< Luke 18 >

1 [Jesus] told [his disciples] a parable to teach them that they always ought to pray confidently and not be discouraged [if God does not immediately answer their prayers].
Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2 He said, “In a certain city there was a judge who did not revere God, and did not care about people, either.
Alisema: “Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3 There was a widow in that city who kept coming to him, saying, ‘Please decide what is just [in the dispute between me and] the man who is opposing me [in court!’]
Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4 For a long time the judge refused [to help her]. But later he thought to himself, ‘I do not revere God and I do not care about people,
Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5 but this widow keeps bothering me! So I will make sure that she is treated justly. [If I do not do that], she will exhaust me by continually coming to me!’”
lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!”
6 Then the Lord [Jesus] said, “[Even though] the judge was not a righteous man, think carefully about what he said!
Basi, Bwana akaendelea kusema, “Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7 [Similarly], (God will certainly show that [what you] have done has been right!/will God not show that [what you] have done has been right?) [RHQ] He will do this for you whom he has chosen. [He will do this for you] who pray earnestly to him night and day, asking him to [help you]. He may delay [helping you].
Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8 But I tell you, [some day] he will show that what you did was right, and he will do it quickly. But when [I], the one who came from heaven, return to earth, (there may not be [many people who will still] be trusting [that I will vindicate them] (OR, who will still be trusting in me)./will there be [many people who will still] be trusting [that I will vindicate them] (OR, who will still be trusting in me)?) [RHQ]”
Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?”
9 [Jesus] also told a parable [to warn] people who mistakenly thought that they were doing things that made them acceptable to God. Besides, they also despised other people.
Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10 [He said this]: “Two men went up to the Temple [in Jerusalem] to pray. One was a Pharisee. The other was a tax collector.
“Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11 The Pharisee stood and prayed silently, ‘God, I thank you that I am not like other men. [Some] extort money [from others]; some treat others unjustly; some commit adultery. [I do not do such things. And I am certainly not] like this tax collector [who cheats people]!
Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12 [Our law says that we(exc) should] (fast/abstain from food) [once a week], [but I do more than that. I] fast twice a week! I give [you] ten percent of all that I earn!’
Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13 But the tax collector stood far [from the other people in the Temple courtyard because he felt very unworthy]. He would not even look up toward heaven. Instead, he beat on his chest [to show that he was sorry for his sin]. He said, ‘God, I am a sinner; be merciful to me [and forgive me]!’”
Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14 [Then Jesus said], “I tell you [(pl)] that as the tax collector went home, the record of his sins was erased {[God] erased the record of his sins}, not that of the Pharisee. [Remember this]: Those who exalt themselves will be humbled {[God] will humble all those who exalt themselves}, but those who humble themselves will be exalted {[he] will exalt those who humble themselves}.”
Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa.”
15 [One day when many people were coming to Jesus], they were also bringing small children. They wanted him to put his hands on [the children and bless them]. When the disciples saw that, they rebuked [those who were bringing those children].
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16 But Jesus called the children [to come to him]. He said to his disciples, “Let the children come to me! Do not stop them! It is people who are [humble and trusting] like they are who can experience God ruling [their lives].
Lakini Yesu akawaita kwake akisema: “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17 Note this: Those who do not [trust God and] allow him to direct [their lives], as children [do], will not enter the [MET] place where God rules.”
Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo.”
18 A [Jewish] leader asked [Jesus], “Good teacher, what shall I do in order to have eternal life?” (aiōnios g166)
Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?” (aiōnios g166)
19 Jesus said to him, “Only God is good! No one [else] is good! (So you(sg) should consider carefully what [you are implying by] calling me good!/[Do you realize that you are implying that I am God by] calling me good?) [RHQ]
Yesu akamwambia, “Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20 [But to answer your question], you [(sg)] know the commandments that [God gave Moses. He commanded such things as] ‘do not commit adultery, do not commit murder, do not steal, do not testify falsely [about what you have seen or heard], honor your father and mother.’”
Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako.”
