< 1 Samuel 2 >

1 Then Hannah prayed, saying, “I rejoice in [what] you, [, have done]. I am strong [MET] because I belong to you. I (laugh at/ridicule) my enemies, because you, Yahweh have rescued me [from being taunted by them].
Hana aliomba akasema, “moyo wangu wamtukuza BWANA. Pembe yangu imejulikana katika BWANA. Kinywa changu kinatamba dhidi ya maadui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There is no one who is holy like you, Yahweh. There is no other god like you. There is no one like you, our God, who can protect us [as though you were putting us beneath] a huge rock [where we can hide from danger].
Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA, kwa kuwa hakuna mwingine zaidi yako; hakuna mwamba kama Mungu wetu.
3 [You people who oppose God], stop boasting! Yahweh is a God who knows [everything], and he will evaluate/judge everyone’s actions. So don’t speak so arrogantly!
Msijivune sana hivyo kwa kiburi; vinywa vyenu visitoke majivuno. Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa; yeye huyapima matendo kwa mizani.
4 Yahweh, you break the bows/weapons of mighty soldiers, and you give strength to those who stumble [because of being weak].
Pinde za mashujaa zimevunjika, bali wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi.
5 Many people who previously had plenty to eat, now have to work for other people [to earn money] to buy food, but many who were always hungry are not hungry any more. The woman who did not have any children before, now has given birth to many/seven children, and the woman who had many children before, now is very lonely [because they have all died].
Wale walio na shibe ya kutosha wamejikodisha ili wapate chakula; wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Hata yule aliye kuwa tasa amezaa watoto saba, bali mwanamke mwenye watoto wengi amenyong'onyea.
6 Yahweh, you cause some people to die, and you restore some people who are almost dead. For some people, [it seems that they will soon] go to where the dead people are, but you cause them to become healthy again. (Sheol h7585)
BWANA huua na huuisha. Hushusha kuzimu na huleta tena juu. (Sheol h7585)
7 Yahweh, you cause some people to be poor and you cause some people to be rich, you humble some people and you honor some people.
BWANA humfanya maskini, na yeye ndiye humtajirisha mtu. Yeye hudhili, lakini pia hukweza
8 [Sometimes] you lift poor people up so that they are no longer [despondent, sitting in the dust, ] or sitting on heaps of ashes; you cause them to sit next to princes; you cause them to sit on chairs/thrones where people who are highly honored sit. Yahweh, you are the one who laid the foundations of the earth, and you have set the whole world on those foundations.
Yeye humwinua juu maskini toka mavumbini: Huwainua wahitaji toka jalalani na kuwaketisha pamoja na wakuu na kuwarithisha kiti cha enzi cha utukufu. Kwa kuwa nguzo za dunia ni za BWANA na ameukalisha ulimwengu juu yake.
9 You will protect your loyal/faithful people [SYN], but you will cause the wicked to die [EUP] and descend to the dark [place where dead people are]. We do not defeat [our enemies] by our own strength;
Yeye atazilinda nyayo za watu wake waaminifu, bali waovu watanyamazishwa gizani, kwa maana hakuna atayeshinda kwa nguvu zake.
10 Yahweh, you will break into pieces those who oppose you. You will cause thunder in the sky to show that you (oppose/are angry with) them. Yahweh, you will judge [people everywhere, even those who live in] the most remote places on the earth. You will give strength to the king whom you will appoint, and give him great power [over his enemies].”
Wale wampingao BWANA watavunjwa vipande vipande; atawapiga radi kutokea mbinguni. BWANA atahukumu miisho ya dunia; atampa nguvu mfalme wake na kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake.”
11 Then Elkanah [and his family] returned to Ramah, but Samuel, the little boy, stayed to help Eli the priest serve Yahweh.
Nndipo Elikana akenda Rama, nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia BWANA machoni pa Eli, kuhani.
12 Eli’s two [, who were also priests, ] were very wicked. They did not revere (OR, respect/obey) Yahweh.
Basi, watoto wa Eli walikuwa wakorofi. Wao hawakumheshimu BWANA.
13 While the people were boiling the meat from their sacrifices [in the huge pot at the temple], one of Eli’s sons, [would send his servant to come with a large three-pronged fork in his hand].
Desturi ya makuhani na watu ilikuwa kwamba endapo mtu yeyote ametoa dhabihu, mtumishi wa kuhani angekuja akiwa na uma wa meno matatu mkononi mwake, nyama ilipokuwa inatokoswa.
