< 2 Kings 23 >

1 Then the king summoned all the elders of Jerusalem and [of the other places in] Judah.
Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
2 They went together to the temple, along with the priests and the prophets, and many other [HYP] people, from the most important people to the least important people. And while they listened, the king read to them all of the laws that Moses had written. He read from the scroll that had been found in the temple.
Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
3 Then the king stood next to the pillar [where the kings stood when they made important announcements], and while Yahweh was listening, he repeated his promise to sincerely obey [DOU] all of Yahweh’s commands and regulations [DOU]. He also promised to (fulfill the conditions of/do what was written in) the agreement he made with Yahweh. And all the people also promised to obey the agreement.
Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
4 Then the king commanded Hilkiah the Supreme Priest and all the other priests who assisted him and the men who guarded the entrance to the temple to bring out from the temple all the items that people had been using to worship Baal, the goddess Asherah, and the stars. [After they carried them out, ] they burned all those things outside the city near the Kidron Valley. Then they took all the ashes to Bethel, [because that city was already considered to be desecrated/unholy].
Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
5 There were many pagan priests that the previous kings of Judah had appointed to burn incense on the altars on the tops of hills in Judah. They had been offering sacrifices to Baal, to the sun, the moon, the planets, and the stars. The king stopped them from doing those things.
Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
6 He [commanded that] the statue of the goddess Asherah [be] taken out of the temple. Then they took it outside Jerusalem, down to the Kidron Brook, and burned it. Then they pounded the ashes to powder and scattered that over the graves in the public cemetery.
Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
7 He also destroyed the rooms in the temple where the temple male prostitutes lived. That was where women wove robes that were used to worship the goddess Asherah.
Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
8 Josiah also brought [to Jerusalem] all the priests who were offering sacrifices in the other cities in Judah. He also desecrated the places on the tops of hills where the priests had burned incense [to honor idols], from Geba [in the north] to Beersheba [in the south]. Those priests were not allowed to offer sacrifices in the temple, but they [were allowed to] eat the unleavened bread that the priests [who worked in the temple] ate. He also [commanded that] the altars that were dedicated to the goat demons near the gate built by Joshua, the mayor of Jerusalem, [be] destroyed. Those altars were at the left of the main gate into the city.
Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
9
Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 Josiah also desecrated the place named Topheth, in the Hinnom Valley, in order that no one could offer his son or daughter there to be completely burned for a sacrifice to [the god] Molech.
Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
11 He also removed the horses that the [previous] kings of Judah had dedicated to worshiping the sun, and he burned the chariots that were used in that worship. Those horses and chariots were kept in the courtyard outside the temple, near the entrance to the temple, and near the room where [one of Josiah’s] officials, whose name was Nathan-Melech, lived.
Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
12 Josiah also commanded his servants to tear down the altars that the previous kings of Judah had built on the roof of the palace, above the room where King Ahaz had stayed. They also tore down the altars that had been built by King Manasseh in the two courtyards outside the temple. He commanded that they be smashed to pieces and thrown down into the Kidron Valley.
Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
13 He also commanded that the altars that King Solomon had built east of Jerusalem, south of Olive Tree Hill, be desecrated. Solomon had built them for the worship of the disgusting idols—the [statue of the goddess] Astarte [worshiped by the people in] Sidon [city], Chemosh the god of the Moab people-group, and Molech the god of the Ammon people-group.
Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
14 They also broke into pieces the stone pillars that the Israeli people worshiped, and cut down the [pillars that honored the goddess] Asherah, and they scattered the ground there with human bones [to desecrate it].
Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
15 Furthermore, he commanded them to tear down the place of worship at Bethel which had been built by King Jeroboam, the king who persuaded the people of Israel to sin. They tore down the altar. Then they broke its stones into pieces and pounded them to become powder. They also burned the statue [of the goddess] Asherah.
Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
16 Then Josiah looked around and saw some tombs there on the hill. He commanded his men to take the bones out of those tombs and burn them on the altar. By doing that, he desecrated the altar. That was what a prophet had predicted many years before when Jeroboam was standing close to that altar at a festival. Then Josiah looked up and saw the tomb of the prophet who had predicted that.
Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
17 Josiah asked, “Whose tomb is that?” The people of Bethel replied, “It is the tomb of the prophet who came from Judah and predicted that these things that you have just now done to this altar would happen.”
Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
18 Josiah replied, “Allow his tomb to remain as it is. Do not remove the prophet’s bones from the tomb.” So the people did not remove those bones, or the bones of the other prophet, the one who had come from Samaria.
Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
19 In every city in Israel, at Josiah’s command, they tore down the shrines that had been built by the previous kings of Israel, which had caused Yahweh to become very angry. He did to all those shrines/altars the same thing that he had done to the altars at Bethel.
Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
20 He ordered that all the priests who offered sacrifices on the altars on the tops of hills must be killed on those altars. Then he burned human bones on every one of those altars [to desecrate them]. Then he returned to Jerusalem.
Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 Then the king commanded all the people to celebrate the Passover Festival to honor Yahweh their God, which was written in the law of Moses that they should do [every year].
Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
22 During all the years that leaders ruled Israel and during all the years that kings had ruled Israel and Judah, they had not celebrated that festival.
Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
23 But now, after Josiah had been ruling for almost 18 years, to [honor] Yahweh they celebrated the Passover Festival in Jerusalem.
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
24 Furthermore, Josiah got rid of all the people in Jerusalem and other places in Judah who practiced sorcery and those who requested the spirits of dead people [to tell them what they should do]. He also removed from Jerusalem and from the other places in Judah all the household idols and all the other idols and abominable things. He did those things in order to obey what had been written in the scroll that Hilkiah had found in the temple.
Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
25 Josiah was totally devoted to Yahweh. There had never been [in Judah or Israel] a king like him. He obeyed all the laws of Moses. And there has never since then been a king like Josiah.
Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
26 But Yahweh had become extremely angry with the people of Judah because of all the things that [King] Manasseh had done to infuriate him, and he continued to be very angry.
Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
27 He said, “I will do to Judah what I have done to Israel. I will banish the people of Judah, with the result that they will never enter my presence again. And I will reject Jerusalem, the city that I chose [to belong to me], and I will abandon the temple, the place where I said that I [MTY] should be worshiped.”
Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
28 [If you want to know more about] [RHQ] all the other things that Josiah did, they are written in the scroll called ‘The History of the Kings of Judah’.
Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
29 While Josiah was the king of Judah, King Neco of Egypt led his army north to the Euphrates River to help the king of Assyria. King Josiah tried to stop the army of Egypt at Megiddo [city], but Josiah was killed in a battle there.
Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
30 His officials placed his corpse in a chariot and took it back to Jerusalem, where it was buried in his own tomb, a tomb where the other previous kings had not been buried. Then the people of Judah poured [olive] oil on [the head of] Josiah’s son Joahaz, to appoint him to be the new king.
Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
31 Joahaz was 23 years old when he became the king [of Judah], but he ruled from Jerusalem for [only] three months. His mother was Hamutal, the daughter of Jeremiah from Libnah [city].
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
32 Joahaz did many things that Yahweh said were evil, just like many of his ancestors had done.
Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
33 King Neco’s [army came from Egypt and captured him and] tied him up with chains and took him as a prisoner to Riblah [town] in Hamath [district], to prevent him from continuing to rule in Jerusalem. Neco forced the people of Judah to pay to him (7,500 pounds/3,400 kg.) of silver and (75 pounds/34 kg.) of gold.
Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
34 King Neco appointed another son of Josiah, Eliakim, to be the new king, and he changed Eliakim’s name to Jehoiakim. Then he took Joahaz to Egypt, and later Joahaz died there in Egypt.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
35 King Jehoiakim collected a tax from the people [of Judah]. He collected more from the rich people and less from the poor people. He collected silver and gold from them, in order to pay to the king of Egypt what he commanded them to give.
Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
36 Jehoiakim was twenty-five years old when he became the king [of Judah], and he ruled from Jerusalem for eleven years. His mother was Zebidah, the daughter of Pedaiah from Rumah [town].
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
37 He did many things that Yahweh says are evil, like his ancestors had done.
Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.

< 2 Kings 23 >