< Micah 7 >

1 I am very miserable/frustrated! I am like [SIM] someone who is hungry, [who searches for fruit to pick] after all the fruit had been picked and who finds no grapes or figs to eat.
Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
2 [All] the godly people have disappeared from this land; there is not one of them left. [The people who are left] are all murderers [MTY]; [it is as though] everyone is eager to kill his fellow countryman.
Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
3 They [all] use both hands to do what is evil. [Government] officials and judges [all] ask for bribes. Important people tell others what they want, and they plot/scheme together [about how to get it done].
Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
4 [Even] the best people are [as worthless] [SIM] as briers; the people [who are considered by others to be] [IRO] the most honest are worse than clumps of thornbushes. But, [Yahweh] will soon judge them; now is the time that he will punish people, a time when they will be [very] confused [because of being defeated].
Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
5 [So], do not trust anyone! Do not trust [even] a friend; [even] be careful what you say to your wife whom you love!
Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
6 Boys will despise their fathers, and girls will defy their mothers. Women will defy their mothers-in-law. Your enemies will be those who live in your own houses.
Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
7 As for me, I wait for Yahweh [to help me]. I confidently expect that God, my Savior, will answer me [when I pray].
Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
8 You who are our enemies, do not gloat/rejoice about [what has happened to] us, [because even] if we have experienced disasters, [those disasters will end and] we will be restored. [Even] if [it is as though] we are sitting in the darkness, Yahweh will be our light.
Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
9 We must be patient while Yahweh punishes us because we have sinned against him. But later, [it will be as though] he will go to court and defend us, and he will make sure that the judge makes a right decision about us. [It will be as though] he will bring us out into the light, and we will see it when he rescues us.
Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
10 Our enemies will [also] see that, and they will be disgraced because they [ridiculed us], saying “Why is [RHQ] Yahweh, that God of yours, [not helping you]?” But with our own eyes we will see them when they are defeated; we will see them trampled like [SIM] mud in the streets.
Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
11 [You people of Israel, ] at that time your cities will be rebuilt, and your territory will become larger.
Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
12 [People from many countries will come to honor you]: people from Assyria and from [near] the [Euphrates] River [in the east] and from Egypt [in the south], from distant seas, and from many mountains.
Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
13 But [the other countries on] the earth will become desolate because of the [evil] things that their people have done.
Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
14 Yahweh, protect your people like [MET] [a shepherd protects his sheep] by using his walking stick; lead your people [MET] whom you have chosen to belong to you. [Even though some of them] live by themselves in a forest, give them the fertile pastureland in the Bashan and Gilead [regions] that they possessed long ago.
Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
15 [Yahweh says/replies], “[Yes], I will perform miracles for you like the miracles that I performed when I rescued your [ancestors] from [being slaves in] Egypt.”
“Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
16 [People from many] nations will see [what Yahweh does for you], and they will be ashamed because they do not have any power. They will put their hands over their mouths and their ears [because they will be very amazed because of what Yahweh does], [and they will not be able to say anything or hear anything].
Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
17 [Being very humiliated, ] they will crawl on the ground [MTY] like [SIM] snakes. They will come out of their homes trembling, and stand revering Yahweh our God. They will be very afraid of him, and will tremble in front of him.
Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
18 [Yahweh], there is no [RHQ] God like you; you forgive the sins [DOU] that were committed by the people who have survived, the people who belong to you. You do not remain angry forever; you are very happy [to show us] that you faithfully love [us].
Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
19 You will again act kindly/compassionately toward us. You will get rid of [the scroll on which you have written] the sins that we have committed [as though you were] trampling it under your feet or throwing it into the deep ocean.
Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
20 You will show that you faithfully [do what you promised for us] and faithfully love us, just like you solemnly promised long ago to our ancestors Abraham and Jacob that you would do.
Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.

< Micah 7 >