< Jeremiah 30 >

1 Yahweh gave me another message. He said,
Neno lilokuja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe likisema,
2 “[I], Yahweh, the God whom the Israeli people [say they belong to], am telling you that you should write down everything that I have said to you.
“Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema, 'Jiandikie mwenyewe katika baraua maneno yote niliyotangaza kwako katika barua.
3 [I want you to know that] some day I will free my people, [the people of] Israel and Judah, from being slaves [in Babylon]. I will bring them back to this land that I gave to their ancestors, and this land will belong to them again. [That will surely happen because] I, Yahweh, have said it.”
Maana ona, siku zinakuja—hili ni tangazo la Yahwe—nitakapowarudisha mateka wa watu wangu Israeli na Yuda. Mimi, Yahwe, nimesema hili. Kwa maana nitawarudisha kwenye nchi ambayo niliwapa babu zao, na wataimiliki.”'
4 Yahweh gave [to me] another message concerning [the people of] Israel and Judah.
Haya ni maneno ambayo Yahwe anatangaza kuhusu Israeli na Yuda,
5 This is what he said: “I hear people screaming because they are terrified [DOU]; there is no peace [in the land].
“Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Tumesikia sauti ya kutetemesha ya hofu na wala siyo ya amani.
6 But think about this: Men certainly do not [RHQ] give birth to babies. Therefore, why do strong men stand there, with their faces very white/pale, with their hands pressed against their stomachs, like women who are about to give birth to babies?
Ulizeni na muone kama mwanaume anamwogopa mtoto. Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake kama mwanamke anayejifungua mtoto? Kwa nini nyuso zao wote zimegeuka rangi?
7 [Terrible things will soon happen]; that will be a terrible day! There has never been such a time. It will be a time when [my] Israeli people will experience great trouble, but [finally] they will be saved [from their sufferings].”
Ole! Kwa maana siku hiyo itakuwa kuu, isiyofanana na yoyote. Utakuwa wakati wa huzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.
8 The Commander of the armies of angels says this: “At that time [it will be as though] I will sever/cut the ropes [that are around my people], and I will free them from being (slaves/forced to do what the King of Babylon wants them to do) [MET]. People in other countries will no longer be their bosses.
Kwa maana itakuwa katika siku hiyo—hili ni tangazo la Yahwe wa majeshi—kwamba nitaivunja nira ya shingo zenu, na nitaisambaza minyororo yenu, kwa hiyo wageni hawatawafanya watumwa tena.
9 My people will [again] serve me, Yahweh, their God, and [they will serve a king who is a descendant of] King David; [they will serve the king] whom I will appoint for them.
Bali watamwabudu Yahwe Mungu wao na kumtumikia Daudi mfalme wao, ambaye nitamfanya mfalme juu yao.
10 So, [you people of] Israel who serve me, do not be dismayed/worried [now], because [some day] I will bring you back from distant places; I will bring your descendants [back home] from the land to which they were exiled. [Then you] Israeli people will [again] live peacefully and safely, and there will not be any [nation] that will cause you to be terrified.
Kwa hiyo wewe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope—hili ni tangazo la Yahwe—na usikate tamaa, Israeli. Maana ona, niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa, Yakobo atarudi na kuwa katika amani; ataokolewa, na hapatakuwa na hofu zaidi.
11 I, Yahweh, say that I will be with you and will rescue you; I will completely destroy the nations to which I have scattered you. But I will not completely destroy you. I will punish you [for your many sins], but I will punish you [only] as severely as you deserve: I would be doing wrong if I did not punish you at all.”
Kwa maana niko pamoja nawe—hili ni tangazo la Yahwe—ili kukuokoa. Kisha nitaleta mwisho kamili kwa mataifa yote ambako nimewatawanya. Bali sitaweka mwisho kwako, ingawa ninakuadhibu kwa haki na kwa hakika sitakuacha bila kukuadhibu.'
