< Exodus 35 >

1 Moses/I gathered all the Israeli people together and said to them, “This is what Yahweh has commanded you to do:
Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Bwana amewaamuru ninyi mfanye:
2 [Each week] you may work for six days, but on the seventh day you must rest. It is a sacred day, dedicated to Yahweh. Anyone who does any work on the seventh day must be executed.
Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa Bwana. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe.
3 Do not [even] light a fire in your homes on days of rest.”
Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”
4 Moses/I also said to all the Israeli people, “This is [also] what Yahweh has commanded:
Mose akaiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo Bwana aliloamuru:
5 Make offerings to Yahweh. Everyone who wants to should bring to Yahweh an offering. [These are the things that they may offer]: Gold, silver, bronze,
Toeni sadaka kwa Bwana kutoka mali mliyo nayo. Kila mmoja aliye na moyo wa kupenda atamletea Bwana sadaka ya dhahabu, fedha na shaba;
6 fine white linen, blue or purple or red cloth, [cloth made from] goats’ hair,
nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu na kitani safi; singa za mbuzi;
7 rams’ skins that are (tanned/dyed red), fine leather made from goatskins, wood from acacia [trees],
ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
8 oil for the lamps, spices to put in the olive oil for anointing and in the sweet-smelling incense,
mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezi kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
9 [valuable] onyx stones or [other] valuable stones to fasten onto the [priest’s] sacred apron and put on his sacred chest pouch.
vito vya shohamu, na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kisibau na kile kifuko cha kifuani.
10 “All the skilled workers among you should come and make all the things that Yahweh has commanded:
“Wote wenye ujuzi miongoni mwenu inawapasa kuja na kutengeneza kila kitu Bwana alichoamuru:
11 The Sacred Tent and its covering, its fasteners and its frames, its crossbars, its posts, its bases,
Maskani pamoja na hema lake na kifuniko chake, vibanio, mihimili, mataruma, nguzo na vitako;
12 the sacred chest with its poles and its lid, the curtain that will separate the Holy Place from the Very Holy Place,
Sanduku la Agano pamoja na mipiko yake, kifuniko cha kiti cha rehema na pazia linalokizuia;
13 the table with the poles [for carrying it] and all the things that will be used with the table, the sacred bread that will be offered to God,
meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate ya Wonyesho;
14 the lampstand for the lamps with all the things that will be used to take care of them, the oil for the lamps,
kinara cha taa kwa ajili ya mwanga pamoja na vifaa vyake vyote, taa na mafuta kwa ajili ya mwanga;
15 the altar for [burning] incense, and the poles [for carrying that altar], the oil for anointing and the sweet-smelling incense, the curtain for the entrance of the Sacred Tent,
madhabahu ya kufukiza uvumba pamoja na mipiko yake, mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri; pazia la mlangoni mahali pa kuingilia ndani ya maskani;
16 the altar for offering [sacrifices that will be completely] burned and its bronze grating, the poles [for carrying] that altar and all the things that will be used with it, the washbasin and its base,
madhabahu ya sadaka za kuteketeza pamoja na wavu wake wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote; sinia la shaba pamoja na tako lake;
17 the curtains [to surround] the courtyard and the posts and bases [for the posts from which to hang the curtains], the curtain for the entrance to the courtyard,
pazia la eneo la ua pamoja na nguzo zake na vitako vyake, pazia la ingilio la kwenye ua;
18 the pegs and ropes for the Sacred Tent and for the courtyard,
vigingi vya hema kwa ajili ya maskani pamoja na ua na kamba zake;
19 and the beautiful clothes that Aaron and his sons are to wear when they do their work in the Holy Place.”
mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu kwa ajili ya kuhani Aroni, na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.”
20 Then all the Israeli people returned [to their tents].
Ndipo jumuiya yote ya Waisraeli ilipoondoka mbele ya Mose,
21 Everyone who wanted to brought an offering to Yahweh. They brought some of the things that would be used to make the Sacred Tent and all the other items that would be used in the rituals, and the materials to make the sacred clothes [for the priests].
na kila mmoja aliyependa na ambaye moyo wake ulimsukuma alikuja na kuleta sadaka kwa Bwana, kwa ajili ya kazi katika Hema la Kukutania, kwa ajili ya huduma yake yote na kwa ajili ya mavazi matakatifu.
