< Amos 1 >

1 This is the message that [Yahweh] gave to [me], Amos. I am a (shepherd/man who takes care of sheep). I am from [near] Tekoa [town south of Jerusalem]. I received this message about Israel in a vision two years before the [big] earthquake. It was when Uzziah was the king of Judah, and Jeroboam, the son of [King] Jehoash, was the king of Israel.
Haya ni mambo yanayoihusu Israeli ambayo Amosi, mmoja wa wachungaji katika Tekoa, aliyapokea katika ufunuo. Alipokea haya mambo katika siku za Uzia mfalme wa Yuda, na pia katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la aridhi.
2 This is what Yahweh said: “I will roar [like a lion] [MET]; when I speak from Zion [Hill in] Jerusalem [DOU], my voice will [resemble the sound of] thunder. [When that happens], the pastures where you shepherds [take care of] your sheep will dry up, and [the grass] on top of Carmel [Mountain] will (wither/become brown) [because I will cause that no rain will fall].”
Alisema, “Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu. Malisho ya wachungaji yatanyamaza kimya; kilele cha Karmeli kitanyauka.”
3 This is [also] what Yahweh said [to me]: “[I will punish the people of] Damascus, [the capital of Syria, ] because of the many sins that they have committed; I will not [change my mind about punishing them] [MTY], because [the cruel things that they did to the people of the] Gilead [region] [were like] [MET] people threshing grain using sledges [that have (iron teeth/sharp iron nails) in them].
Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Damaskasi, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya chuma.
4 I will cause a fire to burn the palace [that King] Hazael [built and lived in], the fortress where [his son King] Ben-Hadad [also] lived.
Nitapeleka moto kwenye nyumba ya Hazaeli, na utaiteketeza ngome za Ben Hadadi.
5 I will cause the gates of Damascus to be broken [down]; I will get rid of the king who rules in Aven Valley and the one who rules in Beth Eden. And the people of Syria will be captured and taken to the Kir [region where they originally lived].”
Nitazivunja komeo za Damaskasi na kumkatilia mbali mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni, na pia yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni. Na watu wa shamu watakwenda utumwani hata Kiri,” asema Yahwe.
6 Yahweh [also] said this [to me]: “[I will punish the people of the cities in Philistia]: [I will punish the people of] Gaza [city] because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they captured large groups of people and took them to Edom and sold them to become the slaves of [the people of] Edom.
Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu waliwachukua mateka watu wote, kuwaweka juu ya mkono wa Edomu.
7 I will cause a fire to completely burn the walls of Gaza and [also] destroy its fortresses.
Nitatuma moto kwenye kuta za Gaza, na kuziteketeza ngome zake.
8 I will get rid of the king of Ashdod [city] and the king who rules [MTY] in Ashkelon [city]. I will [also] strike/punish [the people of] Ekron [city], and [all] the people of Philistia who are still alive will be killed.”
Nitamkatilia mbali yule mtu aishiye katika Ashdodi na mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, na mabaki ya Wafilisti wataangamia,” asema Bwana Yahwe.
9 Yahweh [also] said this [to me]: “[I will punish the people of] Tyre [city] because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they [also] captured large groups of our people and took them to Edom, disregarding the treaty of friendship that they had made [with your rulers].
Hivi ndivyo Yhawe asemavyo: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa nne, sintobadili adhabu, kwa sababu waliwapelekea watu wote wa Edomu, na wamevunja agano lao la undugu.
10 So I will cause a fire to completely burn the walls of Tyre and [also] destroy its fortresses.”
Nitapeleka moto kwenye kuta za Tiro, nao utaziteketeza ngome zake.”
11 Yahweh [also] said this [to me]: “I will punish [the people of] Edom because of the many sins that they have committed; I will not change my mind about punishing them, because they pursued the people [of Israel], who descended from Esau’s [brother Jacob, and killed them] with swords; they did not act mercifully toward them at all. They were extremely angry [with the people of Israel], and they continued to be angry [with them].
Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu alimfuatilia ndugu yake kwa upanga na kutupilia mbali huruma zote. Hasira yake ikaendelea kuwa kali, na ghadhabu yake ikabaki milele.
12 I will cause a fire to burn Teman [district in Edom] and completely burn the fortresses of Bozrah, [the biggest city in Edom].”
Nitapeleka moto juu ya Temani, na utaziteketeza nyumb a za kifalme za Bozra.”
13 Yahweh [also] said this [to me]: “I will punish [the people of] Ammon because of the many sins that [they] have committed; I will not change my mind about punishing them, because [their soldiers even] ripped open [the bellies of] pregnant women [when their army attacked] the Gilead [region] to gain more territory.
Hivi ndivyo Yahwe asemavyo, “Kwa dhambi tatu za watu wa Amoni, hata kwa nne, sintobadilisha adhabu, kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili waweze kupanua mipaka yao.
14 I will cause a fire to [completely] burn the walls around Rabbah [city] and completely burn its fortresses. During that battle, [their enemies] will shout loudly and the fighting will be [like] [MET] a fierce/raging wind/storm.
Nitawasha moto katika kuta za Raba, nao utaziteketeza nyumba za kifalme, pamoja na kupiga kelele katika siku ya vita, pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga.
15 [After the battle], the king [of Ammon] and his officials will be (exiled/forced to go to another country).”
Mfalme wao ataenda utumwani, yeye na maafisa wake pamoja,” asema Yahwe.

< Amos 1 >