< Mark 15 >

1 Very early in the morning the chief priests met together with [the rest of] the Jewish council, [in order to decide how to accuse Jesus before the Roman governor. Their guards] tied Jesus’ hands [again]. They took him to [the house of] Pilate, [the governor, and they started to accuse him, saying] “[Jesus is claiming that he is a king!]!”
Asubuhi na mapema wakuu wa makuhani walikutana pamoja na wazee na waandishi na baraza zima la wazee. Kisha wakamfunga Yesu wakampeleka kwa Pilato. Pilato akamwuliza, “wewe ni Mfalme wa Wayahudi?”
2 Pilate asked Jesus, “Do you [claim to be] the king of the Jews?” Jesus answered him, “You yourself have said so.”
“Akamjibu, “Wewe umesema hivyo.”
3 Then the chief priests claimed that Jesus had done many bad things.
Wakuu wa makuhani wakaeleza mashitaka mengi juu ya Yesu.
4 So Pilate asked him again, “Don’t you have anything to say? Listen to how many bad things they are saying that you [have done]!”
Pilato akamwuliza tena, “Hujibu chochote? Huoni jinsi wanavyokushtaki kwa mambo mengi?
5 But [even though Jesus was not guilty], he did not say anything more. The result was that Pilate was very much surprised.
Lakini Yesu hakumjibu Pilato, na hiyo ilimshangaza.
6 It was the governor’s custom [each year] during the [Passover] celebration to release [one person who was in prison. He customarily released] whichever prisoner the people requested.
Kwa kawaida wakati wa sikukuu humfungulia mfungwa mmoja, mfungwa waliyemwomba.
7 [At that time] there was a man called Barabbas who had been {whom [the soldiers had]} [put in prison with some other men]. Those men had murdered [some soldiers] when they rebelled [against the Roman government].
Kulikuwapo wahalifu gerezani, miongoni mwa wauaji kati ya walioasi wanaotumikia makosa yao. Alikuwepo mtu mmoja aitwaye Baraba.
8 A crowd approached [Pilate] and asked him [to release someone], just like he customarily did for them [during the Passover celebration].
Umati ulikuja kwa Pilato, na kumwomba afanye kama alivyofanya huko nyuma.
9 Pilate answered them, “Would you like me to release for you the [man whom you] Jewish [people say is your] king?”
Pilato akawajibu na kusema, “Mnataka niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?”
10 [He asked this] because he realized what the chief priests were wanting to do. They were accusing Jesus because they were jealous of him [because many people were becoming his disciples].
Kwa kuwa alijua ni kwa sababu ya wivu wakuu wa makuhani walimkamata Yesu na kumleta kwake.
11 But the chief priests urged the crowd [to request] that Pilate release Barabbas for them instead [of Jesus].
Lakini wakuu wa makuhani walichochea umati kupiga kelele kwa sauti kwamba afunguliwe Baraba badala yake.
12 Pilate said to them again, “[If I release Barabbas], what do you want me to do with the man whom [some of] you Jews say is [your] king?”
Pilato akawajibu tena na kusema, “Nimfanye nini Mfalme wa Wayahudi?
13 Then they shouted again, “[Command that your soldiers] crucify him!”
Wakapiga kelele tena, “Msulibishe!”
14 Then Pilate said to them, “Why? What crime has he committed?” But they shouted even louder, “[Command your soldiers to] crucify him!”
Pilato akasema, “Amefanya jambo gani baya?” Lakini wakazidi kupiga kelele zaidi na zaidi “Msulibishe.”
15 So, because Pilate wanted to please the crowd, he released Barabbas for them. Then, after [his soldiers] had whipped Jesus with leather straps into which they had fastened metal pieces, [Pilate told the soldiers to take him away] in order that he would be crucified {they would crucify him}.
Pilato akitaka kuwaridhisha umati, akawafungulia Baraba. Akampiga Yesu mijeledi kisha akamtoa ili asulibiwe.
16 The soldiers took Jesus into the [courtyard of the] palace [where Pilate lived]. That place was the government headquarters. Then they summoned the whole (cohort/group of soldiers) [who were on duty there].
Askari walimwongoza hadi ndani ya ua (ule ulio ndani ya kambi) na walikusanyika pamoja kikosi cha askari.
17 [After the soldiers gathered together], they put a purple robe on Jesus. Then they placed on his head a crown that they made from [branches of] thornbushes. [They did those things in order to ridicule him by pretending that he was a king].
Wakamvika Yesu kanzu ya rangi ya zambarau, na wakasokota taji ya miiba wakamvika.
