< Deuteronomy 29 >

1 These are the things that the Israelis were required to do to keep the agreement that Yahweh was making with them. Moses/I commanded them to keep this agreement [when they/we were] in the Moab region [on the east side of the Jordan River]. This was in addition to the agreement that Yahweh had made with them/us at Sinai [Mountain].
Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
2 Moses/I summoned all the Israeli people and said to them, “You saw [SYN] for yourselves what Yahweh did to the king of Egypt and to his officials and to his entire country.
Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
3 You [SYN] saw all the plagues [that Yahweh caused them to experience], and all the various miracles [DOU] [that Yahweh performed].
mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
4 But until now, Yahweh has not enabled you to understand [the meaning of] all that you have seen and heard.
Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
5 For 40 years Yahweh has led you while you traveled/walked through the desert. During that time, your clothes and your sandals have not worn out.
Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
6 You did not have bread to eat or wine or other fermented/strong drinks to drink, but Yahweh [took care of you], in order that you would know that he is your God.
Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
7 “And when we came to this place, Sihon, the king who ruled in Heshbon [city], and Og, the king who ruled the Bashan [region], came [with their armies] to attack us, but we defeated them.
Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
8 We took/conquered their land and divided it among the tribes of Reuben and Gad, and half of the tribe of Manasseh.
Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
9 “So faithfully keep all of this agreement, in order that you will be successful in everything that you do.
Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
10 Today all of us are standing in the presence of Yahweh our God. The leaders of all our tribes, our elders, our officials, all you Israeli men,
Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
11 your wives, your children, and the foreigners who live among you and cut wood for you and carry water for you, are here.
watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
12 [We are here] today to promise to keep this solemn agreement with Yahweh.
Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
13 [He is making this agreement with you] in order to confirm that you are his people, and that he is your God. This agreement is what he promised you, and which is what he vowed to give to your ancestors Abraham, Isaac and Jacob.
ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
14 This agreement is not only with you.
Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
15 He is making this agreement with us [who are here today] and also with our descendants who are not yet born.
pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
16 “You remember [the things that our ancestors suffered] in Egypt, and how they traveled through the land that belonged to other nations [after they came out of Egypt].
Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
17 In those countries they saw those disgusting idols made of wood and stone and [decorated with] silver and gold.
Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
18 So be sure that no man or woman or family or tribe that is here [today] turns away from Yahweh our God, to worship/serve the gods of those nations. Doing that would be like a root [of a plant that would grow] among you and bear poisonous and bitter fruit [MET].
Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
19 “Be sure that no one here today who hears this agreement thinks, ‘Everything will go well with me, even if I stubbornly do what I want to.’ If you are stubborn like that, the result will be that Yahweh will eventually get rid of all of you, both good people and evil people [MET].
Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
20 Yahweh will not forgive anyone who is [stubborn] like that. Instead, he will be extremely angry [DOU] with that person, and that person will experience all the curses that I have told you about, until Yahweh gets rid of that person and his family [IDM].
Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
21 From all the tribes of Israel, Yahweh will separate that individual. Yahweh will cause him to experience all the disasters that I have listed in the agreement that states the things that Yahweh will do to curse [those who disobey] the laws [that I have written] in this scroll/book.
Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
22 “In the future, your descendants and people from other countries will see the disasters and the illnesses that Yahweh has caused to happen to you.
Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
23 They will see that all your land has been ruined by burning sulfur and salt. Nothing will have been planted. Not even weeds will grow there. Your land will resemble Sodom and Gomorrah [cities], and Admah and Zeboiim [cities], which Yahweh destroyed when he was very angry [DOU] [with the people who lived there].
na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
24 And the people from those other nations will ask, ‘Why did Yahweh do this to this land? Why was he very angry [with the people who lived here]?’
watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
25 “Then other people will reply, ‘It is because they refused to keep the agreement that Yahweh, the God whom their ancestors [worshiped], had made with them when he brought them out of Egypt.
Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
26 Instead, they served/worshiped other gods that they had never worshiped before, gods that Yahweh had told them not to worship.
na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
27 So, Yahweh became very angry with the Israeli people in this land, and he caused them to experience all the disasters that their leader warned them about.
Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
28 Yahweh became extremely angry [DOU] with them and took/yanked them [MET] out of their land and banished them into another land, and they are still there.’
Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
29 “[There are some] things that Yahweh our God has (kept secret/not revealed), but he has revealed his laws to us, and [he expects] us and our descendants to obey them forever.”
Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.

< Deuteronomy 29 >