< 2 Chronicles 8 >

1 Solomon’s [workers] worked for 20 years to build the temple and the king’s palace.
Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
2 Then his [workers] rebuilt the cities that [King] Hiram had given back to Solomon, and Solomon sent Israelis to live in those cities.
Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
3 Solomon’s [army] then went to Hamath-Zobah [town] and captured it.
Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
4 His workers also rebuilt walls around Tadmor [town] in the desert, and in [the] Hamath [region] in all the towns where they kept supplies.
Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
5 They rebuilt Upper Beth-Horon [town] and Lower Beth-Horon [city], and built walls around them with gates [in the walls] and bars [to fasten the gates].
Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
6 They also rebuilt Baalath [town] and all the cities where supplies were kept and the cities where Solomon’s chariots and horses were kept. Solomon’s [workers] built whatever he wanted them to build, in Jerusalem and in Lebanon, and in other places in the area that he ruled.
Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
7 Solomon forced people from many other groups who were not Israelis to work for him like slaves. They were people from the Heth, Amor, Periz, Hiv, and Jebus people-groups.
Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
8 They were descendants of groups whom the Israelis had not completely destroyed. Solomon forced them to become his slaves, and they are still slaves.
yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
9 But Solomon did not force Israelis to work for him. Israelis became his soldiers and commanders of his chariots and his chariot-drivers.
Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
10 They were also King Solomon’s chief officials. There were 250 of them, and they supervised the workers.
Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
11 Solomon moved his wife, who was the daughter of the king of Egypt, from [the place outside Jerusalem called] ‘The City of David’ to the place that his workers had built for her. He said, “I do not want my wife to live in the palace that [my father] King David’s workers built, because the Sacred Chest [was in that palace for a while], and any place where the Sacred Chest has been is holy.”
Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
12 On the altar that Solomon’s [workers] had built in front of the entrance [to the temple], Solomon sacrificed many offerings that were to be completely burned.
Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
13 He did that to obey the rules about what sacrifices Moses had declared should be made. These included sacrifices for every day and for the Sabbath days and to celebrate each day on which there was a new moon and for the three other festivals that were celebrated each year. Those festivals were the Festival of Eating Unleavened Bread, the Harvest Festival, and the Festival of Living in Temporary Shelters.
kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
14 Obeying what his father David had commanded, he appointed the groups of priests for their work, and he appointed the descendants of Levi to lead the people while they sang to praise Yahweh and while they assisted the priests in their daily work. He also appointed groups of them to guard all the gates, because that was also what David, the man who pleased God [very well], had commanded.
Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
15 The priests and other descendants of Levi obeyed completely everything that the king commanded, including [taking care of] the storerooms.
Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
16 They did all the work [of building the temple] that Solomon told them to do, until it was all completed. So they finishing building the temple.
Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
17 Then some of Solomon’s men went to Ezion-Geber and Elath [cities] on the coast of the Red Sea, an area that belonged to the Edom people-group.
Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
18 King Hiram sent to Solomon from [Tyre city] some ships that were commanded by his officers. They were men who were experienced sailors. These men went in the ships with Solomon’s men to [the] Ophir [region] and brought back about 17 tons of gold, which they delivered to King Solomon.
Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.

< 2 Chronicles 8 >