< Job 37 >

1 “My heart pounds [DOU] when [I think about] that.
Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
2 Listen, all of you, to the thunder, which is like God’s voice [DOU].
Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
3 He causes thunder to be heard all across the sky, and he causes lighting to flash to the most distant places on the earth.
Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
4 After [the lightning flashes], we hear the thunder which is like [MET] God’s majestic voice; he does not restrain the lightning when he speaks.
Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
5 When God speaks, it is awesome, like thunder; he does amazing things which we cannot [fully] understand.
Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
6 He commands the snow to fall on the ground, and [sometimes] he causes it to rain very hard.
Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
7 And [when God does that, ] it prevents people [SYN] from working, in order that all people may know that he is the one who has done that (OR, what he can do).
Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
8 [When it rains, ] animals go into their hiding places, and they remain there [until the rain stops].
Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
9 The storms/hurricanes come from the place [in the south where they start], and the cold wind comes from the north.
Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
10 [In the (winter/cold season), the cold north wind is like] God’s breath [that] causes [MET] water to freeze; he causes the lakes/streams to become ice.
Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
11 God fills the clouds with moisture/hail, and lightning flashes from the clouds.
Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
12 He guides the clouds and causes them to move back and forth in order that they may accomplish all that he commands them to do, all over the world.
Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
13 Sometimes God sends rain to punish us, and sometimes he sends rain to show us that he acts kindly toward us.
Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
14 “Job, listen to this; stop and think about the wonderful things that God does.
Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
15 (Do you know how God commands the lightning to flash down from the clouds?/We do not know how God commands the lightning to flash down from the clouds.) [RHQ]
Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
16 Only God knows everything perfectly; so (do you know how he causes the clouds to (move/float) (amazingly/wonderfully) across the sky?/you certainly do not know how he causes the clouds to (move/float) (amazingly/wonderfully) across the sky!) [RHQ]
Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
17 No, you just sweat there in your clothes; [it is very oppressive] when the [hot] wind stops blowing from the south and [all the leaves on the trees] (become still/do not move).
Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
18 (Can you stretch out the skies like God does and make them as hard as [SIM] a sheet of polished brass?/You certainly cannot stretch out the skies like God does and make them as hard as [SIM] a sheet of polished brass!) [RHQ]
Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
19 “Job, tell us(exc) what we should say to God; we do not know anything [IDM]. As a result, we do not know what to say to him to defend ourselves.
Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
20 Should I tell God that I want to speak to him? No, because [if I did that, ] he might destroy me.
Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
21 Now, people cannot look [directly] at the sun when it shines brightly in the sky after the wind has blown the clouds away; [so, we certainly cannot look at the brightness of God].
Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
22 God comes out of the north with a light [that shines like] gold; his glory causes us to be afraid.
Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
23 Almighty God is very powerful, and we cannot come near to him. He always acts righteously, and he will never oppress us.
Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
24 That is the reason that we have an awesome respect for him; he does not pay attention to those who proudly, [but wrongly], think that they are wise.”
Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”

< Job 37 >