< Ecclesiastes 7 >

1 [Having] a good reputation [MTY] is better than fine perfume, and the day that we die is better than the day that we are born.
Jina zuri ni bora kuliko manukato ya gharama, na siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
2 It is better to go to a house where people are mourning [about someone who has died] than to go to a house where people are feasting, because everyone will die some day, and people who are alive should think seriously [IDM] about that.
Ni bora kwenda kwenye nyumba ya maombolezo kuliko nyumba ya karamu, kwa kuwa maombolezo huja kwa watu wote wakati wa mwisho wa uhai, kwa hiyo watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni.
3 It is better to be sad than to be [always] laughing, because being sad can cause us to think more about how we should conduct our lives [IDM].
Huzuni ni bora kuliko kicheko, kwa kuwa baada ya uso wa huzuni huja furaha ya moyo.
4 Wise [people] who go to where others are mourning think about [the fact that some day they also will] die, but foolish people [PRS] [do not think about that]; they are always [MTY] laughing.
Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu.
5 It is better to pay attention to [someone who is wise] you than to listen to the songs of a foolish person.
Ni bora kusikiliza maonyo ya mtu mwenye hekima kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
6 By [listening to] foolish people laughing we will not [learn any more than by listening to] the crackling of thorns [being burned] under a pot. Listening to fools is senseless.
Kwa kuwa kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Huu pia ni mvuke.
7 When wise people say to others, “You must pay me a lot of money for me to protect you,” that causes those wise people to become foolish, and [accepting] bribes causes people to become unable to do what is fair/just.
kweli jeuri humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, na rusha huharibu moyo.
8 Finishing something is better than starting something, and being patient is better than being proud.
Ni heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo; na watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni.
9 Do not quickly (lose your temper/react to things angrily), because it is foolish people [SYN] who become very angry.
Usikasirike haraka rohoni mwako, kwa sababu hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu.
10 Do not say, “Things were a lot better [RHQ] previously,” because it is people who are not wise who say that.
Usiseme, “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa kuwa sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili.
11 Being wise is better than inheriting [valuable things]; being wise provides lasting benefits for every person on the earth [MTY].
Hekima ni njema kama vitu vya thamani tunavyorithi kutoka kwa wazazi wetu. Inatoa faida kwa wale wanaoliona jua.
12 We are [sometimes] protected by being wise like we are [sometimes] protected by having a lot of money, but being wise is better [than having a lot of money], [because] being wise prevents us from [doing foolish things that would] cause us to die.
Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
13 Think [carefully about] what God has done. Certainly no one can [RHQ] cause to become straight the things that God has caused to be crooked.
Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
14 When things are going well for you, be happy, and when things are not going well for you, remember that God is the one who causes good things to happen and who also causes disasters.
Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
15 During all the time that I have been alive I have seen a lot of [HYP] things that seem senseless. I have seen righteous people die [while they are still young], and I have seen wicked people remain alive for a very long time in [spite of] their continuing to be wicked.
Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
16 [So] do not think that you are very righteous and do not think that you are very wise, [because if you think those things], you will destroy yourself.
Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
17 If you do what is evil or do what is foolish, you might die while you are still young.
Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
18 Continue to avoid doing what is evil and doing what is foolish; avoid doing both of those things by continually revering God.
Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
19 If you are wise, you will be more powerful/influential than the ten most powerful/influential men in your city.
Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
20 There is no one in this world who [always] does what is right and who never sins.
Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
21 Do not pay attention [IDM] to everything that people say, because if you do that, you might hear your servant cursing you.
Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
22 You know that you have also cursed other people.
Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
23 I said [to myself] that I would use my wisdom to study all the things [that I have written about], but I was not able to do it successfully.
Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
24 Wisdom seems to be far from me; there is no one [RHQ] who can truly understand everything.
Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
25 But I decided to investigate things and by my wisdom try to understand the reason for everything. I also wanted to understand why people act wickedly and why they act very foolishly.
Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.
26 [One thing I learned was that] (allowing a woman to seduce you/having sex with a woman to whom you are not married) is worse than dying. A woman who tries to seduce men is [as dangerous as] a trap [MET]. [If you allow her to put] her arms [around you, it will be as though she will be fastening you with] chains. Women like that will capture sinful men, but men who please God will escape from such women.
Nikapata kufahamu kwamba uchungu kuliko kifo, ndivo alivyo mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego, na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo. Yeyote ampendezaye Mungu ataponyoka kutoka kwake, lakini mwenye dhambi atachukuliwa naye.
27 This is what I have learned: I tried to learn more and more about things to try to find out the reason for everything,
“Tafakari kile nilichovumbua,” asema Mwalimu. “Nimekuwa nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli.
28 and I continued to try to learn more, but I could not find [all that I was searching for]. [But] one thing that I found out was that among 1,000 [people] I found one righteous man, but I did not find even one righteous woman.
Hii ndiyo bado natafuta, lakini bado sijapata. Sikupata mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu, lakini sikupata mwanamke miongoni mwa wale wote.
29 [But] I did learn one thing: When God created people, they were righteous, but they have found many ways to do many evil things.
Nimegundua hili: kwamba Mungu alimuumba binadamu akiwa mnyoofu, lakini wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi.

< Ecclesiastes 7 >