< 2 Samuel 10 >

1 Some time later, the king of the Ammon people-group died, and his son Hanun became their king.
Ikawa baadaye mfalme wa watu wa Amoni akafa, na Hanuni mwanaye akawa mfalme mahali pake.
2 David thought, “Nahash was kind to me, so I will be kind to his son.” So David sent some officials there, to tell Hanun that David was sorry that Hanun’s father [had died]. When those messengers arrived in the land where the Ammon people-group lived,
Daudi akasema, “Nitaonesha fadhiri Hanuni mwana wa Nahashi, kwa kuwa baba yake alinifadhiri.” Hivyo Daudi akatuma watumishi wake kumfariji Hanuni kwa habari ya baba yake. Watumishi wake wakaingia katika nchi ya watu wa Amoni.
3 the leaders of the Ammon people-group said to Hanun, “Do you think that it is to honor your father that King David has sent these men to say that he is sorry that your father died [RHQ]? [We think that] he has sent them here to look around the city to determine how his [army] can conquer us!”
Lakini viongozi wa watu wa Amoni wakamwambia Hanuni bwana wao, “Je unathani kwa hakika Daudi anamweshimu baba yako hata ametuma watu kukutia moyo? Daudi hajawatuma watumishi wake kwako ili kuuangalia mji, kuupeleleza, ili kuupindua?
4 Hanun [believed what they said; so he commanded some soldiers to] seize David’s officials and [insult them by] shaving off one side of each man’s beard, and [by] cutting off the lower part of their robes, [with the result that their buttocks could be seen], and then they sent them away.
Hivyo Hanuni akawachukuwa watumishi wa Daudi, akawanyoa nusu ya ndevu zao, akachana mavazi yao hadi kwenye matako, naye akawaacha waende zao.
5 The men were very humiliated/ashamed, [so they did not want to return home]. When David found out about what had happened to his officials, he sent someone to tell them, “Stay at Jericho until your beards have grown again, and then return home.”
Daudi alipoelezwa kuhusu hili, akatuma watu kwenda kuwalaki, kwa kuwa walikuwa wamefedheheshwa sana. Mfalme akawambia, “Kaeni Yeriko mpaka ndevu zenu zitakapoota, ndipo mrudi.”
6 Then [the leaders of] the Ammon people-group realized that they had greatly insulted [IDM] David [IDM]. So they sent some men to hire/pay some soldiers [from other nearby areas to help defend them]. They hired 20,000 soldiers from [the] Beth-Rehob and Zobah [regions northeast of Israel], and 12,000 soldiers from [the] Tob [region], and 1,000 soldiers from [the army of] the king of Maacah [region].
Watu wa Amoni walipoona kwamba wamenuka kwa Daudi, wakatuma wajumbe na kuwaajiri Washami wa Bethi Rehobu na Soba, askari elfu ishirini waendao kwa mguu, na mfalme wa Maaka pamoja na watu elfu, na watu wa Tobu elfu kumi na mbili.
7 When David heard about that, he sent Joab with all of the army [that Joab commanded], to fight against them.
Daudi aliposikia, akamtuma Yoabu na jeshi lote la askari.
8 The soldiers of the Ammon people-group marched out and (stood in their positions/arranged themselves for battle) at the entrance [to their capital city, Rabbah]. The other soldiers from Syria and Tob and Maacah stood by themselves (in their positions/arranged themselves for battle) in the nearby fields.
Waamoni wakatoka na wakafanya mistari ya vita katika maingilio ya lango la mji wao, wakati Washami wa Soba na wale wa Rehobu, na watu wa Tobu na Maaka, wakasimama peke yao uwandani.
9 Joab saw that there were groups of enemy soldiers in front of his troops and behind his troops. So he chose some of the best Israeli soldiers, and put them in positions to fight against the soldiers of Syria.
Yoabu alipoona mistari ya vita ikimkabili pote mbele na nyuma, alichagua baadhi ya waisraeli wajuao kupigana vizuri na akawapanga dhidi ya Washami.
