< Joshua 1 >

1 After Moses, who served Yahweh [well], died, Yahweh said to Nun’s son Joshua, who had been Moses’ assistant,
Baada ya kifo cha Mose mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Mose:
2 “[You know that] my servant Moses is [now] dead. So now get ready to lead all these [Israeli] people across the Jordan [River]. Enter the land that I will soon give to you.
“Mtumishi wangu Mose amekufa. Sasa basi, wewe pamoja na watu wote hawa, jiandaeni kuvuka huu Mto Yordani kuingia nchi ambayo karibu nitawapa wana wa Israeli.
3 I will give to you all the land that you walk on, as I promised Moses.
Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga nimewapa, kama vile nilivyomwahidi Mose.
4 That land will extend from the desert [in the south], to the Lebanon [Mountains in the northwest], and to the big Euphrates River [in the northeast], and to the Mediterranean Sea on the west. [It will include] all the land where the descendants of Heth [live].
Nchi yenu itaenea kuanzia jangwa hili hadi Lebanoni, tena kuanzia mto mkubwa wa Frati, yaani nchi yote ya Wahiti, hadi Bahari ile Kubwa iliyoko upande wa magharibi.
5 No group will be able to oppose [and defeat] you during your life. I will help you as I helped Moses. I will always be with [LIT] you; I will never forsake you.
Hakuna mtu yeyote atakayeweza kushindana na wewe siku zote za maisha yako. Kama vile nilivyokuwa pamoja na Mose, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakuacha wala sitakupungukia.
6 “Be strong and courageous, because you are the one who will lead these Israeli people [and enable them] to possess the land that I solemnly promised to their ancestors that I would give them.
“Uwe hodari na shujaa, kwa sababu wewe ndiwe utakayewaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia baba zao kuwapa.
7 Just be strong and very courageous. Be sure to obey all the laws that my servant Moses gave to you. In order that you may be successful wherever you go, do not stop obeying any of them [IDM].
Uwe hodari na uwe na ushujaa mwingi. Uwe na bidii kutii sheria yote aliyokupa Mose mtumishi wangu, usiiache kwa kugeuka kuelekea kuume au kushoto, ili upate kufanikiwa popote uendako.
8 Make sure to habitually read [to the people some of] the laws [that God gave Moses]. Meditate on those laws [every] day and [every] night. And be sure to obey all those laws. If you do that, you will be successful in everything that you do [DOU].
Usiache Kitabu hiki cha Sheria kiondoke kinywani mwako; yatafakari maneno yake usiku na mchana, ili upate kuwa mwangalifu kufanya kila kitu sawasawa na yote yaliyoandikwa ndani yake. Ndipo utakapofanikiwa na kisha utastawi.
9 Do not forget [RHQ] that I have commanded you to be strong and courageous. Do not be afraid, and do not be discouraged, because I, Yahweh, your God, will (be with/help) you wherever you go.”
Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakuwa pamoja nawe kokote uendako.”
10 Then Joshua commanded the leaders of the people of Israel,
Ndipo Yoshua akawaagiza maafisa wa watu akisema,
11 “Go throughout the camp and tell the people this: ‘Prepare all the food that you will take with you, because the day after tomorrow you will cross this Jordan [River], in order to possess the land that Yahweh, our God, is about to give you.’”
“Pitieni katika kambi yote mkawaambie watu, ‘Wekeni tayari mahitaji yenu. Siku tatu kuanzia sasa mtavuka hii Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa iwe yenu wenyewe.’”
12 But to the [clans that were] descendants of Reuben and Gad, and to the half clan [that were descendants] of Manasseh, Joshua said,
Lakini kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, Yoshua akasema,
13 “Do not forget what Moses, the servant of Yahweh, commanded you: ‘Yahweh, your God, has given you this land in order that you can [live here] safely/peacefully.’
“Kumbukeni agizo lile Mose mtumishi wa Bwana alilowapa: ‘Bwana Mungu wenu anawapa ninyi raha, naye amewapa nchi hii.’
14 Your wives and your children and your livestock may stay [here] in this land on the east side of the Jordan [River], but all your soldiers must cross [the river], ahead of the people of the other tribes. They must take all their weapons with them. You must continue to help your fellow Israelis
Wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu watakaa katika nchi ile Mose aliyowapa mashariki ya Yordani, lakini mashujaa wenu wote, wakiwa wamevikwa silaha kikamilifu lazima wavuke mbele ya ndugu zenu. Imewapasa kuwasaidia ndugu zenu hadi
15 until they are able to live there safely/peacefully, as Yahweh has enabled you to do. You must help them until after they have conquered all the people in the land that Yahweh, your God, is giving them. After that, your soldiers may return to live in this land that Moses gave to you here on the east side of the Jordan [River].”
Bwana awape nao raha, kama alivyokwisha kufanya kwa ajili yenu hadi wao pia watakapokuwa wamemiliki nchi ile Bwana Mungu wenu anayowapa. Baada ya hilo, mwaweza kurudi na kukalia nchi yenu wenyewe, ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwapa mashariki mwa Yordani kuelekea linakochomoza jua.”
16 The people answered Joshua, “We will do everything that you have commanded us to do, and we will go wherever you tell us to go.
Ndipo wakamjibu Yoshua, “Chochote ambacho umetuagiza tutafanya na popote utakapotutuma tutakwenda.
17 As we obeyed all that Moses told us to do, we will obey all that you tell us to do. We pray that Yahweh will (be with/help) you as he (was with/helped) Moses.
Kama vile tulivyomtii Mose kikamilifu, ndivyo tutakavyokutii wewe. Bwana Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama vile alivyokuwa pamoja na Mose.
18 Anyone who (rejects what you say/opposes you) and does not obey what you command [DOU], we will execute. But we want you to be strong and courageous!”
Yeyote atakayeasi neno lako na kuacha kuyatii maneno yako, au chochote utakachowaamuru, atauawa. Uwe imara na hodari tu!”

< Joshua 1 >