< Luke 19 >

1 Jesus and his disciples entered Jericho and were going through the [city].
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 There was a man [there] named Zacchaeus. He was a chief tax collector, who was rich.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 He tried to see Jesus, but he was very short, and there was a big crowd of people [near Jesus]. So he was not able to see him.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 So he ran further ahead [along the road] that Jesus was walking on. He climbed a sycamore-fig tree to see Jesus.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 When Jesus got there, he looked up and said to him, “Zacchaeus, come down quickly, because [God wants] me to go [with you(sg)] to your house and stay there [tonight]”!
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 So he came down quickly. [He took Jesus to his house] and welcomed him joyfully.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 The people [who saw Jesus go there] grumbled saying, “He has gone to be the guest of a man who is a sinner!”
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Then Zacchaeus stood up [while they were eating] and said to the Lord [Jesus], “Lord, I want you [(sg)] to know that I am going to give half of what I own to poor people. And as for the people whom I have cheated, I will pay them back four times the amount [I have gotten from them by cheating].”
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Jesus said to him, “Today [God] has forgiven [PRS] [you and the other people in] [MTY] this house, because you [(sg)] also [have shown that you have trusted in God as] your ancestor Abraham [did].
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 Remember this: [I], the one who came from heaven, came to seek and save [people like you(sg)] who have [gone astray from God, just like a shepherd who searches for his] lost [sheep].”
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 They were coming near to Jerusalem, and the people who were [going with Jesus] who heard him say these things thought that as soon as [he got to Jerusalem] he would become their king.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 [So] he told them this parable: “A prince prepared to go to a distant country in order that [the Emperor] would make him a king. [He intended] to return later.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 [Before he left], he summoned ten of his servants. He gave each of them a coin worth three months’ wages. He said to them, ‘Do business with these coins until I return!’ [Then he left].
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 But [many of] his fellow-citizens hated him. So after he left they sent some messengers to tell [the Emperor], ‘We [(exc)] do not want this man to be our king!’
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 But [the Emperor] made him king anyway. [Later] the [new king] returned. Then he commanded that the servants to whom he had given the coins should be summoned {that someone should summon the servants to whom he had given the coins}. He wanted to know how much they had gained by doing business with the coins.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 The first man came [to him] and said, ‘Sir, with your one coin [I] have earned ten more [coins]!’
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 He said to this man, ‘[You are a] good servant! [You have] done [very] well! Because you have [handled] faithfully a small amount [of money, I will give you] authority [to rule] ten cities.’
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 Then the second servant came and said, ‘Sir, with your one coin [I] have earned five more [coins]!’
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 He said to that servant similarly, ‘[Good! I will give you authority to rule] five cities.’
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 Then another servant came. He said, ‘Sir, here is your coin. I wrapped it in a napkin and put it away, [so that nothing would happen to it].
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 I did that [because] I was afraid [of what you would do to me if the business failed. I know] you are a man who does not do foolish things with your money. You [even] take [from others money] that does not really belong to you, [like a farmer who] harvests grain [from another man’s field] where he did not [even] do the planting.’
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 The king said to that servant, ‘You wicked servant! I will condemn you by the very words [MTY] that you [have just now spoken]. (You know that I do not [do foolish things with my money]./Did you not know that I do not [do foolish things with my money]?) [RHQ] [You said] that I [even] take [from others money] that does not really [belong to me], [like a farmer who] harvests grain [from another man’s field] where he did not [even] do the planting.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 So (you should at least have given my money to money lenders!/why did you not [at least] give my money to bankers?) [RHQ] Then [when I returned] I could have collected that amount plus the interest [it would have earned]!’
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 Then [the king] said to those who were standing near, ‘Take the coin from him and give it to [the servant] who has ten coins!’
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 They protested, ‘But Sir, he already has ten [coins]!’
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 [But the king said], ‘I tell you this: To the people who [use well what] they have [received], more will be given {[I] will give more}. But from the people who [do] not [use well what they have received], even what they [already] have will be taken away {[I] will take away even what they already have}.
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Now, [as for] those enemies of mine who did not want me to rule over them, bring them here and execute them while I am watching!’”
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 After [Jesus] said those things, he [continued on the road] up to Jerusalem, going ahead of his disciples.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 When they got near Bethphage and Bethany [villages], near the hill that is called {that they call} Olive [Tree] Hill,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 he said to two of [his] disciples, “Go to the village just ahead [of you]. As you [two] enter [it], you will see a young animal that no one has ever ridden, that has been {someone has} tied up. Untie it and bring it [to me].
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 If anyone asks you, ‘Why are you untying it?’ say [to him], ‘The Lord needs it.’”
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 [So] the [two disciples] went [to the village] and found the [animal], just like he had told them.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 As they were untying it, its owners said to them, “Why are you two untying that young animal?”
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 They replied, “The Lord needs it.” [So the owners said that they could take it].
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 The [two disciples] brought [the animal] to Jesus. They threw their cloaks on the animal’s back [for him to sit on] and helped Jesus get on it.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 Then as he rode along, [others] spread their cloaks on the road [to honor him].
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 As they came near [to Jerusalem], on the road that descends from Olive [Tree] Hill, the whole crowd of his disciples began to rejoice and praise God loudly for all the great miracles that they had seen [Jesus do].
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 They were saying things like, “May the Lord [God] bless our king who comes representing [MTY] him!” “May there be peace [between God] in heaven [and us his people]!” “May [everyone] praise God!”
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Some of the Pharisees who were in the crowd said to Jesus, “Teacher, rebuke your disciples [for saying things like that]!”
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 He replied, “I tell you this: If these people would be silent, the stones themselves would shout [to praise me]!”
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 When [Jesus] came near [to] Jerusalem and saw the city, he cried about [its people].
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 He said, “[My disciples know what they need to do] to have peace [with God]; I wish that even today [the rest of] you people knew it. But now you are unable to know [MTY] it.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 I want you to know this: Soon [your enemies] will come and will set up a barricade around your [city]. They will surround [the city] and attack [it] on all sides.
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 They will [break through] the walls [and] destroy everything. They will smash you and your people/children. [When they finish destroying everything], there will not be one stone left on top of another. [All this will happen] because you did not recognize the time when God sent his [Messiah] to [save] you!”
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 [Jesus entered Jerusalem and] went into the Temple [courtyard]. He saw the people who were selling [things there],
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 and he began to chase them out. He said to them, “It has been written {[A prophet] wrote} [in the Scriptures that God said], ‘[I want] my house to be a place where people pray’; but you bandits have made it a cave where you can [hide]!”
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 Each day [during that week Jesus] was teaching people in the Temple [courtyard]. The chief priests and the men who taught the [Jewish] laws and [other Jewish] leaders tried to find a way to kill him.
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 But they did not find any way to do it, because all the people there listened eagerly to him [and would have resisted them if they had tried to hurt him].
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luke 19 >