< Nehemiah 9 >

1 On October 31, the people gathered together again. They (fasted/abstained from eating food), they wore clothes made from rough cloth, and they put dirt on their heads [to show that they were sorry for their sins].
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi ule ule, Waisraeli walikusanyika pamoja, wakifunga na kuvaa nguo za gunia na kujitia mavumbi vichwani mwao.
2 The Israeli people separated themselves from all the foreigners. They stood there and confessed their sins and the sins that their ancestors had committed.
Wale wa uzao wa Israeli walijitenga na wageni wote. Wakasimama mahali pao, na kuungama dhambi zao na uovu wa baba zao.
3 The scroll that contained the laws of Yahweh, the God whom they [worshiped], was read to them for three hours. Then for three more hours they confessed their sins and they worshiped Yahweh.
Wakasimama pale walipokuwa, wakasoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Bwana Mungu wao kwa muda wa robo siku, na wakatumia robo nyingine kwa kuungama dhambi na kumwabudu Bwana Mungu wao.
4 [Some of] the descendants of Levi were standing on the stairs. They were Jeshua, Bani, Kadmiel, Shebaniah, Bunni, Sherebiah, [another] Bani, and Kenani.
Walawi wafuatao walikuwa wamesimama kwenye ngazi: Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia, Bani na Kenani. Hawa walimlilia Bwana Mungu wao kwa sauti kubwa.
5 Then [the leaders of] the Levites called out to the people. They were Jeshua, Bani, Hashabneiah, Sherebiah, Hodiah, Shebaniah, and Pethahiah. They said, “While you are standing there, praise Yahweh your God, who has always lived and will live forever!” [Then one of them continued by praying this to God], “Yahweh, we praise your glorious name! You are much greater than anything that we can think about or talk about!
Nao Walawi Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabnea, Sherebia, Hodia, Shebania na Pethahia wakasema: “Simameni mkamsifu Bwana Mungu wenu, yeye ambaye ni Mungu tangu milele hata milele. “Libarikiwe jina lake tukufu, litukuzwe juu ya baraka zote na sifa.
6 “You only are God. You made the sky and the heavens and all the stars. You made the earth and everything that is on it, and you made the seas/oceans and everything that is in them. You are the one who gives life to everything and helps them remain alive. All the angels who are in heaven worship you.
Wewe peke yako ndiwe Bwana. Uliziumba mbingu, hata mbingu za mbingu na jeshi lote la mbinguni, dunia na vyote vilivyo ndani yake, na pia bahari na vyote vilivyomo ndani yake. Huvipa vitu vyote uhai, nalo jeshi la mbinguni linakuabudu wewe.
7 “Yahweh, you are God. You chose Abram and brought him out of Ur [city] in Chaldea [region]. You gave him a new name, Abraham.
“Wewe ni Bwana Mungu uliyemchagua Abramu na kumtoa kutoka Uru ya Wakaldayo, nawe ukamwita Abrahamu.
8 You saw that he was trustworthy. Then you made (an agreement with/a promise to) him, saying that you would give [to him and] to his descendants the land that the descendants of Canaan, Heth, Amor, Periz, Jebus, and Girgash lived in. And you have done what you promised, because you always do what is right.
Uliona kuwa moyo wake ni mwaminifu kwako, nawe ukafanya Agano naye kuwapa wazao wake nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi. Umetimiza ahadi yako kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 “You saw what our ancestors were suffering in Egypt. You heard them cry to you for help when they were at the Red Sea.
“Uliona mateso ya baba zetu huko Misri, ukasikia kilio chao huko Bahari ya Shamu.
10 Because you knew that the leaders of Egypt were treating our ancestors very arrogantly, you performed many kinds of miracles that caused the king and his officials and all his people to suffer. As a result, you became famous then, and you are still famous!
Ulituma ishara za miujiza na maajabu dhidi ya Farao, dhidi ya maafisa wake wote na watu wote wa nchi yake, kwa kuwa ulifahamu jinsi Wamisri walivyowafanyia ufidhuli. Ukajifanyia jina linalodumu hadi leo.
