< Exodus 32 >

1 [(Moses/I) stayed on top of the mountain a long time]. When the people realized that he/I was not returning quickly, they gathered near Aaron and said to him, “We do not know what has happened to that man Moses who brought us here out of Egypt. So quickly, make us ([an idol/a statue of a god]) who will lead us!”
Watu walipoona kuwa Mose amekawia sana kushuka kutoka mlimani, walimkusanyikia Aroni na kumwambia, “Njoo, tutengenezee miungu itakayotutangulia. Kwa maana huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatujui jambo lililompata.”
2 Aaron replied to them, “All right, [I will do that, but] tell your wives and your sons and your daughters to take off all their gold earrings and bring them to me.”
Aroni akawajibu, “Vueni vipuli vya dhahabu ambavyo wake zenu, wana wenu na binti zenu wamevaa, mkaniletee.”
3 So the people did that. They took off all their gold earrings and brought them to Aaron.
Kwa hiyo watu wote wakavua vipuli vyao, wakavileta kwa Aroni.
4 He took all those gold earrings and melted them in a fire. He [poured the gold into a mold and] made a statue that looked like a young bull. The people saw it and said, “This is the god of us Israeli people! This is the one who brought us up from the land of Egypt!”
Akavichukua vile vitu walivyomkabidhi, akavifanyiza kwa kusubu sanamu yenye umbo la ndama, akaichonga kwa kutumia chombo. Kisha wakasema, “Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli, iliyowapandisha kutoka Misri.”
5 When Aaron saw [what was happening], he built an altar in front of the [statue of the] young bull. Then he announced, “Tomorrow we will have a festival to honor Yahweh!”
Aroni alipoona hili, akajenga madhabahu mbele ya yule ndama na kutangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa Bwana.”
6 So the people got up early the next morning and brought animals to kill and burn as sacrifices on the altar. They also brought sacrifices to maintain fellowship with Yahweh. Then they sat down to eat and drink [wine]. Then they got up and started dancing in a very immoral way.
Kwa hiyo siku iliyofuata watu wakaamka asubuhi na mapema na kutoa sadaka za kuteketeza na sadaka za amani. Baadaye watu wakaketi kula na kunywa, nao wakasimama, wakajizamisha katika sherehe.
7 Then Yahweh said to Moses/me, “Go back down from the mountain, because your people, the ones that you brought up here from Egypt, have [already] (become very depraved/wicked)!
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Shuka, kwa sababu watu wako, uliowatoa Misri, wamepotoka.
8 They have already (left the road that I showed them/stopped obeying me)! They have made [a statue of] a young bull from melted gold. They have worshiped it and offered sacrifices to it. And they are saying, ‘This is the god of us Israeli people! This is the one who brought us up from Egypt!’”
Wamekuwa wepesi kugeuka na kuacha niliyowaamuru, na wamejitengenezea sanamu ya kuyeyusha yenye umbo la ndama. Wameisujudia na kuitolea dhabihu, nao wamesema, ‘Hii ndiyo miungu yenu, ee Israeli iliyokupandisha kutoka Misri.’”
9 Then Yahweh said to Moses/me, “I have seen that these people are very stubborn.
Bwana akamwambia Mose, “Nimeona watu hawa, nao ni watu wenye shingo ngumu.
10 I am very angry with them, and so I am going to get rid of them. Do not try to stop me! Then I will cause you and your descendants to become a great nation.”
Sasa niache ili hasira yangu ipate kuwaka dhidi yao, nami nipate kuwaangamiza. Kisha nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa.”
11 But Moses/I pleaded with his/my God, Yahweh, and said, “Yahweh, (you should not be very angry with your people!/why are you so angry with your people [RHQ]?) These are the people whom you rescued from Egypt with very great power [MTY, DOU]!
Lakini Mose akamsihi Bwana Mungu wake, akasema, “Ee Bwana, kwa nini hasira yako iwake dhidi ya watu wako, wale uliowatoa Misri kwa uweza mkuu na mkono wenye nguvu?