12 Yahweh [also] says this: “[You have (suffered very much/endured many disasters)]; [it is as though] you have a terrible wound that cannot be cured.
Kwa maana Yahwe anasema hivi, 'Jeraha lako si la kupona; kidonda chako kimeenea.
13 There is no one to help you, no one to put a bandage on your wound. There is no [medicine that will] heal you.
Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako; hakuna utetezi kwa ajili ya kidonda chako ili upone.
14 All your allies [MET] have deserted you and they do not want to help you [any more]. [It is true that] I have punished you severely, [like your] enemies would wound you, because you have committed many sins and you are very guilty.
Wapenzi wako wote wamekusahau. Hawatakuangalia, kwa maana nimekujeruhi kwa jeraha la adui na nidhimu ya bwana mkatili kwa sababu ya uovu wako mwingi na dhambi zako zisizohesabika.
15 [Because that is true], why do you protest about my punishing you, [as though I had caused] a wound that could not be cured [RHQ]? It was necessary for me to punish you, because you had committed many sins and you were very guilty.
Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako? Maumivu yako hayaponyeki. kwa sambabu ya uovu wako mwingi, dhambi zako zisizohesabika, nimefanya mambo haya kwako.
16 But [some day] all those who [are trying to] destroy you will be destroyed; all your enemies will be exiled [to other nations]. All those who have stolen things from you will have their [valuable] possessions stolen, and all those who attack you will be attacked.
Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote wataenda utumwani. Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.
17 [Everyone] says that you are (outcasts/people that they no longer associate with), and that [you live in] Jerusalem, a city that no one cares about.” But Yahweh says, “I will heal your injuries/wounds and cause you to be healthy again.”
Kwa maana nitaleta uponyaji juu yako; nitakuponya majeraha yako—hili ni tangazo la Yahwe—nitafanya hivyo kwa sababu walikuita: Mwenyekutupwa. Hakuna anayeujali Sayuni.”
18 This is what Yahweh says: “I will bring the people of Israel back from the lands to which they were taken and enable them to possess their land and their houses again. [When that happens], Jerusalem will be rebuilt on top of its ruins, and the [king’s] palace will be rebuilt to be like it was before.
Yahwe anasema hivi, “Ona, niko karibu kuwarudisha mateka wa hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake. Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu, na jumba litakuwepo tena kama ilivyokuwa kawaida.
19 People will [again] sing joyfully to thank [me], and I will cause there to be more people [in Jerusalem], not fewer; I will cause them to be honored, not despised.
Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya ya shangwe itasikika kutoka kwao, kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza; nitawaheshimu ili kwamba wasifanywe wanyonge.
20 Their children will [prosper] like they did before. I will cause them to be a group of people [who worship] me, and I will punish any [nation] that oppresses them.
Kisha watu watakuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu wakati nitakapowaadhibu wote wanaowatesa kwa sasa.
21 One of their own people will be their king, and I will invite him to come close to me [to worship me], because no one [RHQ] would (dare/have courage) to come close to me [if I did not invite him].
Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao nitakapomleta karibu na atakapanikaribia mimi. kama sitafanya hivyo, ni nani atakayethubutu kunisogelea? —hili ni tangazo la Yahwe.
22 You [Israeli people] will be my people, and I will be your God.”
Kisha mtakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu.
23 Yahweh will punish [MTY] [your enemies]; [it will be like a great] storm; it will come down [like] a whirlwind, swirling around the heads of wicked people.
Ona, tufani ya Yahwe, ghadhabu yake, imekwenda nje. Ni tufani isiyokoma. Itazunguka juu ya vichwa vya watu waovu.
24 He will not stop being angry until he completely accomplishes [all] that he has planned. In the future, you will understand [all] of this [clearly].
Hasira ya Yahwe haitarudi mpaka itoke na kutimiza makusudi ya moyo wake. Katika siku za mwisho mtalielewa hili.”

< Jeremiah 30 >