< Judges 18 >

1 At that time the Israelis had no king. Also at that time, the tribe of Dan was still searching for some land where they could live. The other Israeli tribes had [been able to] ([capture/take possession of]) [the] land that had been allotted to them, but the tribe of Dan had not been able to do that.
Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme. Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli.
2 So they chose five soldiers from their clans, men who lived in Zorah and Eshtaol [cities], to go through the land and explore it [and try to find some land where their tribe could live]. They came to Micah’s house in the hilly area where the tribe of Ephraim lived, and they stayed there that night.
Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.” Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo.
3 While they were in his house and they heard the young man who had become Micah’s priest talking, they recognized from (his accent/the way that he talked) [that he was from the southern part of Israel]. So they went to him and asked him, “Who brought you here? What are you doing here? Why did you come here?”
Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”
4 He told them the things that Micah had done for him. And he said, “Micah (has hired me/is paying me to work for him), and I have become his priest.”
Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”
5 So they said to him, “Please ask God if we will succeed [in what we are trying to do] on this journey.”
Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”
6 The young man replied, “Things will go well for you. Yahweh will go with you on this journey.”
Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”
7 [The next day] the five men left. When they came to Laish [city], they saw that the people there lived safely, like the people in Sidon [city] did. The people there thought that they were safe/protected [from any enemies], and they had plenty of [good fertile] land. They lived very far from the people of Sidon, [so the people of Sidon would not be able to help defend/protect them]. They had no other (allies/groups nearby that would help them in battles).
Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.
8 When those five men returned to Zorah and Eshtaol, their relatives asked them “What did you find out?”
Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”
9 They replied, “We have found some land, and it is very good. We should go and attack the people [who live there]. Why are you staying here and doing nothing [RHQ]? Do not wait any longer! We should go immediately and take possession of that land!
Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki.
10 When you go there, you will see that there is plenty of land, and it has everything [that we will need]. The people there are not expecting anyone to attack them. Surely God is giving that land to us.”
Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”
11 So 600 men from the tribe of Dan left Zorah and Eshtaol, carrying their weapons.
Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli.
12 On their way they set up their tents near Kiriath-Jearim [city] in [the area where the tribe of] Judah [lives]. That is why the area west of Kiriath-Jearim was named ‘Camp of Dan’, and that is still its name.
Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani mpaka leo.
13 From there, they went to the hilly area where the tribe of Ephraim lives. And they arrived at Micah’s house.
Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.
14 The five men who had explored the land near Laish said to their fellow Israelis, “Do you know that in one of these houses there is a sacred vest, several idols, and a statue? [We think that] you know what you should do.” [RHQ]
Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.”
15 So they went to the house where the man from the tribe of Levi lived, which was the house where Micah lived, and they greeted the young man from the tribe of Levi [who had become Micah’s priest].
Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu.
16 The 600 men of the tribe of Dan stood outside the gate of the house, carrying their weapons.
Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango.
17 The five men who had explored the land went into Micah’s house, and took all the idols, the sacred vest, and the statue. While they did that, the 600 men stood outside the gate, [talking] with the priest.
Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.
18 When the priest saw them bringing out the idols and the sacred vest and the statue, he said to them, “What are you doing?”
Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”
19 They replied, “Be quiet! Do not say anything! You come with us and be [like] a father to us and a priest for us. Is it better for you to [stay here and] be a priest for the people in the house of one man, or to be a priest for a clan, and a priest for a whole tribe of Israelis?” [RHQ]
Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?”
20 The priest liked what they were suggesting. So he took the sacred vest and the idols, and he [prepared to] go with the men from the tribe of Dan.
Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu.
21 They all put their little children and their animals and everything else that they owned in front of them.
Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.
22 After they had gone a little distance from Micah’s house, Micah [saw what was happening. He] quickly summoned the men who lived near him, and they ran and caught up with the men from the tribe of Dan.
Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani.
23 They shouted at them. The men of the tribe of Dan turned around and said to Micah, “What is the problem? Why have you gathered these men [to pursue us]?”
Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”
24 Micah shouted, “You took the silver idols that were made for me! You also took my priest! I do not have anything left [RHQ]! So why do you ask me, ‘What is the problem?’”
Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’”
25 The men from the tribe of Dan replied, “You should not shout loudly like that! One of our angry men might attack you and kill you and your family!”
Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.”
26 Then the men from the tribe of Dan continued walking. Micah realized that there was a very large group of them, [so that it would be useless for him to try to fight them]. So he turned around and went home.
Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.
27 The men of the tribe of Dan were carrying the things that had been made for Micah, and they also took his priest, and they continued traveling to Laish. They attacked the people who were peacefully living there, and killed them with their swords, and then they burned everything in the city.
Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto.
28 Laish was far from [the city of] Sidon, [so the people of Sidon could not rescue the people of Laish]. And the people of Laish had no other allies. Laish was in a valley near Beth-Rehob [town]. The people of the tribe of Dan rebuilt the city and started to live there.
Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu. Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo.
29 They gave to the city a [new] name, Dan, in honor of their ancestor Dan, who was one of the sons of Jacob.
Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza.
30 The people of the tribe of Dan set up [in the city] the idols [that had been made for Micah]. Jonathan, who was the son of Gershom and the grandson of Moses, was appointed to be their priest. His descendants continued to be priests until the Israelis were captured and taken [to Assyria].
Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa.
31 After the people of the tribe of Dan set up the idols that had been made for Micah, [they worshiped those idols, even though] the Sacred Tent [where they had been commanded to worship] God, was at Shiloh.
Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.

< Judges 18 >