< Deuteronomy 31 >

1 When Moses/I finished saying all that to the Israeli people,
Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:
2 he/I said to them, “Now I am 120 years old. I am no longer able to go everywhere [that you go] (OR, to be your leader). Furthermore, Yahweh has told me that I will not cross the Jordan [River].
“Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’
3 But Yahweh our God will go ahead of you. He will [enable you to] destroy the nations that are living there, in order that you can occupy their land. Joshua will be your leader, which is what Yahweh already told me.
Bwana Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema.
4 Yahweh will do to those nations what he did to Sihon and Og, the two kings of the Amor people-group when he destroyed their armies [MTY].
Naye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.
5 Yahweh will enable you to conquer those nations, but you must [kill all of the people of those nations, which is] what I have commanded you to do.
Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru.
6 Be brave and confident. Do not be afraid of those people. [Do not forget that] it is Yahweh our God who will go with you. He will always help [LIT] you and never abandon you.”
Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”
7 Then Moses/I summoned Joshua, and while all the Israeli people were listening, he/I said to him, “Be brave and confident. You are the one who will lead these people into the land that Yahweh promised to our ancestors that he would give to them, and you will enable them to occupy it.
Kisha Mose akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ile Bwana aliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao.
8 It is Yahweh who will go ahead of you. He will be with you. He will always help [LIT] you. He will never abandon you. So do not be afraid or dismayed.”
Bwana mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”
9 Moses/I wrote down all these laws [on two scrolls] and gave [one scroll] to the priests, who carried the chest containing the Ten Commandments, and [gave the other scroll] to the Israeli elders.
Kwa hiyo Mose akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano la Bwana na wazee wote wa Israeli.
10 Moses/I told them, “At the end of every seven years, at the time that all debts are canceled, [read this to the people] during the Festival of [Living in Temporary] Shelters.
Kisha Mose akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda,
11 Read it to all the Israeli people when they gather at the place that Yahweh chooses for them to worship him.
Waisraeli wote wanapokuja mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao.
12 Gather together everyone—men, women, children, even the foreigners [who are living] in your towns—in order that they may hear [these laws] and learn to revere Yahweh our God, and to faithfully obey everything that is written in these laws.
Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu na kufuata kwa bidii maneno yote ya sheria hii.
13 [If they do that], your descendants who have never known these laws will hear them and will also learn to revere Yahweh our God, during all the years that they live in the land that you are about to cross the Jordan [River] to occupy.”
Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumcha Bwana Mungu wenu kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
14 Then Yahweh said to Moses/me, “Listen carefully. You will soon die. Summon Joshua, and you go to the Sacred Tent with him, in order that I may appoint him [to be the new leader].” So Joshua and Moses/I went to the Sacred Tent.
Bwana akamwambia Mose, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Mose na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.
15 There Yahweh appeared to them/us in a pillar of cloud, and that cloud was close to the door of the tent.
Kisha Bwana akatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema.
16 Yahweh said to Moses/me, “You will soon die [EUP]. Then these people will become unfaithful [MET] to me. They will abandon me and (break/stop obeying) the agreement that I made with them. They will begin to worship the foreign/pagan gods [that are worshiped by the people] of the land that they will enter.
Kisha Bwana akamwambia Mose: “Unakwenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja Agano nililofanya nao.
17 When that happens, I will become very angry with them. I will abandon them [DOU] and I will no longer help them [IDM], and I will destroy them {they will be destroyed}. Many terrible things will happen to them, with the result that they will say, ‘[We are certain that] [RHQ] these things are happening to us because our God is no longer with us.’
Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’
18 And because of all the evil things that they will have done, and [especially because] they will have started to worship other gods, I will refuse to help [IDM] them.
Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.
19 “So, [I am going to give you] a song. Write it [on a scroll] and teach it to the Israeli people and cause them to memorize it. It will be like a witness that accuses them.
“Sasa ujiandikie wimbo huu, uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao.
20 I am about to take them into a very fertile [IDM] land, a land that I solemnly promised their ancestors that I would give to them. There they will have plenty to eat, with the result that their [stomachs] will [always] be full and they will become fat. But then they will turn to other gods and start to worship them, and they will despise me and (break/stop obeying) the agreement that I made with them.
Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi itiririkayo maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja Agano langu.
21 And they will experience many terrible disasters. After that happens, their descendants will never forget this song, and it will be like a witness [that says, ‘Now you know why Yahweh punished your ancestors].’ I will soon take them into the land that I vowed that I would give to them; but now, before I do that, I know what they are thinking [that they will do when they are living there].”
Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.”
22 So on the day that [Yahweh gave Moses/me this song], he/I wrote it down, and he/I taught it to the Israeli people.
Hivyo Mose akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.
23 Then Yahweh (appointed/set apart) Joshua and said to him, “Be brave and confident, because you will lead the Israeli people into the land that I vowed that I would give to them. And I will be with you.”
Bwana akampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”
24 Then Moses/I finished writing on a scroll all the laws that Yahweh had told to him/me.
Baada ya Mose kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho,
25 Then Moses/I told the descendants of Levi, who were carrying the Sacred Chest that contained the Ten Commandments,
akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Bwana agizo hili, akawaambia:
26 “Take this scroll on which these laws [are written], and place it beside the Sacred Chest that contains the agreement that Yahweh our God made with you, in order that it may remain there to testify [about what Yahweh will do] to the people [if they disobey him].
“Chukueni Kitabu hiki cha Sheria mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Bwana Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu.
27 [I say this] because I know that these people are very stubborn [DOU]. They have rebelled against Yahweh all during the time that I have been [with them], and they will rebel much more after I die!
Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Bwana nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu!
28 So gather all the elders of the tribes and your officials, in order that I can tell them the words [of this song], and request all those who are in heaven and on the earth to be witnesses to testify against these people.
Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao.
29 I say that because I know that after I die, the people will become very wicked. They will turn away from doing everything that I have commanded them to do. And in the future, because of all the evil things that they will do, they will cause Yahweh to become angry with them. And he will cause them to experience disasters.”
Kwa kuwa ninajua baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata kwa sababu mtafanya maovu mbele ya macho ya Bwana, na kuchochea hasira yake kwa yale mikono yenu itakayokuwa imefanya.”
30 Then, while all the Israeli people listened, Moses/I sang/recited this entire song to them:
Mose akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:

< Deuteronomy 31 >