14 [He] would stick the fork into [the meat in] the pot, and whatever meat fastened onto the fork, he would take [and give it] to the priest who sent him. Eli’s sons did this to all the Israeli people who came to Shiloh [to offer sacrifices].
Naye angeutia uma huo sufuriani, au birikani au chomboni au chunguni; nyama yote ambayo ingeinuliwa na uma huo ingetwaliwa na kuhani mwenyewe. Ndivyo walivyofanya huko Shilo kwa Waisraeli wote waliokwenda huko.
15 Furthermore, before the fat [on the meat] was [cut off and] and burned [as a sacrifice to Yahweh], the servant of the priest would [sometimes] come to the man who was making the sacrifice and say to him, “Give me some meat [now to take] to the priest for him to roast! He wants raw meat; he does not want boiled meat.”
Tena, kabla ya kuteketeza mafuta, mtumishi wa kuhani alikuja, na kumwambia aliyekuwa akitoa dhabihu, “Tenga nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani; kwa sababu hataikubali ile ya kutokosa kutoka kwako, bali tu ile mbichi.”
16 If the man said to the servant, “Let the priests [cut off and] burn the fat first; then you can take what you want,” the servant would reply, “No, give it to me now; if you do not give it to me, I will take it forcefully!”
Ikiwa mtu atamwambia, “Wachome mafuta kwanza, na kisha uchukue kiasi utakacho.” Ndipo angesema, “Hapana, utanipatia sasa hivi; la sivyo; Nitaichukua kwa lazima.”
17 Yahweh considered that the young [sons of Eli] were committing a very great sin, because they were treating very disrespectfully the offerings that were being given to Yahweh.
Dhambi ya vijana hawa ilikuwa mbaya sana mbele za BWANA, kwa sababu waliidharau dhabihu ya BWANA.
18 As for Samuel, who was still a very young boy, he continued to do work for Yahweh, wearing a little sacred linen vest [like the Supreme Priest wore].
Lakini Samweli alimtumikia BWANA akiwa mdogo akivaa nguo ya naivera ya kitani.
19 Each year his mother made a [new] little robe for him and took it to him when she went up [to Shiloh] with her husband to offer a sacrifice.
Kila mwaka mama yake alimtengenezea kanzu dogo na kumletea, wakati wakija na mmewe kutoa dhabihu ya kila mwaka.
20 Then Eli would [ask God to] bless Elkanah and his wife, and he would say to Elkanah, “I hope/desire that Yahweh will enable your wife to give birth to other children, to take the place of the one whom she dedicated to Yahweh.” Then Elkanah and his family would return home.
Eli aliwabariki Elikana na mke wake na kusema, “BWANA akupatie watoto zaidi kwa mwanamke huyu kwa sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa BWANA.” Baadaye walirudi nyumbani kwao.
21 And Yahweh was very kind to Hannah, and enabled her to give birth to three [other] sons and two daughters. Their son Samuel grew up while he was doing work for Yahweh [in the Sacred Tent].
BWANA alimsaidia tena Hana, akawa amebeba mimba nyingine. Akazaa watoto watatu wa kiume na wa kike wawili. Wakati huo huo mtoto Samweli akakua akiwa mbele za BWANA.
22 Eli became very old. He often heard about all the [evil] things that his sons were doing to the Israeli people. He heard that they [sometimes] (slept with/had sex with) the women who worked at the entrance to the tent where [God] spoke to [his people].
Basi Eli alikuwa mzee sana, akayasikia yote ambayo watoto wake walikuwa wakiwafanyia Waisraeli wote, na jinsi walivyotembea na mwanamke aliyekuwa akitumika katika lango la hema ya kukutania.
23 He said to them, “(It is terrible that you do such things!/Why do you do such things?) [RHQ] Many people keep telling me about the evil things that you do.
Akawaambia, “Kwa nini mnafanya mambo hayo? Kwa maana nasikia matendo yenu maovu kutoka kwa watu hawa wote.”
24 My sons, stop it! The reports [about you] that the people who belong to Yahweh tell others are terrible [EUP]!
Sivyo hivyo, watoto wangu, maana hii ninayoisikia siyo taarifa njema. Mnawakosesha watu wa BWANA.
25 If one person sins against another person, God can (intercede/act as a referee) between them. But if someone sins against Yahweh, no one can [RHQ] (intercede/act as a referee) between them!” But Eli’s sons would not listen to what their father said. This was because Yahweh had decided [that someone should] them.
“Kama mtu mmoja akimkosea mwenzake, Mungu atamhukumu; Lakini mtu akimkosea BWANA, ni nani atakayemtetea mtu huyo?” Lakini hawakuitii sauti ya baba yao, sababu BWANA alinuia kuwaua.
