< 2 Corinthians 5 >

1 We know that [these bodies] we live in [here in this world are like] [MET] tents. [They are like temporary living/dwelling places]. [So we should not be concerned about what happens to our bodies]. We know that if we are killed {if [someone] kills us}, God will give us [permanent living places. Those permanent living places] [MET] will not be houses that people have made. They [will be new bodies in which we will live forever] in heaven. (aiōnios g166)
Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono. (aiōnios g166)
2 [While we are here on earth, we suffer]. We often groan because we desire [to go] to heaven [where God] will give us our new [bodies] [MET].
Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
3 When [God gives us(inc) our new bodies] [MET], our [spirits will have] [LIT, MET] bodies to live in [that will last forever].
Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
4 [It is true that] while we are still living in these bodies [MET] [that do not last forever], we often groan [DOU] [because we desire to be free from them]. We are not longing to be without a body. Instead, [we groan because] we desire to receive our new bodies [MET] in heaven. We long for this to happen so that these bodies that are going to die some day will suddenly be changed [into bodies] that will live [forever].
Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
5 It is God himself who has prepared us to [receive] these [new bodies]. He is also the one who has guaranteed/assured us [(inc)] that this will happen. He has guaranteed it by sending his Spirit [to live inside us now].
Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
6 So, [because God’s Spirit lives in us], we are always confident [that God will give us new bodies]. We know that as long as we have bodies here on [earth], we are not yet [living together] with the Lord [Jesus in heaven].
Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
7 While we [(exc)] live [here, we] do not have our [new bodies, but we are] trusting [that God will give them to us].
Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
8 [As I said], we [(exc)] are confident [that he will give us new bodies]. We [(exc)] would much prefer to leave these bodies [which we have now], and be with the Lord [Jesus in our] home in [heaven].
Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
9 Because of all that, we always want to please [Jesus in everything that we do]. Whether we [(exc)] are [still living] here [in these] bodies or whether we have [left] them and are living in our home [in heaven], we want to please him.
Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
10 [And we need to try hard to do that] because each one of us [believers] must stand before Christ [to be] judged [by him] {[when he will] judge [his people]}. [At that time] he will [reward each one of] us according to what we have done [while we lived in this world] in these bodies. [He will reward us according to] whether we have done good things or whether we have done evil things.
Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
11 It makes me fearful [to think that some day I will stand before the Lord for him to judge me]. So I [do everything that I can to] convince people [that they should believe] (OR, [that I teach] sincerely) [God’s message]. God knows very well [how I conduct my life and what I teach], and I really believe that you know it, too.
Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
12 Once again [I say, as I write this], I am not just [trying to] make you think well/highly of me, [as some people will probably say that I am]. Instead, I am [telling you in this letter why you have] good reason [to tell those who criticize me] that you think highly of me. [I am telling you this] so that you will know what to say to those [teachers of false doctrine among you]. They are proud [of what they have done], instead of [making sure that] they [are right with God and being pleased with that].
Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
13 [Some of them say that after God has enabled me to see visions], I [talk like] a crazy person. If [that is so, I want you to realize that I talk that way in order to please] God. On the other hand, if [you think that] I [speak and act] wisely, [that is good. I want you to know that I do] speak and act wisely in order to [help] you.
Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
14 [I speak and act the way I do] because the love that Christ [has for people] influences me [in everything that I say and do]. When Christ died, [he suffered the punishment] for [the sins of] all people. So, we should all [think of ourselves as having] died with him, [being as unresponsive to sinful desires as] [MET] a corpse is.
Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
15 When [Christ] died for the everyone, he died in order that [we believers who are alive now] should not conduct our lives in a way that will just [please ourselves]. Instead, [we should conduct our lives in a way that will please] Christ, [because] he is the one who died for us and was brought back to life {whom [God] raised} again.
Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
16 So, [because I realize how much Christ loves everyone], I no longer think about people in the way that those who do not believe [in Christ] think about [them]. Before I [was a believer], I thought about Christ in the way that other non-believers did. But I do not think of him that way any more.
Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
17 The fact is that God makes every one [of us] who [trusts] in Christ to be completely different [than we were before]. Our old [way of conducting our lives] is gone. We now have a [completely] new way of [conducting our lives].
Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
18 This [complete change in our lives] is all something that God [does]. It is God who made it possible for us to have a peaceful relationship with him. [He was able to do that] because of what Christ [did for us]. Now God [has sent] me, and those [who work] with me, to tell [people that they] can have a peaceful relationship with him.
Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
19 That is, [he sent us(exc) to tell them that] when Christ [died], God was [making it possible for everyone] [MTY] in the world to have a peaceful relationship with him. He no longer keeps a record of the sinful things that [we believers] have done. The message that [God] has given to us [to tell people is how we can have a] peaceful relationship with him.
Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
20 So, it is I and my companions who are Christ’s representatives [in this world. When we tell people the message about Christ], it is God himself who is pleading with them by means of what we [say]. So, as true representatives of Christ, we plead with you: [Believe God’s true message about Christ in order that you may] be reconciled to {have a peaceful relationship with} him.
Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
21 [You must believe that even though] Jesus never sinned, God [punished him for all the] sinful things [that people do, just] as [if Jesus had done those sinful things himself]. And because of our close relationship with Christ, God has erased the record of our sins/declared us no longer guilty for our sins.
Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.

< 2 Corinthians 5 >