12 Do not [do anything that would] allow the people of Egypt to say, ‘Their god led them out from our country, but [he did that] only [because he wanted] to kill them in the mountains and get rid of them completely [RHQ]!’ Stop being so angry! (Change your mind/Do not do what you have told me that you will do)! Do not do to your people this terrible thing [that you have just said that you will do]
Kwa nini Wamisri waseme, ‘Ni kwa nia mbaya aliwatoa Misri, ili awaue milimani na kuwafuta usoni mwa dunia’? Achilia mbali hasira yako kali, waonee huruma na usilete maafa juu ya watu wako.
13 Think about your servants Abraham, Isaac, and Jacob. You solemnly promised them, ‘I will enable you to have as many descendants as there are stars in the sky.’ You said to them, ‘I will give to your descendants all the land that I am promising to give them. It will be their land forever.’”
Wakumbuke watumishi wako Abrahamu, Isaki na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe: ‘Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa wazao wako nchi hii yote ambayo niliwaahidia, nayo itakuwa urithi wao milele.’”
14 So Yahweh changed his mind. He did not do to his people the terrible thing that he said he would do.
Kisha Bwana akawaonea huruma, wala hakuleta juu ya watu wake maafa aliyokuwa amekusudia.
15 Moses/I turned away from God and went down the mountain, carrying in his hands the two stone slabs on which Yahweh had engraved his commandments. He had written on both sides of the slabs.
Mose akageuka, akashuka kutoka mlimani akiwa na vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake. Vilikuwa vimeandikwa pande zote mbili, mbele na nyuma.
16 God [himself] had made the slabs, and he was the one who had engraved the commandments on them.
Vibao hivyo vilikuwa kazi ya Mungu; maandishi yalikuwa mwandiko wa Mungu, yaliyochorwa kama muhuri juu ya vibao.
17 Joshua heard the very loud noise of the people shouting. So when he and I got near the camp, Joshua said, “There is a noise in the camp that sounds like [the noise of] a battle!”
Yoshua aliposikia sauti za watu wakipiga kelele, akamwambia Mose, “Kuna sauti ya vita kambini.”
18 But Moses/I replied, [“No], that is not the shouting that people do when they have won a victory or when they have been defeated [in a battle] What I hear is the sound of [loud] singing!”
Mose akajibu: “Si sauti ya ushindi, wala si sauti ya kushindwa; ni sauti ya kuimba ninayosikia.”
19 As soon as Moses/I came close to the camp and saw the statue of the young bull and saw the people dancing, he/I became extremely angry. He/I threw the stone tablets that he/I was carrying down onto the ground, there at the base of the mountain.
Mose alipoikaribia kambi na kuona yule ndama na ile michezo, hasira yake ikawaka, akatupa vile vibao vilivyokuwa mikononi mwake, akavipasua vipande vipande pale chini ya mlima.
20 Then he/I took the statue of the young bull that they had made and melted it in the fire. [When it cooled], he/I ground it into [fine] powder. Then he/I mixed the powder with water and forced the Israeli people to drink it.
Kisha akamchukua yule ndama waliokuwa wamemtengeneza na kumchoma kwenye moto, kisha akamsaga kuwa unga, akanyunyiza kwenye maji na kuwafanya Waisraeli wanywe.
21 Then he/I said to Aaron, “What did these people do to you, with the result that you have made them commit such a terrible sin?”
Mose akamwambia Aroni, “Watu hawa walikufanyia nini, hata ukawaongoza kufanya dhambi kubwa hivyo?”
22 Aaron replied, “Please do not be angry with me, sir. You know that these people are very determined to do evil things.
Aroni akamwambia, “Usikasirike bwana wangu. Unajua jinsi watu hawa walivyo tayari kwa maovu.
23 They said to me, ‘As for that man Moses, the one who brought us up here from the land of Egypt, we do not know what has happened to him. So make for us an idol that will lead us!’
Wao waliniambia, ‘Tufanyie miungu itakayotuongoza. Kwa kuwa huyu jamaa yetu Mose aliyetupandisha kutoka Misri, hatufahamu yaliyompata.’
