< 2 Chronicles 25 >

1 Amaziah was 25 years old when he became the king [of Judah], and he ruled from Jerusalem for 29 years. His mother was Jehoaddin; she was from Jerusalem.
Amazia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani kutoka Yerusalemu.
2 Amaziah did many things that pleased Yahweh, but he did not do them enthusiastically.
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, lakini sio kwa moyo wake wote.
3 As soon as he was in complete control of his kingdom, he caused to be executed the officials who had murdered his father.
Baada ya ufalme kuimarika mikononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
4 But he did not command their sons to be executed; he obeyed what was in the laws that Moses had written. In those laws Yahweh had commanded, “People must not be executed because of [what] their children [have done], and children must not be executed for [what] their parents [have done]. People must be executed only for the sins that they themselves have committed.”
Hata hivyo hakuwaua watoto wao, lakini akafanya sawasawa na ilivyoandikwa katika Sheria, katika Kitabu cha Mose, ambako Bwana aliamuru: “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
5 Amaziah summoned the men of [the tribes of] Judah and Benjamin to come to Jerusalem, and there he put them in groups, each clan in a group by themselves. Then he appointed officers to command each group. Some officers commanded 100 men and some commanded 1,000 men. They counted the men who were at least 20 years old; altogether there were 300,000 men. They were all men who were prepared to be in the army, and able to [fight well, ] using spears and shields.
Amazia akawaita watu wa Yuda pamoja, akawaweka chini ya majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia kufuatana na jamaa zao katika Yuda yote na Benyamini. Kisha akawahesabu wale wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na akakuta kwamba walikuwa wanaume 300,000 watu walio tayari kwa utumishi wa jeshi, walio na uwezo wa kutumia mkuki na ngao.
6 Amaziah also hired 100,000 capable soldiers from Israel and paid almost four tons of silver for them.
Akawaajiri pia watu 100,000 wapiganaji kutoka Israeli kwa talanta 100 za fedha.
7 But a prophet came to him and said, “Your majesty, you must not allow those soldiers from Israel to march with your soldiers, because Yahweh does not help the people of the tribe of Ephraim or from [anywhere else in] Israel.
Lakini mtu wa Mungu akamjia na kumwambia, “Ee mfalme, haya majeshi kutoka Israeli kamwe usiyaruhusu yaende pamoja na wewe kwa kuwa Bwana hayuko pamoja na Israeli, wala hayupo pamoja na yeyote wa watu wa Efraimu.
8 Even if your soldiers go and fight courageously in battles, God will cause your enemies to defeat you; do not forget that God has the power to help armies or to cause them to be defeated.”
Hata kama ukienda na kupigana kwa ujasiri katika vita, Mungu atakufanya ukimbie mbele ya adui, kwa kuwa Mungu anao uwezo wa kusaidia au wa kuangusha.”
9 Amaziah asked that prophet, “If I do that, what about the huge amount of silver that I paid to hire those soldiers from Israel?” The prophet replied, “Yahweh is able to pay you back more money than you paid [to hire those soldiers].”
Amazia akamuuliza yule mtu wa Mungu, “Lakini itakuwaje kwa zile talanta 100 za fedha nilizolipa kwa ajili ya haya majeshi ya Israeli?” Yule mtu wa Mungu akajibu, “Bwana aweza kukupa zaidi sana ya hizo.”
10 So Amaziah told those soldiers from Israel to return home. They left to go home, but they were very angry with the king of Judah [for not allowing them to stay and fight].
Hivyo Amazia akayaondoa yale majeshi yaliyokuwa yamekuja kutoka Efraimu na kuyarudisha nyumbani. Waliwakasirikia sana Yuda, nao wakarudi nyumbani wakiwa na hasira kali.
11 Then Amaziah became brave, and he led his army to the Salt Valley. There they killed 10,000 men from the Edom people-group.
Ndipo Amazia akajitia nguvu na kuliongoza jeshi lake kwenye Bonde la Chumvi, ambako aliua watu 10,000 wa Seiri.
12 The army of Judah also captured 10,000 others, and took them to the top of a cliff and threw them all down over the cliff, with the result that their corpses were all smashed to pieces.
Jeshi la Yuda pia likawateka watu 10,000 wakiwa hai, likawapandisha juu ya jabali na kuwatupa chini kwa nguvu hata wote wakavunjika vipande vipande.
13 While that was happening, the soldiers from Israel whom Amaziah had sent home after not allowing them to fight along with his soldiers, raided cities and towns in Judea, from Samaria [city] to Beth-Horon [town]. They killed 3,000 people and took away a great amount of valuable things.
Wakati huo yale majeshi Amazia aliyoyarudisha na ambayo hakuyaruhusu kushiriki katika vita, yalivamia miji ya Yuda kuanzia Samaria hata Beth-Horoni. Yakawaua watu 3,000 na kuchukua kiasi kikubwa sana cha mateka.
14 When Amaziah returned [to Jerusalem] after his army had slaughtered the soldiers from Edom, he brought the idols that were worshiped by the people of Edom. He set them up to be his own gods. Then he bowed down to [worship] them and offered sacrifices to them.