11 You caused the Red Sea to divide, with the result that your people walked through it on the ground without [getting their feet] wet. [After they were all safely on the other side, ] you [caused the water to come back again], and you hurled into the deep water the [soldiers of the Egyptian army] that were pursuing our ancestors. Their soldiers sank into the deep sea like stones!
Ukagawa bahari mbele yao, ili waweze kupita katikati yake penye nchi kavu, lakini uliwatupa Wamisri waliowafuatilia katika vilindi, kama jiwe kwenye maji mengi.
12 During each day you led our ancestors with a bright cloud that resembled a huge pillar, and each night you led them by a flaming cloud that gave them light to show them where to walk.
Mchana uliwaongoza kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto kuwamulikia njia iliyowapasa kuiendea.
13 “When our ancestors were at Sinai Mountain, you came down from heaven and spoke to them. You gave them many regulations and instructions that are just and reliable, and you gave them commands and laws that are good.
“Ulishuka katika Mlima Sinai, ukanena nao kutoka mbinguni. Uliwapa masharti na sheria zile ambazo ni za kweli na haki, pia amri na maagizo mazuri.
14 You taught them about your holy (Sabbath/day of rest), and you gave many kinds of laws to your servant Moses for him to tell to the people.
Uliwafahamisha Sabato yako takatifu na ukawapa amri, maagizo na sheria kupitia mtumishi wako Mose.
15 When they were hungry, you gave them manna from the sky; and when they were thirsty, you gave them water from a rock. You commanded them to go and take, from the people who lived there, the land which you had promised to give to them.
Katika njaa yao uliwapa mkate kutoka mbinguni, na katika kiu yao uliwatolea maji kutoka kwenye mwamba. Uliwaambia waingie na kuimiliki nchi ambayo ulikuwa umeapa kuwapa kwa mkono ulioinuliwa.
16 “But our ancestors were very proud and stubborn [IDM], and they did not do what you commanded them to do.
“Lakini wao, baba zetu, wakawa na kiburi na shingo ngumu, nao hawakutii maagizo yako.
17 They refused to heed you, and they forgot about all the miracles that you had performed for them. Instead, they became stubborn [IDM], and they appointed someone to lead them back to Egypt, where they would be slaves again! But you are a God who forgives us and who is kind and merciful [to us]. You do not quickly become angry. You always faithfully love us.
Wakakataa kusikiliza na kushindwa kukumbuka miujiza uliyoifanya miongoni mwao. Wakawa na shingo ngumu, na katika uasi wao wakamchagua kiongozi ili warudi kwenye utumwa wao. Lakini wewe ni Mungu mwenye kusamehe, mwenye neema na mwingi wa huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa upendo. Kwa hiyo hukuwaacha,
18 So, even though their [leaders] made an idol that resembled a calf and insulted you by saying [about the idol], ‘This is our god, who brought you up out of Egypt,’ you did not desert them.
hata wakati walijitengenezea sanamu ya ndama ya kusubu na kusema, ‘Huyu ni mungu wenu, aliyewapandisha kutoka nchi ya Misri,’ au walipofanya makufuru makubwa.
19 “Because you always act mercifully, you did not abandon them when they were in the desert. The bright cloud which was like a huge pillar continued to lead them during the daytime, and the fiery cloud showed them where to walk at night.
“Kwa sababu ya huruma zako kuu hukuwaacha jangwani. Wakati wa mchana ile nguzo ya wingu haikukoma kuwaongoza katika njia yao, wala nguzo ya moto haikuacha kuwamulikia usiku njia iliyowapasa kuiendea.
20 You sent your good Spirit to instruct them. You continued to provide water when they were thirsty.
Uliwapa Roho wako mwema ili kuwafundisha. Hukuwanyima mana yako vinywani mwao, nawe ukawapa maji kwa ajili ya kiu yao.
