I would certainly have killed you already, but I would have allowed the donkey to live.”
Yule punda aliniona na akageuka kutoka kwangu mara tatu. Kama asingekuwa amegeuka kutoka kwangu, hakika ningekuwa nimekua na yeye kumwacha hai.
34 Then Balaam said to the angel, “I have sinned. But I did not realize that you were standing there, trying to block my path. So if you do not want me to continue going, I will return home.”
Balaamu akamwambia malaika wa BWANA, nimetenda dhambi. Sikujua kuwa ulisimama kinyume na mimi barabarani. Kwa hiyo sasa, kama haikupendezi, Nitageuka.”
35 But the angel replied, “I will allow you to go with these men, but you must say only what I tell you to say!” So Balaam went on with the leaders whom Balak [had sent].
Lakini yule malaika wa BWANA akamwambia Balaamu, “endelea na wale watu. Lakini utasema maneno nitakayokwambia tu.”Kwa hiyo Balaamu akaendelea na wale vioingozi wa Balaki.
36 When King Balak heard that Balaam was coming, he went to meet him at a Moab town alongside the Arnon [River] that was at the border of his own land.
Balaki aliposikia kuwa Balaamu alikuwa amekuja, alienda kukutana naye kule mjini Moabu pale Amoni, ambao uko mpakani.
37 [When he arrived where] Balaam was, he said to him, “I sent you [RHQ] a message saying that you should come immediately [RHQ]! Why did you not come immediately? [Did you think that] I was not able to pay you a lot of money for coming?”
Balaki akamwambia Balaamu, “Je, mimi sikutuma watu kukuita? Basi kwa nini hukuja kwangu? Je, mimi sina uwezo wa kukufanya uheshimike?”
38 Balaam replied, “I have come here now, but I am not able to say anything [that I want to]. I will say only the words that God tells me to say [MTY].”
Ndipo Balaamu alipomjibu Balaki, “Tazama, mimi nimekuja kwako. Je mimi sina mamlaka ya kusema chochote? Mimi ninaweza kusema maneno ambayo Mungu ameweka kinywani mwangu.”
39 Then Balaam went with Balak to Kiriath-Huzoth [town].
Balaamu akaenda na Balaki, na Wakafika Kiriathi Huzothi.
40 There Balak killed some cattle and sheep as sacrifices, and offered [parts of the meat] to Balaam and the leaders who were with him.
Kisha Balaki akatoa sadaka ya maksai na kondoo na kumpatia Balaamu baadhi ya hiyo nyama na wale viongozi waliokuwa pamoja naye.
41 [They slept there], and the next morning Balak took Balaam part way up [the mountain] to Bamoth-Baal [village]. From there, they could see some of the Israeli people who were down below.
Kesho yake asubuhi, Balaki akampeleka Balaamu mpaka juu mahali pa Baali. Kule juu Balaamu aliweza kuona sehemu tu ya kambi za Waisraeli.

< Numbers 22 >