Amazia aliporudi kutoka kuwachinja Waedomu, alileta pia kutoka huko miungu ya watu wa Seiri. Akaisimamisha kama miungu yake mwenyewe, akaisujudia na kuitolea kafara za kuteketezwa.
15 Because of that, Yahweh was very angry with Amaziah. He sent a prophet to him, who said, “Why do you worship these foreign gods that were not even able to save their own people when your army attacked them?”
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Amazia, naye akamtuma nabii kwake, ambaye alisema: “Kwa nini unauliza kwa miungu ya hawa watu, ambayo haikuweza kuwaokoa watu wake wenyewe kutoka mkononi mwako?”
16 While he was still speaking, the king said to him, “We certainly did not appoint you to be one of my advisors. So stop [talking]! If you say anything more, [I will tell my soldiers to] kill you!” So the prophet said, “I know that God has determined to get rid of you, because you have [begun to] worship idols, and have not heeded my advice.” Then the prophet said nothing more.
Wakati nabii alipokuwa angali anazungumza, mfalme akamwambia, “Je, wewe tumekuchagua kuwa mshauri wa mfalme? Nyamaza, ya nini uuawe?” Hivyo nabii akanyamaza lakini akasema, “Najua kuwa Mungu ameazimia kukuangamiza kwa sababu umefanya jambo hili na hukusikiliza shauri langu.”
17 Some time later Amaziah, the king of Judah, consulted his advisors. Then he sent a message to Jehoash, the king of Israel. He wrote, “Come here and let’s talk together.”
Baada ya Amazia mfalme wa Yuda kushauriana na washauri wake akatuma ujumbe kwa Yehoashi, mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli kusema: “Njoo tukabiliane uso kwa uso.”
18 But Jehoash replied to King Amaziah, “One time a thistle growing [in the mountains] in Lebanon sent a message to a cedar tree saying, ‘Let your daughter marry my son.’ But a wild animal in Lebanon came along and trampled the thistle under its feet.
Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda, “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
19 [The meaning of what I am saying is that] you are saying to yourself that your army has defeated the army of Edom, so you have become very proud. But you should stay at your home. It would not be good for you to cause trouble, which would result in you and your kingdom of Judah being destroyed.”
Wewe unasema moyoni mwako kwamba umemshinda Edomu, nawe sasa unajigamba na kujivuna. Lakini kaa nyumbani kwako! Kwa nini utafute matatizo na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
20 But Amaziah refused to heed Jehoash’s message. That happened because God wanted Jehoash’s army to defeat them, because they were worshiping the gods of Edom.
Hata hivyo, Amazia hakutaka kusikia, kwa kuwa Mungu alifanya hivyo ili awatie mikononi mwa Yehoashi, kwa sababu waliitafuta miungu ya Edomu.
21 So Jehoash’s army attacked. Their two armies faced each other at Beth-Shemesh [city] in Judah.
Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akakwea kuwashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakabiliana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
22 The army of Judah was badly defeated by the army of Israel, and all the soldiers of Judah fled to their homes.
Yuda ikashindwa na Israeli na kila mtu akakimbilia nyumbani kwake.
23 King Jehoash’s army also captured King Amaziah there. Then he brought Amaziah to Jerusalem, and his soldiers tore down the wall [that was around the city], from the Ephraim Gate to the Corner Gate. That was a section that was about 600 feet long.
Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akamleta Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa 400.
24 His soldiers also carried away the gold and silver and other valuable furnishings from the temple which the descendants of Obed-Edom had previously been guarding. They also took away the valuable things in the palace, and they took to Samaria some prisoners whom they had captured.
Akachukua dhahabu yote, fedha na vyombo vyote vilivyopatikana katika Hekalu la Mungu, ambavyo vilikuwa chini ya uangalizi wa Obed-Edomu, pamoja na hazina za jumba la mfalme na mateka, kisha akarudi Samaria.
25 King Jehoash of Israel died, and King Amaziah of Judah lived for 15 years after that.
Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na mitano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
26 An account of all the other things that Amaziah did while he was the king [of Judah] is written in the scroll called ‘The History of the Kings of Judah and Israel’.
Kwa habari ya matukio mengine katika utawala wa Amazia, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kitabu cha wafalme wa Yuda na wa Israeli?
27 From the time that Amaziah started to disobey Yahweh, some men in Jerusalem planned to kill him. He was able to escape to Lachish [city], but those who wanted to kill him sent another group of people to Lachish and killed him there.
Kuanzia wakati ule Amazia alipogeuka na kuacha kumfuata Bwana walifanya shauri baya dhidi yake huko Yerusalemu naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi nao wakamuulia huko.
28 They put his corpse on a horse and brought it back to Jerusalem and buried it where his ancestors [had been buried] in the part of Jerusalem called ‘The City of David’.
Akarudishwa kwa farasi na akazikwa pamoja na baba zake katika Mji wa Yuda.

< 2 Chronicles 25 >