22 All the men and women who wanted to brought gold ornaments, earrings, rings, necklaces, and many other kinds of things made of gold, and they dedicated them to Yahweh.
Wote waliokuwa na utayari, wanaume kwa wanawake, wakaja wakaleta vito vya dhahabu vya kila aina: vipini, vipuli, pete na mapambo. Wote wakatoa dhahabu zao kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
23 And many [HYP] people who had blue, purple, or red cloth or fine white linen or cloth made from goats’ hair or rams’ skins that were (tanned/dyed red) or leather made from goatskins brought some of these things.
Kila mmoja aliyekuwa na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi, au singa za mbuzi, ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, au ngozi za pomboo, wakavileta.
24 All those who had silver or bronze brought them as offerings to Yahweh. All those who had some acacia wood that could be used for any of the work brought it.
Wale waliotoa sadaka ya fedha au shaba wakavileta kama sadaka kwa Bwana, na kila aliyekuwa na mti wa mshita kwa ajili ya kazi yoyote ile akauleta.
25 All the women who were skilled to make cloth brought fine linen thread and blue, purple, or red yarn/thread that they had made/spun.
Kila mwanamke aliyekuwa na ujuzi alisokota kwa mikono yake na alileta kile alichosokota, iwe ni nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, au za rangi nyekundu au kitani safi.
26 And all the women who wanted to made/spun thread from goats’ hair.
Wanawake wote waliopenda na waliokuwa na ujuzi wakasokota singa za mbuzi.
27 All the leaders brought valuable onyx stones and other valuable stones to be fastened to Aaron’s sacred apron and his sacred chest pouch.
Viongozi wakaleta vito vya shohamu pamoja na vito vingine vya thamani kwa ajili ya kuweka kwenye kisibau na kwenye kifuko cha kifuani.
28 They also brought spices [to put in the sweet-smelling incense], and they brought olive oil for the lamps and for the oil for anointing and for putting in the sweet-smelling incense.
Wakaleta pia vikolezi na mafuta ya zeituni kwa ajili ya mwanga, kwa ajili ya mafuta ya upako na kwa ajili ya uvumba wenye harufu nzuri.
29 All the Israeli men and women who wanted to brought these things to offer them to Yahweh, for doing the work that he had commanded Moses/me to do.
Waisraeli wote waume kwa wake waliokuwa wanapenda wakaleta mbele za Bwana kwa hiari yao wenyewe sadaka kwa ajili ya kazi yote ya Bwana aliyokuwa amewaagiza kuifanya kupitia kwa Mose.
30 Moses/I said to the Israeli people, “Listen carefully. Yahweh has chosen Bezalel, the son of Uri and grandson of Hur, from the tribe of Judah.
Kisha Mose akawaambia Waisraeli, “Tazameni, Bwana amemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
31 Yahweh has enabled his Spirit to completely control Bezalel and has given him ability and enabled him to know how to do very skilled work.
naye amemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, na uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
32 He can engrave skillful designs in gold, silver, and bronze.
ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
33 He can cut (jewels/valuable stones) and enclose them [in tiny gold frames]. He can carve things from wood and do other skilled work.
kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi wa kupendeza.
34 Yahweh has also given to him and to Oholiab, the son of Ahisamach, from the tribe of Dan, the ability to teach their skills to others.
Tena amempa yeye pamoja na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, uwezo wa kufundisha wengine.
35 He has given to them the ability to do all kinds of work that is done by craftsmen—those who create artistic things, those who make fine white linen, those who embroider designs using blue or purple or red yarn/thread, and those who make other cloth. They are able to do many [HYP] kinds of skillful work.
Amewajaza ustadi wa kufanya kazi za aina zote zifanywazo na mafundi, na wenye kubuni michoro, pia na watarizi kwa rangi za buluu, zambarau, nyekundu na kitani safi, na wafumaji: wote wakiwa mafundi na wabunifu hodari.

< Exodus 35 >