< Joshua 17 >

1 [This is a list of] the land that was allotted to the tribe of Manasseh. Manasseh’s oldest son was Makir and his grandson was Gilead. Makir’s descendants were great warriors, so the lands in the Gilead and Bashan regions were allotted to their clan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 Land was also allotted to the other clans of the tribe of Manasseh: The clans of Abiezer, Helek, Asriel, Shechem, Hepher, and Shemida.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 Hepher’s son Zelophehad had no sons, but he had five daughters: Mahlah, Noah, Hoglah, Milcah, and Tirzah.
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 They went to Eleazar the Supreme Priest, and to Joshua and to the other Israeli leaders. They said, “[We want you to give us some land, because] Yahweh told Moses that he should give to us some land, just like you gave to the men.” So Eleazar did what Yahweh had commanded, and he allotted to them some land, just like he allotted to their uncles.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 So the tribe of Manasseh eventually had ten sections [of land west of the Jordan River] and [two sections, ] Gilead and Bashan, on the east side of the Jordan [River].
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 So those female descendants of Manasseh also were allotted land [on the west side of the river] just like the men were allotted. The other parts of the Gilead area were allotted to the male descendants of Manasseh.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 The land allotted to the tribe of Manasseh was between the land where the tribe of Asher lives and Michmethath [town], near Shechem [city]. The border extended south to the Tappuah Spring.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 The land near the Tappuah area belonged to the tribe of Manasseh, but the town of Tappuah, which was at the border of the land that was allotted to the tribe of Manasseh, was allotted to the tribe of Ephraim.
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 The border [of the land allotted to the tribe of Manasseh] extended south to Kanah Gorge. From there it extended [west] along the north side of the gorge and ended at the [Mediterranean] Sea.
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 The land on the south side of the gorge belonged to the tribe of Ephraim, and the land on the north side belonged to the tribe of Manasseh. The western border of the land allotted to the tribe of Manasseh was the [Mediterranean] Sea. To the north, the border of their land extended from the land allotted to the tribe of Asher [at the northwest] to the land allotted to the tribe of Issachar [at the northeast.]
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 But there are cities inside the area allotted to the tribes of Issachar and Asher. Those cities, along with their surrounding villages, were allotted to people from the tribe of Manasseh. These cities are Beth-Shan, Ibleam, Dor (which is also named Naphoth-Dor, ) Endor, Taanach, and Megiddo.
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 The men of the tribe of Manasseh were not able to force the people who lived in those cities to leave, so the people of the Canaan people-group continued to live in those cities.
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 But [years later] when the Israelis became better [warriors], they forced the Canaan people-group to work for them as slaves, although they did not force them to leave the land.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 The people of the tribes of Ephraim and Manasseh said to Joshua, “You allotted to us only one area of land, but there are a lot of us. Yahweh has blessed us very much [with the result that our tribe has grown very large]. So why did you give us only a small part of the land [RHQ]?”
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 Joshua replied to them, “[I agree that] you do not have enough land in the hilly area of the tribe of Ephraim. So, since you have a lot of people, I will allot more land to you, in the hilly region. But you will have to [cut down the trees] in the forest [and] make a place for yourselves in the land where the Periz and Repha people-groups live.”
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 The people of the tribes of Ephraim and Manasseh replied, “It is true that the land in the hilly area is not big enough for us, but the Canaan people-group who live in the lowlands, in Beth-Shan and the surrounding villages in that area, and in the Jezreel Valley, have iron chariots, [so we will not be able to defeat them]!”
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 Joshua replied to them, “Your tribe is very numerous and very powerful. So I will allot more land for you in the hilly area,
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 but you will have to cut down the trees in order to make a place for you to live. [It is true that] the Canaan people-group are strong and have iron chariots, but you will be able to force them to leave that valley.”
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Joshua 17 >