21 For 40 years you took care of them in the desert. During all that time, they had everything [that they needed]. Their clothes did not wear out, and their feet did not swell up [even though they were continually walking].
Kwa miaka arobaini uliwatunza jangwani. Hawakukosa chochote, na nguo zao hazikuchakaa wala miguu yao haikuvimba.
22 “You helped our ancestors to defeat armies of great kings who ruled many people-groups. By doing that, you enabled our ancestors to (occupy/live in) even the most distant places in this land. They occupied the land over which King Sihon ruled from Heshbon [city] and the land over which King Og ruled in [the] Bashan [area].
“Uliwapa falme na mataifa, ukiwagawia hata mipaka ya mbali. Wakaimiliki nchi ya Sihoni mfalme wa Heshboni, na nchi ya Ogu mfalme wa Bashani.
23 You caused our ancestors’ descendants to become as numerous as the stars in the sky, and you brought them into this land, the land that you told their fathers to enter and occupy.
Uliwafanya wana wao kuwa wengi kama nyota za angani, nawe ukawaleta katika nchi ambayo uliwaambia baba zao kuingia na kuimiliki.
24 Their sons went in and took the land [from the people that lived there]. You enabled them to defeat the descendants of Canaan who lived here in this land. You enabled them to conquer the descendants of Canaan and their kings and the people whom they ruled. You enabled our ancestors to do to those people whatever they wanted to do.
Wana wao wakaingia na kuimiliki nchi. Uliwatiisha Wakanaani mbele yao, walioishi katika nchi, ukawatia Wakanaani mikononi mwao, pamoja na wafalme wao na watu wa nchi, wawafanyie kama wapendavyo.
25 Our ancestors captured cities that had walls around them, and they took possession of fertile land. They took possession of houses that were full of good things, where there were wells that were already dug. They took possession of many vineyards and groves of olive trees and fruit trees. They ate all that they wanted to and became fat. They were delighted in all these good things that you gave to them.
Wakateka miji yenye ngome na nchi yenye rutuba, wakamiliki nyumba zilizojazwa na vitu vizuri vya kila aina, visima vilivyochimbwa tayari, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni na miti yenye matunda kwa wingi. Wakala, wakashiba nao wakanawiri sana, wakajifurahisha katika wema wako mwingi.
26 “But they disobeyed you and rebelled against you. They (turned their backs on/rejected) your laws. They killed the prophets who warned them that they should return to you. They badly insulted you.
“Lakini hawakukutii nao wakaasi dhidi yako, wakatupa sheria zako nyuma yao. Wakawaua manabii wako, waliowaonya ili wakurudie, na wakafanya makufuru makubwa.
27 So you allowed their enemies to defeat them. But when their enemies caused them to suffer, they called out to you. You heard them from heaven, and because you are very merciful, you sent them people to help them, and those leaders rescued them from their enemies.
Hivyo ukawatia mikononi mwa adui zao, ambao waliwatesa. Lakini walipoteswa, wakakulilia wewe. Kutoka mbinguni uliwasikia, nawe kwa huruma zako kuu ukawapa waokozi, waliowaokoa kutoka mikononi mwa adui zao.
28 “But after there was a time of peace again, our ancestors again did things that displeased you. So again you allowed their enemies to conquer them. But whenever they cried out to you again [to help them], you heard them from heaven, and because you act mercifully, you rescued them many times.
“Lakini mara walipokuwa na raha, wakafanya maovu tena machoni pako. Kisha ukawaacha mikononi mwa adui zao, nao wakawatawala. Walipokulilia tena, ukasikia kutoka mbinguni, na kwa huruma zako ukawaokoa kila mara.
29 “You warned them that they should again [obey] your laws, but they became proud and stubborn, and they disobeyed your commands. They sinned by disobeying what you commanded them to do, the things that would enable them to live a good long life [if they obeyed them]. They stubbornly refused [IDM] to listen to you and continued sinning.