18 Then they greeted him [like they would greet a king, in order to ridicule him], saying, “Hooray for the King [who rules] the Jews!”
Wakaanza kumdhihaki na kusema, “Salam, Mfalme wa Wayahudi!”
19 They repeatedly struck his head with a reed and spat on him. By kneeling down, they [pretended to honor] him.
Wakampiga kichwani kwa mwanzi na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake kwa kumheshimu.
20 When they had finished ridiculing him, they pulled off the purple robe. They put his own clothes on him, and then they led him outside [of the city] in order to nail him to a cross.
Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua ile kanzu ya rangi ya zambarau na kumvika mavazi yake, na wakamtoa nje kwenda kumsulibisha.
21 [After Jesus carried his cross a short distance], a man named Simon from Cyrene [city came along]. He was the father of Alexander and Rufus. He was passing by while he was returning [home] from outside [the city. The soldiers] compelled Simon to carry the cross [for Jesus].
Wakamlazimisha mpita njia kumsaidia, aliyekuwa anaingia mjini kutoka shamba. Aitwaye Simoni Mkirene (baba yake Iskanda na Rufo); wakamlazimisha kubeba msalaba wa Yesu.
22 They brought them both to a place that they [call] Golgotha. That name means, ‘a place [like] a skull’.
Askari wakampeleka Yesu mahali paitwapo Goligotha (maana ya tafsiri hii ni, Sehemu ya Fuvu la kichwa).
23 Then they tried to give Jesus wine that was {that they} mixed with [medicine called] myrrh. [They wanted him to drink it so that he would not feel so much pain when they crucified him]. But he did not drink it.
Wakampa mvinyo iliyochanganywa na manemane, lakini hakunywa.
24 [Some] of the [soldiers took his clothes]. Then they nailed him to a cross. Afterwards, they divided his clothes among themselves by gambling with [something like] dice. They did this [in order to determine] which [piece of clothing] each one would get.
Wakamsulibisha na wakagawana mavazi yake, wakayapigia kura kuamua kipande atakachopata kila askari.
25 It was nine o’clock in the morning when they crucified him.
Yapata saa tatu asubuhi walipomsulibisha.
26 They [attached to the cross above Jesus’ head] a sign on which it had been written {someone had written} the reason why [they were nailing him to the cross]. [But all] that it said was, “The King of the Jews.”
Wakaweka juu yake ubao ulioandikwa shitaka, “Mfalme wa Wayahudi.”
27 They also nailed to crosses two men who were bandits. They nailed one to a cross at the right side [of Jesus] and one to a cross at the left side [of Jesus].
Walimsubisha pamoja na majambazi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine kushoto kwake.
(Zingatia: Mstari huu, “Na maandiko yakatimia yaliyonena” haumo katika nakala za kale).
29 The people who were passing by insulted him by shaking their heads as [if here were an evil man]. They said, “Aha! You said that you would destroy the Temple and then you would build it again within three days.
Nao waliokuwa wakipita walimtukana, wakitikisa vichwa vyao wakisema, “Aha! wewe utakayevunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu,
30 [If you could do that, then] rescue yourself by coming down from the cross!”
jiokoe mwenyewe na ushuke chini toka msalabani!”
31 The chief priests, along with the men who taught the [Jewish] laws, also [wanted to] make fun of Jesus. So they said to each other, “He [claims to have] saved others [from their sicknesses] [IRO] but he cannot save himself!
Kwa namna ile ile wakuu wa makuhani walimdhihaki wakisemezana, pamoja na waandishi na kusema, “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe.
32 He said, ‘I am the Messiah, I am the King who [rules the people of] Israel.’ [If his words are true], he should come down now from the cross! Then we will believe [him]!” The [two] men who were crucified beside him also insulted him.
Kristo Mfalme wa Israel, shuka chini sasa toka msalabani, ili tuweze kuona na kuamini.” Na wale waliosulubiwa pamoja naye pia walimdhihaki.
33 At noon the whole land became dark, [and it stayed dark] until three o’clock in the afternoon.
Ilipofika saa sita, giza likaja juu ya nchi yote hadi saa tisa.
34 At three o’clock Jesus shouted loudly, “Eloi, Eloi, lama sabachthani?” That means, “My God, my God, why have you deserted me?”
Wakati wa saa tisa, Yesu alipiga kelele kwa sauti kubwa, “Eloi, Eloi, lama sabaktani?” ikiwa na maana “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
35 When some of the people who were standing there heard [the word ‘Eloi’, misunderstanding it], they said, “Listen! He is calling for [the prophet] Elijah!”
