< Judges 2 >

1 Yahweh [appeared in the form of] an angel [and] went up from Gilgal to [a place that was later called] Bokim. He said [to the Israeli people], “I brought your [ancestors] up here from Egypt. I led them into this land that I solemnly promised to give to your ancestors. I said to them, ‘The agreement that I made with you, as for me, I will never (break it/say that it is ended).
Malaika wa Bwana akakwea kutoka Gilgali hadi Bokimu, naye akasema, “Niliwapandisha kutoka Misri na kuwaingiza katika nchi niliyoapa kuwapa baba zenu. Nikasema, ‘Kamwe sitalivunja Agano langu nanyi.
2 But as for you, you must never make a peace agreement with the people who live in this land. You must tear down the altars [where they make sacrifices to idols].’ But you have not obeyed me.
Nanyi msifanye agano na watu wa nchi hii, bali mtazibomoa madhabahu yao.’ Lakini ninyi hamkunitii mimi. Kwa nini mmefanya jambo hili?
3 So now, I am telling you that I will not expel [your enemies] as you advance. They will be like thorns in your sides. And [they] will try to trap you [by making you worship] their idols.”
Sasa basi ninawaambia kuwa sitawafukuza watoke katikati yenu ila watakuwa miiba kwenu, nao miungu yao itakuwa tanzi kwenu.”
4 After he told that to all the Israelis, the people cried loudly.
Malaika wa Bwana alipomaliza kusema mambo haya kwa Waisraeli wote, watu wakalia kwa sauti kuu.
5 They called that place Bokim, [which means ‘weeping’]. There they offered sacrifices to Yahweh.
Wakapaita mahali pale Bokimu. Nao wakamtolea Bwana sadaka.
6 After Joshua sent the Israeli people away, each group went to possess the land that had been allotted to them.
Baada ya Yoshua kuwapa watu ruhusa waende zao, Waisraeli wakaenda kwenye urithi wao wenyewe ili kumiliki nchi yao.
7 They served Yahweh as long as Joshua was alive, and as long as the elders, those who had seen all the great things that Yahweh had done for Israel, were alive.
Watu wakamtumikia Bwana siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, waliokuwa wameona mambo makuu ambayo Bwana alikuwa ametenda kwa ajili ya Israeli.
8 Then Yahweh’s servant Joshua died. He was 110 years old when he died.
Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Bwana, akafa akiwa na umri wa miaka 110.
9 They buried his body in the area he had received [from Moses], at Timnath-Serah, in the area where the descendants of Ephraim lived, north of Gaash Mountain.
Wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Heresi katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini ya Mlima Gaashi.
10 After all the people died who lived at the same time as Joshua [EUP], a group of people grew up who did not know Yahweh, and did not know what great things he had done for the Israeli people.
Baada ya kizazi kile chote kukusanywa pamoja na baba zao, kikainuka kizazi kingine baada yao ambacho hakikumjua Bwana, wala matendo yale aliyokuwa ametenda kwa ajili ya Waisraeli.
11 They did things that Yahweh said were very evil. They worshiped [idols that represented the god] Baal and the goddess Astarte. They worshiped [DOU] the various gods that the people-groups around them worshiped. They stopped worshiping Yahweh, the God their ancestors worshiped, the one who had brought their ancestors out of Egypt. That caused Yahweh to be very angry.
Kwa hiyo Waisraeli wakatenda maovu machoni pa Bwana na kuwatumikia Mabaali.
Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri. Wakaifuata na kuiabudu miungu mbalimbali ya mataifa yanayowazunguka. Wakamkasirisha Bwana,
kwa sababu walimwacha na kutumikia Baali na Maashtorethi.
14 So he allowed people from other groups to raid them and steal their crops and animals. They were no longer able to resist their enemies, and Yahweh allowed all their enemies around them to defeat them.
Hivyo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia mikononi mwa wavamizi waliowateka nyara. Akawauza katika mikono ya adui zao pande zote, hivyo hawakuweza tena kuwazuia adui zao.
15 Whenever the Israelis went to fight [their enemies], Yahweh [MTY] was opposing them, and allowed their enemies to defeat them, just as he had promised he would do. So the Israelis were greatly distressed.
Popote Israeli walipotoka kwenda kupigana, mkono wa Bwana ulikuwa kinyume nao ili kuwashinda, kama vile alivyokuwa amewaapia. Nao wakawa katika taabu kubwa.
16 Then Yahweh gave leaders to them. These leaders rescued the Israelis from the people who were raiding them.
Ndipo Bwana akawainua waamuzi, ambao waliwaokoa katika mikono ya hao watu waliowashambulia.
17 But the Israelis still would not pay attention to their leaders. Instead, they went to the idols, [acting like] prostitutes [who gave themselves to men who were not their husbands] [MET], and they worshiped those idols. They were not like their ancestors. Their ancestors obeyed what Yahweh commanded, but their descendants quickly stopped behaving as their ancestors had behaved.
Lakini hawakuwasikiliza hata waamuzi wao, bali walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine na kuiabudu. Waligeuka mara na kuiacha njia ambayo baba zao waliiendea, yaani, njia ya kutii amri za Bwana.
18 Whenever Yahweh gave a leader to them, he helped that leader and enabled him to rescue the people from their enemies. He helped them like that as long as that leader was alive. Yahweh pitied them as they groaned because they were being oppressed and caused to suffer.
Kila mara Bwana alipowainulia mwamuzi, Bwana alikuwa pamoja na huyo mwamuzi, naye aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui zao kwa kipindi chote alichoishi yule mwamuzi. Kwa kuwa Bwana aliwahurumia kwa sababu ya kilio chao cha huzuni kwa ajili ya wale waliokuwa wakiwatesa na kuwataabisha.
19 But after that leader died, the people went back to behaving in ways even more evil than their ancestors had behaved. They worshiped other gods and bowed down to them and did all [LIT] the things that they thought those gods wanted them to do.
Lakini kila mara mwamuzi alipofariki, watu walirudia katika hali mbaya ya uovu zaidi kuliko baba zao, wakiifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu. Walikataa kuacha matendo yao maovu na njia zao za ukaidi.
20 So Yahweh was very angry with the Israeli people. He said, “These people have disobeyed the agreement I made with their ancestors. They have not done what I told them to do.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia sana Israeli na kusema, “Kwa kuwa taifa hili limevunja Agano lile nililofanya na baba zao na hawakunisikiliza,
21 So I will no longer expel the people-groups that Joshua left in this land when he died.
mimi nami sitafukuza taifa lolote ambalo Yoshua aliliacha alipofariki.
22 I will use them to test the Israeli people to see whether they will do what I want them to do, as their ancestors did.”
Nitayatumia ili nipate kuwapima Israeli na kuona kama wataishika njia ya Bwana na kuenenda katika hiyo kama njia baba zao walivyofanya.”
23 Yahweh had allowed those people-groups to stay in that land. He did not expel them by allowing Joshua [and his men] to defeat them.
Bwana alikuwa ameyaacha hayo mataifa yabaki; hakuyaondoa mara moja kwa kuyatia mikononi mwa Yoshua.

< Judges 2 >