< Nehemiah 12 >

1 [Many] priests and [other] descendants of Levi returned (from Babylonia/to Jerusalem) with Zerubbabel and Jeshua. They included Seraiah, Jeremiah, Ezra,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amariah, Malluch, Hattush,
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Shecaniah, Rehum, Meremoth,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Iddo, Ginnethon, Abijah,
Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Mijamin, Moadiah, Bilgah,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Shemaiah, Joiarib, Jedaiah,
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Sallu, Amok, Hilkiah, and Jedaiah. All those men were leaders of the priests during the time that Jeshua [was the Supreme Priest].
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 [Some of the other] descendants of Levi who returned were Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, and Mattaniah. They were in charge of singing songs to thank [God].
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 Bakbukiah, Unni, and other descendants of Levi formed a choir that stood opposite the other group [and sang in reply to them].
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 Jeshua [who was the Supreme Priest] was the father of Joiakim, who was the father of Eliashib, who was the father of Joiada,
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 who was the father of Jonathan, who was the father of Jaddua.
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 When Joiakim was the Supreme Priest, these were the leaders of the clans of priests: Meraiah, from [the clan of] Seraiah; Hananiah, from [the clan of] Jeremiah;
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 Meshullam, from [the clan of] Ezra; Jehohanan, from [the clan of] Amariah;
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 Jonathan, from [the clan of] Malluch; Joseph, from [the clan of] Shecaniah;
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 Adna, from [the clan of] Harim; Helkai, from [the clan of] Meremoth/Maraioth;
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 Zechariah, from [the clan of] Iddo; Meshullam, from [the clan of] Ginnethon;
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 Zicri, from [the clan of] Abijah. There was also a leader from [the clan of] Miniamin; Piltai, from [the clan of] Moadiah;
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 Shammua, from [the clan of] Bilgah; Jehonathan, from [the clan of] Shemaiah;
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 Mattenai, from [the clan of] Joiarib; Uzzi, from [the clan of] Jedaiah;
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 Kallai, from [the clan of] Sallu/Sallai; Eber, from [the clan of] Amok;
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 Hashabiah, from [the clan of] Hilkiah; and Nethanel, from [the clan of] Jedaiah.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 During the years that Eliashib, Joiada, Johanan, and Jaddua [were Supreme Priests], they (wrote/kept a list of) the names of the clans who were descendants of Levi. When Darius was the king of Persia, they stopped writing that list.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 They wrote the names of the leaders of the clans who were descendants of Levi in the Book of Events [in Israel], but they stopped writing those names when Eliashib’s grandson Johanan [was the Supreme Priest].
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 These are the leaders of the clans [who are] descendants of Levi: Hashabiah, Sherebiah, Jeshua, Binnui, Kadmiel and others who were divided into two groups. The two groups faced each other, one group replying to the other, during the time that they praised and thanked God. They did that just as King David, the man who served God well, had instructed.
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 These singers included Mattaniah, Bakbukiah, and Obadiah. The men who guarded the storerooms close to the gates [of the temple] were Meshullam, Talmon, and Akkub.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 They did that work during the time that Joiakim, who was the son of Jeshua and the grandson of Jehozadak, [was the Supreme Priest, ] and I was the governor, and Ezra was the priest who knew the Jewish laws very well.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 When we dedicated the wall around Jerusalem, we summoned the descendants of Levi [who help the priests] from the nearby places where they [were living]. We asked them to [join with us to] celebrate when we dedicated the wall. We wanted them to sing songs to thank [Yahweh] and make music by playing cymbals and harps and other stringed instruments.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 We summoned the descendants of Levi who habitually sang together. They came to Jerusalem from nearby areas [where they had settled], and from places around Netophah [town southeast of Jerusalem],
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 and from three places [northeast of Jerusalem]—Beth Gilgal [city] and the areas around Geba and Azmaveth. Those singers had built villages to live in near Jerusalem.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 [When they came to Jerusalem], the priests and [other] descendants of Levi [who help the priests] performed rituals to cause themselves to be acceptable to God, and then they performed similar rituals to purify the [other] people, the gates, and the wall.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Then I gathered together the leaders of Judah on top of the wall, and I appointed them to lead two large groups to march around the city [on top of the wall], thanking God. [As they faced the city, ] one group walked to the right toward the Dung Gate.
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 Behind their leaders marched Hoshaiah and half of the leaders of Judah.
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 Behind them marched a group of priests who were blowing trumpets. They were Azariah, Ezra, Meshullam, Judah, Benjamin, Shemaiah, and Jeremiah. Next came Zechariah, the son of Jonathan, the son of Shemaiah, the son of Mattaniah, the son of Micaiah, the son of Zaccur, a descendant of Asaph.
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 Behind them marched other members of Zechariah’s clan: Shemaiah, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, Judah, and Hanani. They all were playing the same kinds of musical instruments that King David had played [many years previously]. Ezra, the man who knew the Jewish laws very well, marched in front of this group.
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 When they reached the Fountain Gate, they went up the steps to David’s City, past his palace, and then to the wall at the Water Gate, on the east side [of the city].
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 The other group of those who were thanking [Yahweh] marched to the left on top of the wall. I followed them with half of the people. [We marched] past the Tower of the Ovens to the Broad Wall.
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 [From there we marched] past Ephraim Gate, Jeshanah Gate, the Fish Gate, the Tower of Hananel, the Tower of the Hundred Soldiers, to the Sheep Gate. We finished marching near the gate into the temple.
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 Both the groups reached the temple while they were thanking God. They stood in their places there. The leaders who were with me [also stood with me in our places].
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 My group included these priests who were [all blowing] trumpets: Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah, Hananiah,
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 [another] Maaseiah, Shemaiah, Eleazar, Uzzi, Jehohanan, Malchijah, Elam, and Ezer. The singers, whose leader was Jezrahiah, sang loudly.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 [After we went outside the temple, ] we offered many sacrifices. We men all rejoiced because God had caused us to be very happy. The women and the children also rejoiced. People far away could hear the noise that we made there in Jerusalem.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 On that day, men were appointed {they appointed men} to be in charge of the storerooms where they kept the money that people contributed [for the temple]. They also kept there [the other things that the people contributed—] the tithes and the first part of the grain and fruit that was harvested each year. Those men collected those things from the fields/farms near the cities, and [took them to Jerusalem and] gave them to the priests and the [other] descendants of Levi, as [Moses had said in his] laws that they should do. All the Israeli people were happy about the work that the priests and the descendants of Levi did,
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 because they performed the rituals to purify things, and the other rituals that God had commanded. The musicians in the temple also did their work as King David and his son Solomon had declared that they should do.
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 Ever since the time that David had been the king and Asaph had been his chief musician, the musicians had led the people while they sang songs to praise and thank God.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 During the years that Zerubbabel and I governed the Israeli people, they all contributed the food that the singers and temple gatekeepers needed each day. They gave (a tithe/10%) of their crops to the descendants of Levi [who helped the priests], and those descendants of Levi gave (a tithe/10%) of that to [the priests, who were] descendants of Aaron [the first Supreme Priest].
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

< Nehemiah 12 >