< Joshua 21 >

1 While Eleazar the Supreme Priest and Joshua and the leaders of all the Israeli tribes were at Shiloh, the leaders of the clans of the tribe of Levi went to them and said, “Yahweh commanded Moses that you should give us towns where we can have pasture/fields/grassland for our animals, [but you have not done these things yet].”
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 So the Israeli leaders obeyed this command from Yahweh. They agreed to give towns and pasturelands to the tribe of Levi.
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 [First] they allotted some cities to the Kohath clans, who belonged to the tribe of Levi. To those who were descendants of the first Supreme Priest Aaron, they allotted 13 towns in the areas that had been allotted to the tribes of Judah, Simeon, and Benjamin.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 To the other members of the Kohath clan they allotted ten cities in the areas that had been allotted to the tribes of Ephraim, Dan, and the part of the tribe of Manasseh [that lives on the west side of the Jordan River].
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 The people from the Gershon clans were allotted 13 cities in the areas that had been allotted to the tribes of Issachar, Asher, Naphtali, and the part of the tribe of Manasseh that lives on the east side of the Jordan [River].
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 The people from the Merari clans were allotted twelve cities in the areas that had been allotted to the tribes of Reuben, Gad, and Zebulun.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 So the Israeli leaders gave cities and pastureland to the tribe of Levi, just as Yahweh had commanded Moses that they should do.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 These are the names of the cities and surrounding pasturelands that were allotted to them, that were in the areas where the tribes of Judah and Simeon lived.
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 First, they allotted cities to the members of the Kohath clans.
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 They allotted to them Kiriath-Arba (which is [now named] Hebron), in the hilly area of Judah. Arba received its name because Arba was the ancestor of [the giants of] the Anak people-group.
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 But the fields and villages surrounding Arba had already been allotted to Caleb.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 They allotted to them Hebron, which was one of the cities to which people could run/escape to be safe/protected. They also allotted to the Kohath clan the cities of Libnah,
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 Jattir, Eshtemoa,
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 Holon, Debir,
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 Ain, Juttah, and Beth-Shemesh. Altogether they were allotted those nine cities which were located in the areas that had been allotted to the tribes of Judah and Simeon.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 The Kohath clan was also allotted these four cities: Gibeon, Geba,
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Anathoth, and Almon. Those cities were in the area that had been allotted to the tribe of Benjamin.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Altogether those 13 towns and surrounding pastureland were allotted to the priests who were descended from Aaron.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 The other members the Kohath clan were allotted four cities and the surrounding pastureland in the area that had been allotted to the tribe of Ephraim.
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 Those cities were Shechem (which was one of the cities to which people could run/escape to be safe/protected), Gezer,
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 Kibzaim, and Beth-Horon.
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 They were also allotted four cities and surrounding pastureland in the area that had been allotted to the tribe of Dan. Those cities were Eltekeh, Gibbethon,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Aijalon, and Gath-Rimmon.
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 They were also allotted two towns and surrounding pastureland that had been allotted to [the] part of the tribe of Manasseh [that lived on the west side of the Jordan River]. Those cities were Taanach and Gath-Rimmon.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 Those were the ten cities and surrounding pastureland that were allotted to the other members of the Kohath clan.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 They also allotted towns and the surrounding pastureland to the Gershon clans. Those clans were also descended from Levi. They were allotted two cities from the area that had been allotted to the tribe of Manasseh [that is on the east side of the Jordan River]. Those cities were Golan in the Bashan region, which was one of the cities to which people could run/escape to be safe/protected, and Be-Eshtarah.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 From the area that had been allotted to the tribe of Issachar they were allotted four cities. Those cities were Kishion, Daberath,
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Jarmuth, and En-Gannim.
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 From the area that had been allotted to the tribe of Asher they were allotted four cities. Those cities were Mishal, Abdon,
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Helkath, and Rehob.
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 From the area that had been allotted to the tribe of Naphtali they were allotted three cities. Those cities were Kedesh in the Galilee region (it was one of the cities to which people could run/escape to be safe/protected), Hammoth-Dor, and Kartan.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 So altogether the Gershon clans were allotted 13 cities and the surrounding pasturelands.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 The other descendants of Levi, the ones who belonged to the Merari clans, were also allotted towns and their surrounding pasturelands. From the area that had been allotted to the tribe of Zebulun they were allotted four cities. They were Jokneam, Kartah,
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Dimnah, and Nahalal.
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 From the area that had been allotted to the tribe of Reuben they were allotted four cities. They were Bezer, Jahaz,
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Kedemoth, and Mephaath.
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 From the area that had been allotted to the tribe of Gad they were allotted four cities. They were Ramoth, which was one of the cities in the Gilead region to which people could run/escape to be safe/protected, Mahanaim,
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Heshbon, and Jazer.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Altogether twelve cities were allotted to the Merari clans.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 So altogether 48 cities were allotted to the tribe of Levi,
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 and each city had surrounding pastureland.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 In that way Yahweh allotted to the Israeli people all the land that he had promised to give to their/our ancestors. The Israeli people took control of [most of] those areas and started to live there.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 Just like he had promised our ancestors, Yahweh allowed them/us to have peace with the enemies that surrounded them/us. Yahweh enabled the Israelis/us to defeat their/our enemies.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Yahweh did all the things that he had promised to the Israeli people/us. Everything that he said would happen did happen.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.

< Joshua 21 >