< Acts 1 >

1 [Dear] Theophilus, In my first book [that I wrote for you], I wrote about many of the things that Jesus did and taught
Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2 until the day on which he was taken {[God] took him} up [to heaven]. Before [he went to heaven], saying what the Holy Spirit [told him], he told the apostles whom he had chosen [the things that he wanted them to know].
mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 After he had suffered [and died on the cross], [he became alive again]. As he appeared to them [often] during [the next] 40 days, the apostles saw him many times. He proved to them in many ways that he was alive again. He talked [with them] about [how] God would rule [MET] [the lives of people who accepted him as their king].
Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4 [One time] while he was with them, he told them, “Do not leave Jerusalem [yet]. Instead, wait [here] until my Father sends [his Spirit] [MTY] [to you], as he promised [to do]. You have heard me speak [to you] about that.
Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: “Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5 John baptized people in water [because they said that they wanted to change their lives], but after a few days [LIT] [God] will put the Holy Spirit within you(pl) [to truly change your lives].”
Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 One day when the [apostles] met together [with Jesus], they asked him, “Lord, will you [(sg)] now become the King [MET] over [us] Israelite people [like King David, who ruled long ago]?” (OR, “Lord, will you [(sg)] now [defeat the Romans and] restore the kingdom [to us] Israelite people?”)
Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, “Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?”
7 He replied to them, “You do not [need] to know the time [periods] and days [when that will happen]. My Father alone has decided [when he will make me king].
Lakini Yesu akawaambia, “Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8 But [you do need to know that] the Holy Spirit will make you [spiritually] strong when he comes to live in you. Then you will [powerfully] tell people about me in Jerusalem and in all [the other places in] Judea [district], in Samaria [district], and in places far away all over [IDM] the world.”
Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia.”
9 After he said that, he was taken {[God] took him} up [to heaven], while they were watching. [He went up into] a cloud [PRS], which prevented them from seeing him [any more].
Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10 While [the apostles] were [still] staring towards the sky as he was going up, suddenly two men who were wearing white clothes stood beside them. [They were angels].
Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11 One [of] them said, “You men from Galilee [district], (you do not need to stand [here any longer] looking up at the sky!/why do you still stand [here] looking up at the sky?) [RHQ] [Some day] this same Jesus, whom [God] took from you up to heaven, will come back [to earth]. He will return in the same manner as you [just now] saw him when he went up to heaven, [but he will not return now].”
wakasema, “Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni.”
12 Then [after the two angels left], the apostles returned to Jerusalem from Olive [Tree] Hill, which was about (a half mile/one kilometer) [MTY] from Jerusalem.
Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13 When they entered [the city], they went upstairs to the room [in the house] where they were staying. [Those who were there included] Peter, John, James, Andrew, Philip, Thomas, Bartholomew, Matthew, [another] James [the son] of Alphaeus, Simon who belonged to the group that wanted to expel the Romans, and Judas [the son] of [another man named] James.
Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 All these apostles agreed concerning the things about which they continually were praying [together. Others who prayed with them] included the women [who had accompanied Jesus], Mary who was Jesus’ mother, and his [younger] brothers.
Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15 During those days Peter stood up among his fellow believers. There were [at that place] a group of about 120 of [Jesus’ followers]. Peter said,
Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16 “My fellow believers, [there are words that King] David wrote [MTY] in the Scriptures long ago that needed to be fulfilled {to happen [as he said they would]}. The Holy Spirit, [who knew that Judas would be the one who would fulfill those words], told David what to write.
akasema, “Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17 [Although] Judas had been chosen {[Jesus] had chosen Judas}, along with [the rest of] us [(exc)] to serve [as an apostle], Judas was the person who led to Jesus the people who seized him.”
Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18 [The Jewish leaders] gave Judas money when he [promised to] treacherously/wickedly [betray Jesus. Later Judas returned that money to them]. When Judas [hanged himself], his body fell down [to the ground]. His abdomen burst open, and all his intestines spilled out. [So] the [Jewish leaders] bought a field [using] that money.
(“Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19 All the people who reside in Jerusalem heard [about that], so they called that field in their own [Aramaic] language, Akeldama, which means ‘Field of Blood’, [because it was where someone bled and died].
Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20 [Peter also said], “[I perceive that what happened to Judas is like what the writer of] Psalms [desired to happen]: ‘May his house become deserted, and may there be no one to live in it.’ (OR, ‘[Judge him, Lord, so that neither he nor] anyone [else] may live in his house!)’ And it seems that [these other words that David wrote also refer to Judas: ] ‘Let someone else take over his work as a leader.’”
Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21 “So it is necessary [for us apostles] to choose a man [to replace Judas. He must be one who] accompanied [MTY] us all the time when the Lord Jesus was with us.
Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22 [That would be] from [the time when] John [the Baptizer] baptized [Jesus] until the day when Jesus was taken {when [God] took Jesus} from us up [to heaven]. He must be one who saw Jesus alive again [after he died].”
Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni.”
23 So the [apostles and other believers] suggested [the names of two men who qualified. One man was] Joseph, who was called {whom people called} Barsabbas (OR, Joseph Barsabbas) who [also] had the [Roman] name Justus. The other man was Matthias.
Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24 Then they prayed like this: “Lord [Jesus], Judas stopped being an apostle. [He died and] went to the place where he [deserved to be] [EUP]. [So we(exc) need to choose someone] to replace [Judas in order] that he can serve [you(sg) by becoming] an apostle. You [(sg)] know what everyone is really like. So [please] show us which of these two men you have chosen.”
Kisha wakasali: “Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe.”
26 Then they cast lots [to choose between the two of] them, and the lot fell for Matthias. (OR, Then [one of] the [apostles] shook [in a container] small objects/stones [that] they [had marked to determine which man God had chosen]. And the small object/stone [that they had marked] for Matthias fell [out of the container]). So Matthias was considered {they considered Matthias} [to be an apostle] along with the [other] eleven apostles.
Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.

< Acts 1 >