26 The boy Samuel continued to grow up, and the things that he did pleased Yahweh and the people.
Yule mtoto Samweli aliongezeka umri, na kupata kibali kwa BWANA na kwa watu pia.
27 One day, a prophet came to Eli and told him, “This is what Yahweh has told me: ‘When your ancestors were slaves of the king of Egypt, I appeared to Aaron.
Kisha mtu wa Mungu akamwendea Eli na kumwambia, “BWANA asema, 'Je, sikujifunua mwenyewe kwa nyumba ya baba zako, walipokuwa Misri utumwani nyumbani mwa Farao?
28 From all the tribes of the Israeli people, I chose him [and his male descendants] to be priests for me. I appointed them to go up to my altar, to burn incense, to wear a sacred apron [as they worked] for me. And I declared that they could take [and eat some of the meat] that the Israeli people burned [on the altar].
Mimi nilimchagua yeye kutoka makabila yote ya Israeli awe kuhani wangu, apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba, na kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu. Niliwapa nyumba ya baba zako dhabihu zote za wana wa Israeli zilizotolewa kwa moto.
29 So why do you show disrespect for the sacrifices and offerings that I commanded [the people to bring] to me [RHQ]? You are honoring your sons more than you are honoring me, by allowing them to get fat from eating the best parts of all the sacrifices that the Israeli people bring to me!’
Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu na sadaka ambazo ninazitaka mahali ninapoishi? Kwanini unawaheshimu watoto wako kuliko mimi, kwa kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka ya watu wangu Israeli?'
30 “Therefore, this is what Yahweh, the God whom we Israelis [worship], declares: ‘I definitely promised that Aaron and his descendants would continue to serve [IDM] me forever.’ But now I declare this: ‘It will not continue like that! I will honor those who honor me, but I will despise those who despise me.
Maana, BWANA, Mungu wa Isareli, asema, niliahidi kwamba nyumba yako, na nyumba ya baba yako, yawapasa kwenda mbele zangu milele,' Lakini sasa BWANA asema. 'Mambo haya yapishe mbali. nami nisifanye hivi, maana nitawaheshimu wanaoniheshimu, bali wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.
31 Listen carefully! There will soon be a time when I will cause all the strong [young men] in your family to die. The result will be that no men in your family will [live long enough to] become old men.
Tazama, siku zinakuja nitakapoondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako, ili kwamba pasije kuwepo mtu mzee katika nyumba yako.
32 You will be distressed and envious as you see the blessings that I will give to [the other people in] Israel. And [I repeat that] no men in your family will ever live long enough to become old men.
Nawe utalitazama hangaiko katika makao yangu. Ingawa Israeli watapewa jambo jema, hapatakuwapo tena mtu yeyote mzee katika nyumba yako.
33 There is one of your descendants whom I will spare, and not prevent him from serving me as a priest. But he will become blind, and then he will always be sad and grieving. But all your other descendants will die violently.
Yeyote miongoni mwenu nisiye mwondoa kutoka madhabahuni pangu, Nitasababisha macho yenu yaanguke, na ita nitasababisha huzuni maishani mwenu. Wanaume wote waliozaliwa katika familia yako watakufa.
34 And your two sons, Hophni and Phinehas, will both die on the same day. And that will prove to you [that all that I have said will come true/happen].
Hii ndiyo itakuwa ishara kwako ambayo itawaijia watoto wako wakiume wawili, juu ya Hofni na Finehasi: Wote wawili watakufa siku moja.
35 ‘have chosen another man to be my priest. He is one who will serve me faithfully: He will do everything I want [DOU] him to do. And I will enable him to have many descendants [IDM] who will be priests and will always serve me by helping the king whom I will choose.
Nami nitamwinua juu kuhani wangu mwaminifu atakaye fanya kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu. Nami nitamjengea nyumba madhubuti; naye atakwenda mbele ya mfalme wangu mbarikiwa milele.
36 All of your descendants who remain alive will have to go to that priest and ask him to give them money and food, and they will each have to say, “Please allow me to help the other priests, in order that I may [earn some money to] buy some food.”’”
Kila mmoja aliyebakia nyumbani mwako atakuja na kusujudu mbele ya mtu huyo, akiomba kipande cha fedha na mkate mmoja, naye atasema, “Tafadhali uniajiri katika moja ya nafasi za kuhani ili niweze kula kipande cha mkate'”'

< 1 Samuel 2 >