24 So I said to them, ‘Everyone who is wearing [gold earrings] should take them off.’ So they [took them off and] gave them to me. I threw them into the fire, and out came this statue of a young bull!”
Kwa hiyo nikawaambia, ‘Yeyote aliye na kito chochote cha dhahabu avue.’ Kisha wakanipa hiyo dhahabu, nami nikaitupa motoni, akatokea huyu ndama!”
25 Moses/I saw that Aaron had allowed the people to become completely out of control and to do things that would make their enemies think the Israeli people were foolish.
Mose akaona kuwa watu wameasi, kwa kuwa Aroni alikuwa amewaacha waasi, na hivyo kuwa kichekesho kwa adui zao.
26 So he/I stood at the entrance to the camp and shouted, “Everyone who is loyal to Yahweh should come [closer] to me!” So the descendants of Levi gathered around him/me.
Kwa hiyo Mose akasimama kwenye ingilio la kambi, akasema, “Yeyote aliye upande wa Bwana, aje upande wangu.” Walawi wote wakamjia.
27 Then he/I said to them, “Yahweh, the God of us Israeli people, commands that every one of you should fasten your sword to your side, and then go through the camp from this entrance to the other one, and kill some of your relatives and your companions and your neighbors.”
Ndipo alipowaambia, “Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Kila mmoja wenu ajifunge upanga wake kiunoni aende huku na huko kambi yote mwisho hadi mwisho mwingine, kila mmoja amuue ndugu yake, na rafiki yake na jirani yake.’”
28 The descendants of Levi did what Moses/I told them to do, and they killed 3,000 men on that day.
Walawi wakafanya kama Mose alivyoamuru, siku ile wakafa watu wapatao 3,000.
29 Moses/I said to the descendants of Levi, “Today you have dedicated yourselves to serving Yahweh by (killing/not sparing) [even] your own sons and brothers, and as a result Yahweh will bless you.”
Kisha Mose akasema, “Leo mmewekwa wakfu kwa Bwana, kwa kuwa mlikuwa kinyume na wana wenu wenyewe na ndugu zenu, naye Mungu amewabariki leo.”
30 The next day, Moses/I said to the people, “You have committed a terrible sin. But I will now climb up the mountain again to talk with Yahweh. Perhaps I can [persuade him] to forgive you for sinning [like this].”
Siku iliyofuata Mose akawaambia watu, “Mmefanya dhambi kubwa. Lakini sasa nitapanda juu kwa Bwana, labda nitaweza kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.”
31 So Moses/I went back up the mountain and said to Yahweh, “I am sorry to admit that these people have committed a terrible sin. They have made for themselves a gold idol and have worshiped it.
Hivyo Mose akarudi kwa Bwana na kumwambia, “Lo! Hawa watu wamefanya dhambi kubwa namna gani! Wamejitengenezea miungu ya dhahabu.
32 But now I ask you to please forgive them for having sinned. If you will not forgive them, then erase my name from the book in which you have written [the names of your people].”
Lakini sasa nakusihi, wasamehe dhambi yao; lakini kama sivyo, basi nifute kutoka kwenye kitabu ulichoandika.”
33 But Yahweh said to Moses/me, “It is [only] those who have sinned against me whose names I will erase from that book.
Bwana akamjibu Mose, “Yeyote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta kutoka kwenye kitabu changu.
34 Now you go back down and lead the [Israeli] people to the place that I told you about. Keep in mind that my angel will go in front of you. But, at the time that I determine, I will punish them for their sin.”
Sasa nenda, uongoze hao watu mpaka mahali nilipokuambia, naye malaika wangu atakutangulia. Pamoja na hayo, wakati utakapofika wa mimi kuwaadhibu, nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi yao.”
35 [Later] Yahweh caused a plague to strike the people because they had told Aaron to make the gold [statue of a] young bull.
Ndipo Bwana akawapiga watu kwa ugonjwa wa tauni kwa sababu ya yale waliyoyafanya kwa ndama yule ambaye alitengenezwa na Aroni.

< Exodus 32 >