10 He appointed his [older] brother Abishai to be the commander of all the other soldiers, and he told them to (stand in their positions/arrange themselves) in front of [the army of] the Ammon people-group.
Na sehemu iliyosalia ya jeshi, akawaweka chini ya Abishai nduguye, naye akawaweka katika mistari ya vita dhidi ya jeshi la Amoni.
11 Then Joab said, “If the soldiers from Syria are too strong for us to defeat them, your men must come and help us. But if the soldiers from the Ammon people-group are too strong for you to defeat, we will come and help your men.
Yoabu akasema, “ikiwa Washami watakuwa na nguvu zaidi juu yangu, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe. Lakini ikiwa jeshi la Amoni litakuwa na nguvu zaidi juu yako, nitakuja kukuokoa.
12 We must be strong, and fight hard [IDM] to [defend] our people and the cities [(that belong to/where we worship)] our God. I will pray/request that Yahweh do what he considers to be good.”
Iweni na nguvu, nasi tujioneshe kuwa wenye nguvu kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu, kwa maana Yahwe atatenda yapendezayo kwa ajili ya kusudi lake.
13 So Joab and his army [advanced to] attack the army of Syria, and the soldiers from Syria ran away from them.
Hivyo Yoabu na askari wa jeshi lake wakasonga mbele katika vita dhidi ya Washami, waliolazimika kukimbia mbele ya jeshi la Israeli.
14 And when [the soldiers of] the Ammon people-group saw that the soldiers from Syria were running away, they also started to run away from Abishai and his army, and they retreated back inside the city. So Joab’s [army] stopped fighting against [the army of] the Ammon people-group, and Joab [and his army] returned to Jerusalem.
Jeshi la Amoni lilipoona kwamba Washami wamekimbia, nao pia wakakimbia kutoka kwa Abishai wakarudi ndani ya mji. Ndipo Yoabu akarudi kutoka kwa watu wa Amoni na akarejea Yerusalemu.
15 After [the leaders of] the army of Syria saw that the Israeli army had defeated them, they gathered all their troops together.
Washami walipoona kwamba wameshindwa na Israeli, walijikusanya pamoja tena.
16 [Their king, ] Hadadezer, summoned the soldiers of Syria who lived on the east side of the [Euphrates] River. They gathered at Helam [city]. Their commander was Shobach.
Kisha Hadareza akatuma kuleta vikosi vya Washami ng'ambo ya Mto Frati. Wakaja Helamu pamoja na Shobaki, mkuu wa jeshi la Hadareza juu yao.
17 When David heard about that, he gathered all the Israeli soldiers, and they crossed the Jordan [River] and marched to Helam. There, the army of Syria (took their positions/arranged themselves for battle), and the battle started.
Daudi alipoambiwa, aliwakusanya Israeli wote pamoja, akavuka Yordani, na akafika Helamu. Washami wakajipanga katika mistari ya vita dhidi ya Daudi na wakapigana naye.
18 But the soldiers of Syria ran away from the Israeli soldiers. David [and his army] killed 700 of their chariot-drivers and 40,000 other soldiers. They also wounded Shobach, their commander, and he died there.
Washami wakakimbia mbele ya Israeli. Daudi akaua askari mia saba wa magari na askari wa farasi elfu arobaini. Shobaki mkuu wa jeshi lao alijeruhiwa na akafa huko.
19 When all the kings who had been ruled by Hadadezer realized that they had been defeated by the Israeli [army], they made peace with the Israelis and agreed to accept David as their king. So [the army of] Syria was afraid to help [the army of] the Ammon people-group any more.
Wafalme wote waliokuwa watumishi wa Hadareza walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, walifanya amani na Israeli na wakawa watumishi wao. Hivyo washami wakaogopa kuwasaidia watu wa Amoni tena.

< 2 Samuel 10 >