< Ephesians 6 >

1 You children, because you (belong to/have a close relationship with) the Lord [Jesus], obey your parents, because it is right [for you to do] that.
Enyi watoto, watiini wazazi wenu Kikristo maana hili ni jambo jema.
2 God commanded [in the Scriptures], [Greatly] respect your father and mother. That is the first law [that God] commanded in [which he also] promised [something]. [He promised],
“Waheshimu Baba na mama yako,” hii ndiyo amri ya kwanza ambayo imeongezewa ahadi, yaani,
3 [If you do] that, you will prosper, and you will live a long time.
“Upate fanaka na miaka mingi duniani.”
4 You parents (OR, You fathers), do not treat your children so severely that they become angry. Instead, bring them up well by instructing them and by disciplining them in [the manner that] the Lord [Jesus wants you to do].
Nanyi akina baba, msiwachukize watoto wenu ila waleeni katika nidhamu na mafundisho ya Kikristo.
5 You slaves, obey those who are [your masters]. Obey them very respectfully and sincerely [DOU], just like you obey Christ.
Enyi watumwa, watiini mabwana zenu hapa duniani kwa hofu na tetemeko; fanyeni hivyo kwa unyofu wa moyo kana kwamba mnamtumikia Kristo.
6 Obey them, not only when they are watching [MTY] you, and not only to cause them to think highly/well of you. Instead, obey them as [though you were] [MET] slaves of Christ, [not slaves of your masters]. Do enthusiastically what God wants [you to do].
Fanyeni hivyo si tu wakati wanapowatazama ili mjipendekeze kwao, bali tumikieni kwa moyo kama atakavyo Mungu kwa sababu ninyi ni watumishi wa Kristo.
7 Serve [your masters] zealously/wholeheartedly, as you would serve the Lord [Jesus], not as you would serve [ordinary] people.
Muwe radhi kutumikia kwa ajili ya Bwana na si kwa ajili ya watu.
8 [Do this because] you know that [some day] the Lord Jesus will reward each person for whatever good [deeds] that person has done. He will reward people who are slaves and people who are not slaves.
Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
9 You masters, just like your slaves [should serve you well], you similarly must treat them well. Stop threatening [to beat] them [if they do not do their work well]. Do not forget you and they have the same Lord who is in heaven. [So he is the one who will say to you and your slaves whether he approves of what you and they have done], and [when he judges people], he does not act more favorably [toward some than he acts toward others].
Nanyi mnaotumikiwa, watendeeni vivyo hivyo watumwa wenu, na acheni kutumia vitisho. Kumbukeni kwamba ninyi pia kama vile wao, mnaye Bwana yuleyule mbinguni, kwake cheo cha mtu si kitu.
10 Finally, at all times rely/depend completely on the Lord [Jesus] to strengthen you [spiritually] by his own mighty power.
Hatimaye, nawatakeni muwe imara katika kuungana na Bwana na kwa msaada wa nguvu yake kuu.
11 [Just like a soldier] puts on all his (armor/things [to help him fight]) [MET], you should [use every spiritual resource/help that God provides for you], in order that you may successfully resist the devil when he cleverly tries [to oppose you].
Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.
12 You must do this because the fighting that we [believers] do is not only against human beings [SYN]. Instead, we are also fighting against evil spirits who rule and have authority over all that is evil [MET] in the world. And we are fighting against evil spirits who are in heavenly places (OR, everywhere). (aiōn g165)
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki ulimwengu huu wa giza. (aiōn g165)
13 Therefore, [just like a soldier] puts on all his (armor/things to help him fight) [MET], [use well all the spiritual resources/helps that God provides for you]. Do that in order that you may be able to resist successfully the devil and all his powerful evil spirits [MTY] every time they (attack you/tempt you to sin or cause something bad to happen to you). [Do it also in order that] when you have done all that you can to resist them [when they attack you], you will still be ready to resist them [when they attack you the next time].
Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka mwisho, muwe bado thabiti.
14 You must be ready to firmly [resist the devil and his evil spirits] [MET], [just like soldiers must be ready to resist the enemy. Prepare for doing that by doing these things]: [To be strong spiritually], hold firmly to [God’s] truth, just like soldiers prepare (to stand firm against/to firmly resist) their enemies by fastening their belts around their waists [MET]. Act righteously [in order to protect yourself against demonic attacks, just like soldiers] put on breastplates [to protect their chests against their enemies’ attacks] [MET].
Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,
15 Hold fast the good message [that gives us] peace [with God, just like soldiers] put on their boots firmly [MET] (to stand firm [against/] firmly [resist]) [their enemies].
na hamu ya kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.
16 In addition, keep trusting firmly [in the Lord. That will enable you to protect yourselves from anything that Satan], the evil one, [may do to harm you spiritually, just like soldiers] carry shields [to protect themselves against] the arrows that have flaming tips [that their enemies shoot at them] [MET].
Zaidi ya hayo yote, imani iwe daima kama ngao mikononi mwenu, iwawezeshe kuizima mishale ya moto ya yule Mwovu.
17 And [rely/depend on the fact that God] has saved you, [in order to protect yourselves against demonic attacks, just like soldiers] put on a helmet [to protect] their [heads from attacks by] their [enemies] [MET]. And be ready to use [the weapon that God’s] Spirit [has given you], which is the message of God, [in order to fight against] ([demonic powers/Satan]), [just like soldiers] use their swords [to fight against their enemies] [MET].
Upokeeni wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho Mtakatifu.
18 As you are doing that, keep praying [to God] at all times, and requesting him [to do things for you and others; ] and let God’s Spirit [direct what you pray]. For this purpose, always be [spiritually] alert/watchful, and (always be persistent in/never quit) praying for all God’s people.
Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
19 And [specifically], pray for me. Pray that God will tell me what I should say [MTY] whenever I speak, in order that I may boldly tell others the good message about Christ. People did not know that message before, [but God has now revealed it to me].
Niombeeni nami pia ili niongeapo Mungu anijalie cha kusema, niweze kuwajulisha watu fumbo la Habari Njema kwa uthabiti.
20 I am (a representative [of Christ]/one who speaks on behalf [of Christ]) [as I tell this message to others, and] I am in prison [MTY] [because of that]. Pray that when I tell [others about Christ], I may speak without being afraid, because that is how I ought to speak.
Mimi ni balozi kwa ajili ya Habari Njema hiyo ingawa sasa niko kifungoni. Ombeni, basi, ili niweze kuwa hodari katika kuitangaza kama inipasavyo.
21 In order that you may know about [what is happening] to me and what I am doing, I am sending Tychicus [to you with this letter]. He will tell you everything [that is happening here]. He is a fellow believer whom we all [(inc)] love very much, and he serves the Lord [Jesus] faithfully.
Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu wa Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.
22 That is the reason that I am sending him [to you]; I want you to know (how my companions and I are/what is happening to my companions and me), and I want him to encourage you [SYN].
Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.
23 [I pray that] God our Father and the Lord Jesus Christ will cause all of you fellow believers to have [inner] peace, and [enable you to] love [each other] and to continue trusting [in Christ].
Ninawatakieni ninyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.
24 I pray that God will continue to act kindly to [you and] to all [others] who love our Lord Jesus Christ and will never quit loving him.
Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.

< Ephesians 6 >