Baadhi ya hao waliosimama waliposikia wakasema, “Tazama, anamwita Eliya.”
36 One of them ran and filled a sponge with sour wine. He placed it on [the tip of] a reed, and then he [held it] up for [Jesus] to suck out [the wine that was in] it. [While he was doing that, someone] said, “Wait! Let’s see whether Elijah will come to take him down [from the cross]!”
Mtu mmoja akakimbia, akajaza siki katika sponji na kuiweka juu ya mti wa mwanzi, akampa ili anywe. Mtu mmoja akasema, “Ngoja tuone kama Eliya atakuja kumshusha chini.”
37 And then, after Jesus shouted loudly, he stopped breathing [and died].
Kisha Yesu akalia kwa sauti kubwa na akafa.
38 [At that moment] the [heavy thick] curtain that closed off [the most holy place in] the Temple split into two pieces from top to bottom. [That showed that ordinary people could now go into the presence of God].
Pazia la hekalu likagawanyika vipande viwili toka juu mpaka chini.
39 The officer who supervised the soldiers [who nailed Jesus to the cross] was standing in front of Jesus. When he saw how Jesus died, he exclaimed, “Truly, this man was the man who was also God!”
Ofisa mmoja aliyekuwa amesimama akimwelekea Yesu, alipoona amekufa kwa jinsi ile, akasema, “Kweli huyu mtu alikuwa Mwana wa Mungu.”
40 There were also some women there, watching these events from a distance. They had accompanied Jesus when he was in Galilee [district], and they had provided what he needed. They had come with him to Jerusalem. Among those women was Mary from Magdala [town]. There was [another] Mary, who was the mother of the younger James and of Joses. There was also Salome.
Walikuwepo pia wanawake waliokuwa wakitazama kwa mbali. Miongoni mwao alikuwepo Mariamu Magdalena, Mariamu (mama yake Yakobo mdogo wa Yose), na Salome.
Wakati alipokuwa Galilaya walimfuata na kumtumikia. Na wanawake wengine wengi pia waliambatana naye hadi Yerusalemu.
42 When evening was near, [a man named] Joseph from Arimathea [town came there]. He was a member of the [Jewish] council, one whom everyone respected. He was also one of those who had been waiting expectantly for the [time when] God [would send] his king to begin to rule. [He knew that, according to Jewish law, people’s bodies had to be buried] {[someone had to bury people’s bodies]} [on the day they died. He also realized that] it was the day when [people] prepared [things for] ([the Jewish day of rest/the Sabbath]), [and that the Sabbath would start when the sun set]. So he became courageous and went to Pilate and asked Pilate [to permit him to take] the body of Jesus [down from the cross and bury it immediately].
Kulipokuwa jioni, na kwa kuwa ilikuwa siku ya maandalio, siku kabla ya Sabato,
Yusufu wa Arimathaya alikuja pale. Alikuwa ni mjumbe wa Baraza anayeheshimiwa mtu anayeutarajia Ufalme wa Mungu. Kwa ujasiri akaenda kwa Pilato, na kuuomba mwili wa Yesu.
44 Pilate was surprised [when he heard that] Jesus was already dead. So he summoned the officer who was in charge of the soldiers [who crucified Jesus], and he asked him if [Jesus] had already died.
Pilato akashangazwa kwamba Yesu tayari amekufa; akamwita yule afisa akamwuliza kama Yesu amekufa.
45 When the officer told [Pilate that Jesus was dead], Pilate allowed Joseph [to take away] the body.
Alipopata uhakika kwa afisa kwamba amekufa, alimruhusu Yusufu kuuchukua mwili.
46 After Joseph bought a linen cloth, he [and others] took [Jesus’ body down from the cross]. They wrapped it in the linen cloth and laid it in a tomb that [previously] had been dug out of the rock [cliff]. Then they rolled a [huge flat] stone in front of the entrance to the tomb.
Yusufu alikuwa amenunua sanda. Akamshusha toka msalabani, akamfunga kwa sanda, na kumweka ndani ya kaburi lililochimbwa katika mwamba. Kisha akalivingirisha jiwe mlangoni mwa kaburi.
47 Mary [from] Magdala and Mary the mother of Joses were watching where Jesus’ [body] was placed {where they placed Jesus’ [body]}.
Mariamu Magdalena na Mariamu mama yake Yose waliona sehemu alipozikwa Yesu.

< Mark 15 >