< Hosea 7 >

1 “and when I wanted to heal them [again], [I did not do it, ] [because] I saw the wicked things that [the people of] Samaria [city] and [other places in] Israel [DOU] have done. They constantly deceive others; bandits rob people in the streets.
Wakati wowote ninapotaka kuponya Israeli, dhambi ya Efraimu inafunuliwa, pamoja na matendo maovu ya Samaria, kwa sababu wanafanya udanganyifu; mwizi huingia, na kundi la wanyang'anyi hushambulia mitaani.
2 But they do not realize that I do not forget all the evil things that they do. [It is as though] they are surrounded by [all] the sins that they commit; and [it is though] those sins are [always right] in front of me [MTY].
Hawatambui mioyoni mwao kwamba ninakumbuka matendo yao mabaya. Sasa matendo yao huwazunguka; yapo mbele ya uso wangu.
3 Their king is delighted with the wicked things that the people do; his officials are happy about the people’s lies.
Kwa sababu ya uovu wao wamemfanya mfalme awe na furaha, na maofisa wao kwa uongo wao.
4 [The king and his officials] are all treacherous. [They are always eager to do wicked things; ] they are like [SIM] an oven that is [very] hot: a baker mixes the dough and waits for it to expand, and he does not [need to] cause the oven to become hotter.
Wote ni wazinzi, kama tanuru iliyochomwa na mwokaji, ambaye huacha kuuchochea moto tangu kukanda unga mpaka kuwa chachu.
5 The king and his officials get very drunk during their festivals, carousing with others who also do foolish things.
Siku ya mfalme wetu, viongozi walijifanya wagonjwa na ukali wa divai. Alinyoosha mkono wake kwa wale waliokuwa wakidhihaki.
6 The officials angrily plan to murder the king; it is like [SIM] they have an oven in their inner beings. All during the night their [eagerness/wanting to murder the king] is like a fire that is smouldering, but in the morning it becomes like [MET] a roaring fire.
kwa mioyo kama tanuri, wao hupanga mipango yao ya udanganyifu. Hasira zao hulala usiku wote; asubuhi huwaka juu kama moto.
7 All those officials are like [MET] hot flames that completely burn up their rulers, so all their kings are murdered, and no one pleads with me [to help them].”
Wote wamepata moto kama tanuru, na huwaangamiza wale wanaowatawala. Wafalme wao wote wameanguka; hakuna hata mmoja wao ananiita.
8 “[The leaders of] Israel join with leaders of [godless] nations; so [the leaders of] Israel are [as worthless as] a pancake that is cooked on only one side.
Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu. Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa.
9 Joining with the rulers of foreign nations has caused Israel to be a weak [nation], but the Israelis do not realize that. Israel has become [like] [MET] a gray-haired old man, but the people of Israel do not realize it.
Wageni wamekula nguvu zake, lakini hajui. Nywele za mvi hunyunyiza juu yake, lakini hajui.
10 Their being proud [PRS] testifies against them, but in spite of that, they do not return to [me], Yahweh, their God, or [even] try to know me.
Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; hata hivyo, hawajarudi kwa Bwana, Mungu wao, wala hawakumtafuta licha ya hayo yote.
11 [The people of] Israel have become foolish and stupid like [SIM] doves. [First] they called out to Egypt [to help them], [and then] they sought help from Assyria.
Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara, humwita kwenda Misri, kisha huruka kwenda Ashuru.
12 But wherever they go [to get help], [I will not allow them to succeed]; [it will be as though] [MET] I will throw a net over them like [SIM] [a hunter uses a net to capture] birds; I will punish them for the evil things that they do.
Wakienda, nitasambaza wavu wangu juu yao, nami nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawaadhibu katika kusonga kwao pamoja.
13 Terrible things will happen to them because they abandoned/deserted me! They will be destroyed because they rebelled against me. I wanted to rescue them, but they tell lies about me.
Ole wao! Kwa maana wamepotea kutoka kwangu. Uharibifu unawajia! Wao wameasi dhidi yangu! Napenda kuwaokoa, lakini waliongea uongo dhidi yangu.
14 They do not cry out to me sincerely [IDM]; they [only] lie on their beds and wail. They gather together and ask [me to give them] grain and wine, but they turn away from me.
Wala hawakunililia kwa moyo wao wote, lakini wanaomboleza kwenye vitanda vyao. Wanakusanyika kwa ajili ya nafaka na divai mpya, nao wananiasi mimi.
15 I trained/taught them and enabled them to become strong, but now they plan [to do] evil things to me.
Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao, sasa wanapanga mabaya dhidi yangu.
16 They have rejected me, their Great God, and turned to their god Baal; they are [as useless] as [SIM] a crooked bow. Their leaders boast [that they are very strong], but they will be killed by [their enemies’] swords. As a result, [the people of] Egypt will laugh at them.”
Wanarudi, lakini harudi kwangu, Niliye Juu. Wao ni kama upinde usiotumainika. Maofisa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya udhalimu wa vinywa. Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.

< Hosea 7 >