< Numbers 13 >

1 Yahweh said to Moses/me,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Send some men to Canaan [land] to explore it. That is the land that I will give to you Israelis. Send men who are leaders in their tribes.”
“Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
3 So Moses/I did what Yahweh commanded him/me. He/I sent out twelve Israeli men who were all leaders of their tribes. He/I sent them from their/our camp at Paran in the desert.
Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
4 These are the names of the men [and the tribes they belonged to: ] Shammua, the son of Zaccur, from the tribe of Reuben;
Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Shaphat, the son of Hori, from the tribe of Simeon;
kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Caleb, the son of Jephunneh, from the tribe of Judah;
kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Igal, the son of Joseph, from the tribe of Issachar;
kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
8 Hoshea, the son of Nun, from the tribe of Ephraim;
kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Palti, the son of Raphu, from the tribe of Benjamin;
kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
10 Gaddiel, the son of Sodi, from the tribe of Zebulun;
kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
11 Gaddi, the son of Susi, from the tribe of Manasseh;
kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
12 Ammiel, the son of Gemalli, from the tribe of Dan;
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
13 Sethur, the son of Michael, from the tribe of Asher;
kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
14 Nahbi, the son of Vophsi, from the tribe of Naphtali;
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
15 and Geuel, the son of Maki, from the tribe of Gad.
kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
16 Those are the names of the men whom Moses/I sent out to explore Canaan. [Before they left], Moses/I gave Hoshea a new name, Joshua, [which means ‘Yahweh is the one who saves].’
Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
17 Before Moses/I sent them to explore Canaan, he/I said to them, “Go through the southern part of Canaan, and then go [north] into the hilly area.
Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
18 See what the land is like. See if the people who live there are strong or weak. See if there are many people or only a few people.
Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
19 Find out what kind of land they live in [RHQ]. Is it good or bad? Find out about the towns in which they live [RHQ]. Do they have walls around them or not?
Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
20 Find out about the soil [RHQ]. Is it (fertile/good for growing crops) or not? Find out if there are trees there [RHQ]. Try to bring back some of the fruit that grows in that land.” [He/I said that because] it was the beginning of the time to harvest grapes.
Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
21 So those men went to Canaan. They went [through the entire land], from the Zin desert [in the south] all the way to Rehob [town] near Lebo-Hamath [in the north].
Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
22 In the south, they went to Hebron, where Ahiman, Sheshai, and Talmai, [huge men] descended from Anak, lived. Hebron was a city that was built seven years before Zoan [city] was built in Egypt.
Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
23 In one valley, they cut from a grapevine one cluster of grapes. [Because it was very large, they needed] two men to carry it on a pole. They also picked some pomegranates and some figs [to carry back to their camp].
Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
24 They called that place Eshcol [which means ‘cluster’] because they had cut that [huge] cluster of grapes there.
Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
25 After they explored the land for 40 days, they returned to their camp.
Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 They came to Aaron and Moses/me and the rest of the Israeli people in the desert at Paran. They reported to everyone what they had seen. They also showed them the fruit that they had brought back.
Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
27 But this is what they reported to Moses/me: “We arrived in the land that you sent us to explore. It is truly a beautiful land, and it is very fertile [IDM]. Here is some of the fruit.
Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
28 But the people who live there are very strong. Their cities are large and are surrounded by walls. We even saw some of the [huge] descendants of Anak there.
Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
29 The descendants of Amalek live in the southern part [of the land], and the descendants of Heth, Jebus, and Amor live in the hilly area [to the north]. The descendants of Canaan live along the coast of the [Mediterranean] sea and along the Jordan [River].”
Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
30 [When they said that, the people were afraid and started to cry out very loudly]. But Caleb told the people who were standing near Moses/me to be quiet. Then he said, “We should go there and take the land, because we are certainly able to conquer it!”
Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
31 But the men who had gone with him said, “No, we cannot attack [and defeat] those people! They are much stronger than we are!”
Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
32 So those men gave to the Israeli people a bad report about the land that they had explored. They said, “The land that we explored is very large; we cannot conquer it. And all the people whom we saw are very tall.
Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
33 We even saw the descendants of Nephili there. The descendants of Anak [whom we saw there] are descended from the giant Nephili people. When we saw them, we felt [as small] as grasshoppers [SIM], and they thought that we looked like grasshoppers too!”
Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”

< Numbers 13 >