< Joshua 12 >

1 The Israelis took control of the land that was east of the Jordan River, from the Arnon River gorge [in the south] to Hermon Mountain [in the north], including all the land on the eastern side of the Jordan [River] Valley. That land previously belonged to the two kings whose armies the Israelis defeated.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 One of them was Sihon, the king of the Amor people-group. He lived in Heshbon [city] and ruled over the area from Aroer [town] along the Arnon River Gorge, north to the Jabbok River. His land started in the middle of the gorge, which was the border between his land and the land of the Ammon people-group. Sihon also ruled over [the southern] half of the Gilead region,
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 and over the land on the eastern side of the Jordan [River] Valley, from Galilee Lake [south] to the Dead Sea. He also ruled over the land [east of the Dead Sea] from Beth-Jeshimoth south to the side of Pisgah Mountain.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 The other king whom the Israeli army defeated was Og, the king of the Bashan [region]. He was the last of the descendants of [the giant] Rapha. He ruled that land, living alternately in Ashtaroth and Edrei [cities].
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 He ruled over the area from Hermon Mountain and Salecah [in the north], and over all the Bashan area in the east, and to the borders of the kingdoms of Geshur and Maacah to the west. Og ruled [the northern] half of the Gilead region, as far as the border of the land ruled by King Sihon.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moses, the man who served Yahweh [well], and all the Israeli army defeated the armies of those kings. Then Moses gave that land to the tribes of Reuben and Gad and half of the tribe of Manasseh.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 Joshua and the Israeli army also defeated kings who ruled over the land on the west side of the Jordan [River]. He gave that land to the Israeli people, dividing it among the other tribes. That land was between Baal-Gad [city] in the Lebanon Valley [in the far north all the way south] to Halak Mountain, which is near the land of the Edom people-group.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 That land included the mountains, the western hilly area, the Jordan [River] Valley, the [western] slopes of the mountains, the desert [in Judea], and the Negev [desert in the south]. That whole area was the land where the Heth, Amor, Canaan, Periz, Hiv, and Jebus people-groups lived. The Israeli army defeated the armies of the kings of each of these cities:
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 Jericho, Ai (which was near Bethel),
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 Jerusalem, Hebron,
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 Jarmuth, Lachish,
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 Eglon, Gezer,
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 Debir, Geder,
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 Hormah, Arad,
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 Libnah, Adullam,
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 Makkedah, Bethel,
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 Tappuah, Hepher,
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 Aphek, Lasharon,
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 Madon, Hazor,
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 Shimron Meron, Acshaph,
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 Taanach, Megiddo,
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 Kedesh, Jokneam in the Carmel area,
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 Dor in the Naphoth-Dor area, Goyim in the Gilgal area,
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 and Tirzah. There was a total of 31 kings [that the Israeli army defeated].
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.

< Joshua 12 >