“Ukawaonya warudi katika sheria yako, lakini wakawa na kiburi na hawakutii amri zako. Wakatenda dhambi dhidi ya maagizo yako ambayo kwayo mtu ataishi kama akiyatii. Kwa ukaidi wakakugeuzia kisogo, wakawa na shingo ngumu na wakakataa kusikiliza.
30 You were patient with them for many years. You warned them trough [the messages] your Spirit gave to the prophets. But they did not (heed/pay attention to) those messages. So again you allowed [the armies of] other nations to defeat them.
Kwa miaka mingi ulikuwa mvumilivu kwao. Kwa njia ya Roho wako ukawaonya kupitia manabii wako. Hata hivyo hawakujali, basi ukawatia mikononi mwa mataifa jirani.
31 But because you act very mercifully, you did not get rid of them completely or abandon them [forever]. You are a very gracious/kind and merciful God!
Lakini kwa rehema zako kuu hukuwakomesha wala kuwaacha, kwa kuwa wewe ni Mungu mwenye neema na rehema.
32 “Our God, you are great! You are mighty! You are awesome! You faithfully love us as [you promised in] your agreement with us that you would do! But now we are experiencing great difficulties/hardships. Great troubles have come to us, to our kings, to our [other] leaders, to our priests, and to our prophets. We have been experiencing these troubles since [the armies of] the kings of Assyria [conquered us], and we are still experiencing them. We ask that you sincerely think about [LIT] all these things.
“Basi sasa, Ee Mungu wetu, uliye mkuu, mwenye nguvu na Mungu wa kuogofya, mwenye kushika agano lake la upendo, usiache taabu hizi zote zionekane kuwa kitu kidogo mbele za macho yako, taabu hizi zilizotupata, juu ya wafalme wetu na viongozi, juu ya makuhani wetu na manabii, juu ya baba zetu na watu wako wote, tangu siku za wafalme wa Ashuru hadi leo.
33 [We know that] you acted justly each time that you punished us. We have sinned greatly, but you have treated us fairly.
Katika hayo yote yaliyotupata, umekuwa mwenye haki, na umetenda kwa uaminifu, wakati sisi tumetenda mabaya.
34 Our kings and other leaders and our priests and our other ancestors did not obey your laws. They did not heed your commands or the warnings that you gave to them.
Wafalme wetu, viongozi wetu, makuhani wetu na baba zetu hawakufuata sheria yako. Hawakuzingatia amri zako wala maonyo uliyowapa.
35 Even when they had their own kings, and they enjoyed the good things that you did for them in this large and fertile land that you gave to them, they did not serve you. They refused to quit doing what was evil.
Hata walipokuwa wangali katika ufalme wao, wakiufurahia wema wako mkuu katika nchi kubwa na yenye rutuba uliyowapa, hawakukutumikia wala kugeuka kutoka njia zao mbaya.
36 “So now we are [like] slaves here in this land that you gave to our ancestors, the land that you gave to them in order that they could enjoy all the good things that grow here.
“Lakini tazama, sisi ni watumwa leo, watumwa katika nchi uliyowapa baba zetu ili wapate kula matunda yake na vitu vingine vizuri inayozalisha.
37 Because we have sinned, [we cannot eat the things that grow here]. The kings that now rule over us are enjoying the things that grow here. They rule us and [take] our cattle. We have to serve them and do the things that please them. We are experiencing great misery/distress.
Kwa sababu ya dhambi zetu, mavuno yake mengi huenda kwa wafalme uliowaweka watutawale. Wanatawala juu ya miili yetu na mifugo yetu kama wapendavyo. Tuko katika dhiki kuu.
38 “However, we [Israeli] people now are making an agreement/promise [to obey you], and we are writing this agreement/promise [on a scroll]. We will write on it the names of our leaders and the names of the Levites and the names of the priests, and then we will seal it.”
“Kwa sababu ya haya yote, tunajifunga katika mapatano, na kuyaandika, nao viongozi wetu, Walawi wetu na makuhani wetu wanatia mihuri yao.”

< Nehemiah 9 >