21 The man said, “I have obeyed all those [commandments] ever since I was young. [So] ([there must be something else I have not done./is that enough]?)”
Yeye akasema, “Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu.”
22 When Jesus heard [him say] that, he replied to him, “There is one thing that you [(sg)] have not [done] yet. Sell all that you own. Then give [the money] to poor people. [The result will be that] you will have [spiritual] riches in heaven. Then come and be my disciple!”
Yesu aliposikia hayo akamwambia, “Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate.”
23 The man became sad when he heard that, because he was very rich [and he did not want to give everything away].
Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24 Jesus looked at the man [as he left], and said, “It is very difficult for those who are wealthy [to decide] to let God rule [MET] their [lives].
Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, “Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25 [You would say] that it is impossible for a camel to go through the eye of a needle. It is [almost] as difficult [HYP] for rich people [to decide] to let God rule their [lives].”
Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 [The Jews thought that God favored rich people, so they thought that if God did not save rich people, he would not save others, either]. So [one of the disciples] who heard him say that replied, “If that is so, it seems that no one will be saved {[that God] will not save anyone} [RHQ]!”
Wale watu waliposikia hayo, wakasema, “Nani basi, atakayeokolewa?”
27 But Jesus said, “It is impossible for people [to save themselves]. But [God can save them, because] God can do anything!”
Yesu akajibu, “Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu.”
28 Then Peter said, “[You know that we(exc) have left] everything we had and have become your disciples [RHQ]. [So what about us?] (OR, [So will God accept/save us?]”)
Naye Petro akamwuliza, “Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!”
29 He said to them, “Keep this in mind: Those who have left [their] homes, [their] wives, [their] brothers, [their] parents, [their] children, [or any other family members], [to tell others] about how God wants to rule [MET] [people’s lives],
Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30 will receive in this life many times as much [as they left]. And in the future age they will (live eternally [with God]/ have eternal life).” (aiōn g165, aiōnios g166)
atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao.” (aiōn g165, aiōnios g166)
31 [Jesus] took the twelve [disciples] to a place by themselves and said to them, “Listen carefully! We [(inc)] are [now] going up to Jerusalem. [While we are there], everything that has been written by the prophets {that the prophets have written} about [me], the one who came from heaven, will be fulfilled {will occur}.
Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, “Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32 I will be put into the hands of {[My enemies] will hand me over to} non-Jews. [The non-Jews] will make fun of me and mistreat me and spit on me.
Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33 They will whip me, and [then] they will kill me. But on the third day [after that] I will become alive again.”
Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka.”
34 But [the disciples] did not understand any of those things that [he said]. They were prevented {[Something] prevented them} from understanding the meaning of what [he] was telling [them].
Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35 As [Jesus and his disciples] came near to Jericho [city], a blind man was sitting beside the road. [He was] begging [for money].
Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36 When he heard the crowd [of people] passing by, he asked someone, “What is happening?”
Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, “Kuna nini?”
37 They told him, “Jesus, [the man] from Nazareth [town], is passing by.”
Wakamwambia, “Yesu wa Nazareti anapita.”
38 He shouted, “Jesus, [you who are] descended from [King] David, [the Messiah], pity me!”
Naye akapaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
39 Those who were [walking] at the front [of the crowd] scolded the man [and] told him to be quiet. But he shouted more loudly, “You who are descended from [King] David, [the Messiah], pity me!”
Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: “Mwana wa Daudi, nihurumie;”
40 Jesus stopped and told [people] to bring the man to him. When [the blind man] came near, Jesus asked him,
Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41 “What do you [(sg)] want me to do for you?” He replied, “Lord, enable me to see [again]!”
“Unataka nikufanyie nini?” Naye akamjibu, “Bwana, naomba nipate kuona tena.”
42 Jesus said to him, “[Then] see! Because you have trusted [PRS] [in me], [I] have healed you!”
Yesu akamwambia, “Ona! Imani yako imekuponya.”
43 Immediately he was able to see! And he went with [Jesus], praising God. And when all the people who were [going with Jesus] saw it, they also praised God.
Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.

< Luke 18 >